Ghiti Milimo
JF-Expert Member
- Jul 18, 2011
- 5,136
- 7,655
Wadau, wote tunafahamu kuwa, Serikali(Rais)ilitangaza kuwa, kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi, itakuwa ni siku ya usafi kitaifa.
Wananchi, wakalipokea agizo hili, kwa mikono miwili. Lakini, ki-uhalisia, imekuwa ni kero kubwa!
Maisha kwa sasa yamekuwa magumu, wateja nao wamekuwa ni wa shida, patikana yao japo ni wachache, ni asubuhi, pamoja na mzigo wa kodi, lakini siku hii tunalazimishwa kufungua shughuri zetu saa nne na tano asubuhi! Ukifungua kabla ya hapo, unakamatwa!
Cha kushangaza, hao WAKAGUZI, wanachokagua, si USAFI, bali nani kafungua Duka/biashara yake kabla ya muda waliojipangia!
Mimi nawashauri, wangeturuhusu, tuwe tunafanya usafi kwa wakati wetu. Ila wao, wawe na muda maalumu, wa kukagua huo usafi. Kama mimi nitafanya usafi, usiku, alfajiri, hiyo iwe ni juu yangu!
Sina shaka hili tatizo lipo Nchi nzima! Mimi nipo Shinyanga mjini!
Wananchi, wakalipokea agizo hili, kwa mikono miwili. Lakini, ki-uhalisia, imekuwa ni kero kubwa!
Maisha kwa sasa yamekuwa magumu, wateja nao wamekuwa ni wa shida, patikana yao japo ni wachache, ni asubuhi, pamoja na mzigo wa kodi, lakini siku hii tunalazimishwa kufungua shughuri zetu saa nne na tano asubuhi! Ukifungua kabla ya hapo, unakamatwa!
Cha kushangaza, hao WAKAGUZI, wanachokagua, si USAFI, bali nani kafungua Duka/biashara yake kabla ya muda waliojipangia!
Mimi nawashauri, wangeturuhusu, tuwe tunafanya usafi kwa wakati wetu. Ila wao, wawe na muda maalumu, wa kukagua huo usafi. Kama mimi nitafanya usafi, usiku, alfajiri, hiyo iwe ni juu yangu!
Sina shaka hili tatizo lipo Nchi nzima! Mimi nipo Shinyanga mjini!