Ni upi mtungi bora wa gesi?

Ni upi mtungi bora wa gesi?

momara

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2019
Posts
463
Reaction score
491
Naomba kujua ndugu zangu. Kuna mitungi mingi sana sokon o-gas, mihan, taifa, manjis, lake, oryx n.k

Kuna mtu kanambia oryx inakaa muda mrefu ila mingine kidogo tu umeisha gas, pia amelinganisha bei ya oryx na nyingine akisema ipo juu kwakuwa ni bora kuliko mitungi mingne.

Sasa nawauliza ndugu zangu apa uzoefu wenu kweny hii mitungi ni kwel kuwa oryx ni bora zaid ya mingne?
 
Gesi ni ile ile LPG kwahio kama kuna utofauti ni wizi tu Mitungi ni Container na kilichomo ni kile kile...., unless hakijajazwa to capacity

Kwahio muulize vizuri alete upembuzi yakinifu wa Kwanini na sio kutoa maelezo ya jumla jumla
Ameegemea kweny bei za mitungi. Oryx ipo juu mno kulinganisha na mingne. Asa na mimi nahitaj mtungi ila bei ya January ndo nafelia apo
 
Gesi ni ile ile LPG kwahio kama kuna utofauti ni wizi tu Mitungi ni Container na kilichomo ni kile kile...., unless hakijajazwa to capacity

Kwahio muulize vizuri alete upembuzi yakinifu wa Kwanini na sio kutoa maelezo ya jumla jumla
Kwenye ujazaji ndio watu wanapopigwa
 
Hili suala la aina ya Gesi wewe angalia tu inayopatikana kwa urahisi ulipo

Oryx na Mihan huwa ndio zipo sana. Pick yoyote tu kati ya hizo mbili.

Binafsi Sina uzoefu na kampuni nyingine mana ni miaka sasa nipo loyal kwa Oryx
 
Unaponunua hakikisha unapima uzito wa gesi .ikipelea kilo 1 au 2 hiyo ni matumizi ya karibu wiki 1 unakua umepoteza.
 
Sasa unabisha nini?? Puma gas ni kampuni mpya wanatafuta soko hawawezi uza bei za Oryx au mihani kwa mara ya kwanza utanunua full 70k baada ya hapo bei za kujaza ni 55,000.
Sijabisha. Ila kila 30 + mtungi kwa 70k. Kilo 30? Eniwei sawa.

Otherwise unamaanisha mtungi wa kilo 15? Mana gesi mitungi standard hata kwa puma ni 6kg, 15kg na 38kg. Nadhani uliposema mtungi wa kilo 30 ndio haikua sawa
 
Sijabisha. Ila kila 30 + mtungi kwa 70k. Kilo 30? Eniwei sawa.

Otherwise unamaanisha mtungi wa kilo 15? Mana gesi mitungi standard hata kwa puma ni 6kg, 15kg na 38kg. Nadhani uliposema mtungi wa kilo 30 ndio haikua sawa
Hivi hizi kg ni baada ya kujaza gesi au uzito wa mtungi maana sielewi
 
Hivi hizi kg ni baada ya kujaza gesi au uzito wa mtungi maana sielewi
Kg tunazoongelea ni ujazo wa gesi 6, 15, 38 ni gesi.

Ila kila mtungi huwa unandikwa uzito kamili wa mtung empy hapo unaweza Kuhakiki kama gesi iliyopo ni kiwango sahihi
 
Back
Top Bottom