Ni Ugonjwa au uchafu?

NGULI

JF-Expert Member
Mar 31, 2008
4,803
637
Nilikuwa najiuliza kila saiku kwa nini vijana wengi wakitoka tu chuo Mungu akiwajalia kazi wakikopa tu cha kwanza gari nilidhani ni ubishoo kumbe ni swala la msingi achana na adha ya usafiri kuwa wa shida pia mazingira ndani ya gari yanasikitisha.

Kwa mfano utoke posta mchana uwe unaelekea feri au mbagala au hata basi za mwenge usimame umkute mtu aliyeshiba vizuri/mnene mbele yako then anyooshe mikono kujishika kwenye bomba au kiti harufu kali ya kwapa itakayotoka utatamani ushuke utembee kwa miguu. Je huwa watu hawaogi au ni ugonjwa unaohitaji dawa? Kondacta akiwa anapita kukusanya nauli ndio balaaaa kabisa wengine utazani wanatembea na jalala akinyoosha mkono tu unatoa hela hapo hapo hata chenchi hutamani irudi.

Na kuna wengine wanaotoa harufu mwili mzima mpaka viatu japo amevivaa sijui akivua nini kitatokea. Inakera sana,
 
Ni hulka tu ya uchafu njia za huko wala sio ugonjwa. Mbona magari yanayoenda Masaki wadereva na makonda wao ni wasafi.
 
Hahaha! Kama limetokea feri, usisahau na shombo la samaki hasahasa kwa ma DCM yaendayo Mbagala.
 
Hahahahaha joto kali mpwa unafikiri huyo haogi? Anaoga sana asubuhi na jioni sema wengi wa vijana hawapendi kutumia manukato makali ya kuficha harufu yeye akisha oga basi ndo imetoka hiyo kikwapa kina tabia ya kuchacha na hili joto kikichacha akiinua mkono mtakimbiana utahisi kajamba.
 
Those guys dont love their job!

Na ukitaka kuiona kazi yako mbaya, basi anza kuidharau wewe mwenyewe!

Mimi kila siku huwa najisemea kuwa, hivi hawa makonda wangekuwa wanajitahidi wavae hadi tai siku mojamoja, ndhani hata trafiki wasingewashikashika, maana wangeonekana wastaarabu japo kwa minimum grade!
 
Hahahahaha joto kali mpwa unafikiri huyo haogi? Anaoga sana asubuhi na jioni sema wengi wa vijana hawapendi kutumia manukato makali ya kuficha harufu yeye akisha oga basi ndo imetoka hiyo kikwapa kina tabia ya kuchacha na hili joto kikichacha akiinua mkono mtakimbiana utahisi kajamba.

Ha ha ha ha,

Inabidi watu wa manukato wagawe bure kama promo ili wazoee jamani hali ni mbaya, mitaro michafu watu wanatema tuishi wapi sasa?
 
Those guys dont love their job!

Na ukitaka kuiona kazi yako mbaya, basi anza kuidharau wewe mwenyewe!

Mimi kila siku huwa najisemea kuwa, hivi hawa makonda wangekuwa wanajitahidi wavae hadi tai siku mojamoja, ndhani hata trafiki wasingewashikashika, maana wangeonekana wastaarabu japo kwa minimum grade!

PJ hata mie nashangaa watz wanavyopenda kuiga wanayoyaona kwenye runinga! Hawajaona tu madereva na makonda wa majuu wanavyotinga suit na tie? wako bling bling!
Ila joto la bongo nalo mhhh!Labda kama magari yatakuwa na AC lakini bei nayo ikipanda watz watakubali?
 
Nilikuwa najiuliza kila saiku kwa nini vijana wengi wakitoka tu chuo Mungu akiwajalia kazi wakikopa tu cha kwanza gari nilidhani ni ubishoo kumbe ni swala la msingi achana na adha ya usafiri kuwa wa shida pia mazingira ndani ya gari yanasikitisha.

Kwa mfano utoke posta mchana uwe unaelekea feri au mbagala au hata basi za mwenge usimame umkute mtu aliyeshiba vizuri/mnene mbele yako then anyooshe mikono kujishika kwenye bomba au kiti harufu kali ya kwapa itakayotoka utatamani ushuke utembee kwa miguu. Je huwa watu hawaogi au ni ugonjwa unaohitaji dawa? Kondacta akiwa anapita kukusanya nauli ndio balaaaa kabisa wengine utazani wanatembea na jalala akinyoosha mkono tu unatoa hela hapo hapo hata chenchi hutamani irudi.

Na kuna wengine wanaotoa harufu mwili mzima mpaka viatu japo amevivaa sijui akivua nini kitatokea. Inakera sana,

lakini si kila anaemaliza chuo ananunua gari!mwingine ananunua TUKUTUKU:D
 
lakini si kila anaemaliza chuo ananunua gari!mwingine ananunua TUKUTUKU:D

Ha ha ha aha ha
icon10.gif
,
icon10.gif
nimecheka hapa ofisini hadi watu wameniona kichaa, kwa atakayekuelewa atacheka sana ngoja XSPIN na Fidel80 warudi hapa.
 
Hahahahaha joto kali mpwa unafikiri huyo haogi? Anaoga sana asubuhi na jioni sema wengi wa vijana hawapendi kutumia manukato makali ya kuficha harufu yeye akisha oga basi ndo imetoka hiyo kikwapa kina tabia ya kuchacha na hili joto kikichacha akiinua mkono mtakimbiana utahisi kajamba.


Ukishaoga vizuri unahitaji kuficha harufu ipi tena kwa manukato makali?

Au una maana kutumia anti-perspirants/deodorants..... hizi ni za kukuweka ubaki fresh lakini siyo kufunika uvundo.
 
Ukishaoga vizuri unahitaji kuficha harufu ipi tena kwa manukato makali?

Au una maana kutumia anti-perspirants/deodorants..... hizi ni za kukuweka ubaki fresh lakini siyo kufunika uvundo.


Da ni kweli kwa sababu mtu akiwa anatema harufu kali then achanganye na manukato mchnganyiko utakao tokea hapo utakuwa worse.
 
Ha ha ha aha ha
icon10.gif
,
icon10.gif
nimecheka hapa ofisini hadi watu wameniona kichaa, kwa atakayekuelewa atacheka sana ngoja XSPIN na Fidel80 warudi hapa.
sasa mpwa unacheka halafu unasahau SENKSI!mpwa bwana!
vipi unalizungumziaje tukutuku?hasa likiwa halina breki zote na linatoa sauti kubwa?
 
sasa mpwa unacheka halafu unasahau SENKSI!mpwa bwana!
vipi unalizungumziaje tukutuku?hasa likiwa halina breki zote na linatoa sauti kubwa?

Halafu nyumba zenye huruma za kusimamia zikakosekana. Halafu nyuma uwe umepakia mziki wa Carmel! Hahaha!
 
lakini si kila anaemaliza chuo ananunua gari!mwingine ananunua TUKUTUKU:D

Ha ha ha aha ha, nimecheka hapa ofisini hadi watu wameniona kichaa, kwa atakayekuelewa atacheka sana ngoja XSPIN na Fidel80 warudi hapa.

HAHAAAAA, TUKUTUKU LINASEVU SANA, wataalam wanasema linaadvanteji nyingi kuliko motokaa, kasoro kwenye mvua!, asee unakumbuka ule MSHIKAKI wa siku ile?, duh.
 
nilikuwa najiuliza kila saiku kwa nini vijana wengi wakitoka tu chuo mungu akiwajalia kazi wakikopa tu cha kwanza gari nilidhani ni ubishoo kumbe ni swala la msingi achana na adha ya usafiri kuwa wa shida pia mazingira ndani ya gari yanasikitisha.

Kwa mfano utoke posta mchana uwe unaelekea feri au mbagala au hata basi za mwenge usimame umkute mtu aliyeshiba vizuri/mnene mbele yako then anyooshe mikono kujishika kwenye bomba au kiti harufu kali ya kwapa itakayotoka utatamani ushuke utembee kwa miguu. Je huwa watu hawaogi au ni ugonjwa unaohitaji dawa? Kondacta akiwa anapita kukusanya nauli ndio balaaaa kabisa wengine utazani wanatembea na jalala akinyoosha mkono tu unatoa hela hapo hapo hata chenchi hutamani irudi.

Na kuna wengine wanaotoa harufu mwili mzima mpaka viatu japo amevivaa sijui akivua nini kitatokea. Inakera sana,


ni ugonjwa!
 
HAHAAAAA, TUKUTUKU LINASEVU SANA, wataalam wanasema linaadvanteji nyingi kuliko motokaa, kasoro kwenye mvua!, asee unakumbuka ule MSHIKAKI wa siku ile?, duh.

Si utani; Biashara ya foleni unaitupilia mbali. hakuna kero mbaya kama foleni. We na kistaleti chako unatoka home kuwahi kikao sinza unamkuta mzee wa tukutuku kashatafuna kokoto kadhaa na taska ya nne. Hahahaha!
 
Halafu nyumba zenye huruma za kusimamia zikakosekana. Halafu nyuma uwe umepakia mziki wa Carmel! Hahaha!
huyu mpwa anasifia magari anasahau tukutuku bana!wakati chawote tukipaki pale tunaonekana kama miungu-watu
 
Si utani; Biashara ya foleni unaitupilia mbali. hakuna kero mbaya kama foleni. We na kistaleti chako unatoka home kuwahi kikao sinza unamkuta mzee wa tukutuku kashatafuna kokoto kadhaa na taska ya nne. Hahahaha!
hapa tukutuku linakuwa kama JEEP!linayeya vibaya
 
Back
Top Bottom