MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,244
- 7,966
Wakuu hebu tuliweke sawa hili!
Hivi tunapolilia tume huru ya Uchaguzi bila katiba mpya iili mambo yakae sawa hasa wakati wa uchaguzi tunamaanisha nini? Inawezekanaje tume ya Uchaguzi iwe huru? Kwani muundo wa tume utakua chini ya nani kwa katiba ya sasa?
Kwa katiba yetu hii Rais ndiye mteule wa Viongozi wote wakuu wa tume kuanzia Mwenyekiti wake hadi wakurugenzi wote, tena mbaya zaidi kwa wakati huu teuzi za wakuu wengi wa Idara za Serikali zinaangalia makada wa CCM. Hivyo bila kumuondolea Rais mamlaka ya kua mteuzi wa maafisa wote wa tume hatuwezi kua na tume huru.
Tusililie hili bila kuliangalia kwa umakini mkubwa, mahitaji yetu ili kulibadili taifa hili ni kupunguza mamlaka makubwa yaliyoko Ofisi ya Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama tawala.
Tume ya taifa ya Uchaguzi inatakiwa kuachana na utaratibu wa kutumia wakurugenzi wa halmashauri kua wasimamizi wa chaguzi mbali mbali nchini, viongozi hawa wengi wao ni makada wa CCM kwahiyo lazima kuwe na conflict of interest kwa kiasi kikubwa. Tume ni taasisi kubwa, iajiri maafisa wengi hasa vijana waliohitimu vyuo vikuu kwa masomo ya sheria,siasa na katiba na watapakae kila mkoa na wilaya ili kusimamia Uchaguzi. Mbona TAKUKURU wameweza, mbona taasisi zingine zilizoanzishwa hivi karibuni zina nguvu kazi za kutosha lakini NEC wanashindwaje? Au ni makusudi? Hili suala ni la kutazwa kwa nguvu zote.Upinzani nchini hebu amkeni acheni kulala na kulialia.
Ni tume au katiba? Kipi muhimu zaidi?
Hivi tunapolilia tume huru ya Uchaguzi bila katiba mpya iili mambo yakae sawa hasa wakati wa uchaguzi tunamaanisha nini? Inawezekanaje tume ya Uchaguzi iwe huru? Kwani muundo wa tume utakua chini ya nani kwa katiba ya sasa?
Kwa katiba yetu hii Rais ndiye mteule wa Viongozi wote wakuu wa tume kuanzia Mwenyekiti wake hadi wakurugenzi wote, tena mbaya zaidi kwa wakati huu teuzi za wakuu wengi wa Idara za Serikali zinaangalia makada wa CCM. Hivyo bila kumuondolea Rais mamlaka ya kua mteuzi wa maafisa wote wa tume hatuwezi kua na tume huru.
Tusililie hili bila kuliangalia kwa umakini mkubwa, mahitaji yetu ili kulibadili taifa hili ni kupunguza mamlaka makubwa yaliyoko Ofisi ya Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama tawala.
Tume ya taifa ya Uchaguzi inatakiwa kuachana na utaratibu wa kutumia wakurugenzi wa halmashauri kua wasimamizi wa chaguzi mbali mbali nchini, viongozi hawa wengi wao ni makada wa CCM kwahiyo lazima kuwe na conflict of interest kwa kiasi kikubwa. Tume ni taasisi kubwa, iajiri maafisa wengi hasa vijana waliohitimu vyuo vikuu kwa masomo ya sheria,siasa na katiba na watapakae kila mkoa na wilaya ili kusimamia Uchaguzi. Mbona TAKUKURU wameweza, mbona taasisi zingine zilizoanzishwa hivi karibuni zina nguvu kazi za kutosha lakini NEC wanashindwaje? Au ni makusudi? Hili suala ni la kutazwa kwa nguvu zote.Upinzani nchini hebu amkeni acheni kulala na kulialia.
Ni tume au katiba? Kipi muhimu zaidi?