Ni Taifa gani analolitetea sheikh Farid?

gollocko

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
2,945
2,275
""Ni kweli siku tatu za vurugu mimi sikulala nyumbani, ila sitaji nilipokuwa nikilala…nachukua tahadhari, unajua sisi hatuna jeshi wala silaha, ila linaloandikwa likufike litakufika tu. Heri mimi nife nikiwa jasiri kuliko kuacha taifa langu likiangamia.”

Haya ni maneno aliyozungumza Sheikh Farid mara baada ya kuachiwa kwa dhamana hapo juzi.Lakini tukirudi nyuma tutakumbuka kuwa hawa wakina Sheikh Farid walitumiwa sana na Maalim Seif Sharif Hamad katika kukikampenia chama cha CUF na mara zote baada ya chaguzi za Zanzbar kwisha na CUF kushindwa walikuwa mstari wa mbele kupinga matokeo huku wakiandaa maandamano ya kuwalaani waunguja(CCM) kwa kuwapoka ushindi wapemba(CUF).

Hii ilifikia mpaka wakina Sheikh Farid kuwahamasisha wapemba kuwatenga waunguja huku wakipakaza vinyesi kwenye nyumba zao na hata kuviweka kwenye visima vya maji wayatumiayo waunguja(rejea matukio ya vurugu baada ya uchaguzi mkuu wa 2005).
Baada ya kupata serikali ya umoja wa kitaifa na wapemba kuongoza serikali hiyo sasa wakina Sheikh Farid wamekuja na hoja nyingine ya kuupinga muungano.
Hapa nashindwa kuwaelewa wakina Sheikh Farid wanatetea Taifa gani? La wapemba, la waunguja au la Zanzibar?
 
Katiba ya Zanzibabar imetungwa hivi karibuni na ilikiuka katiba ya Tanzania kwa kutamka wazi kuwa Zanzibabar ni nchi na ikiainisha mipaka yake. Kwa kuwa viongozi tulio nao sasa ni watu wasiotaka kujihusisha katika maamuzi magumu walijifanya kama kwamba hawaoni katiba mama ikivunjwa. Matokeo ya kuvunjwa kwa katiba ndiko sasa kunakotoa ujasiri wa watu kuinuka na kudai mambo mbali mbali kama nchi inayojitegemea. Katiba ya Muungano haina tena uhalali wa kuyahoji makundi yaliyopo ndani ya nchi ya Zanzibabar kwa kuwa imeishakatwa makali na katiba mpya za Zanzibabar. Kwa kifupi machafuko ya Zanzibabar ni matokeo ya watawala tulio nao sasa kukwepa wajibu wao wa kiutawala.
.
 
""Ni kweli siku tatu za vurugu mimi sikulala nyumbani, ila sitaji nilipokuwa nikilala…nachukua tahadhari, unajua sisi hatuna jeshi wala silaha, ila linaloandikwa likufike litakufika tu. Heri mimi nife nikiwa jasiri kuliko kuacha taifa langu likiangamia."

Haya ni maneno aliyozungumza Sheikh Farid mara baada ya kuachiwa kwa dhamana hapo juzi.Lakini tukirudi nyuma tutakumbuka kuwa hawa wakina Sheikh Farid walitumiwa sana na Maalim Seif Sharif Hamad katika kukikampenia chama cha CUF na mara zote baada ya chaguzi za Zanzbar kwisha na CUF kushindwa walikuwa mstari wa mbele kupinga matokeo huku wakiandaa maandamano ya kuwalaani waunguja(CCM) kwa kuwapoka ushindi wapemba(CUF).

Hii ilifikia mpaka wakina Sheikh Farid kuwahamasisha wapemba kuwatenga waunguja huku wakipakaza vinyesi kwenye nyumba zao na hata kuviweka kwenye visima vya maji wayatumiayo waunguja(rejea matukio ya vurugu baada ya uchaguzi mkuu wa 2005).
Baada ya kupata serikali ya umoja wa kitaifa na wapemba kuongoza serikali hiyo sasa wakina Sheikh Farid wamekuja na hoja nyingine ya kuupinga muungano.
Hapa nashindwa kuwaelewa wakina Sheikh Farid wanatetea Taifa gani? La wapemba, la waunguja au la Zanzibar?

Luka 19:27 Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu."`

19:28 Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
 
Back
Top Bottom