ni sahihi kutumia chenji ya WEF kugida na kula?

ni sahihi kutumia chenji ya WEF kugida na kula?

Ngambo Ngali

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2009
Posts
3,517
Reaction score
1,367
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku cheti maalumu Katibu Mkuu Kiongozi Philemon Luhanjo kwa kutambua mchango wake katika kufanikisha kwa ufanisi mkubwa kufanyika kwa mkutano wa World Economic Forum uliofanyika jijini Dar es Salaam wiki iliyopita.Katika hafla hiyo wadau wengine wakiwamo mashirika mbalimbali,kampuni na watu binafsi nao walitunukiwa vyeti kwa kufanikisha mkutano huo wa kimataifa.

source: michuziblogspot

inaelekea chenji za mkutano WEF zilitumika kuandaa hicho chakula cha jioni. Kwa nini hela hizo zisitumike kuziba mashimo ya barabara za dar es salaam ili angalau foleni ipungue? Ni kitu gani cha ziada hawa waandaaji walifanya??? Hawakutoa hela, walifanya kazi kama majukumu yao yanavyowataka at most walilipwa maofisini kwao kwa kutofanya kazi walioajiwa kufanya na badala yake waliconcentrate na maandalizi ya mkutano.
 
Kwa kweli sio sahihi,nilipoona jana kwenye taarifa ya habari nilishangazwa sana na hili..Hivi kwani haikuwezekana kumpa hiyo tuzo kwa staili nyingine?mpaka hafla iandaliwe?Pesa zinatumika hovyo wakati kuna wengine wanakufa kwa kukosa dawa mahospitalini...
 
Kwa kweli sio sahihi,nilipoona jana kwenye taarifa ya habari nilishangazwa sana na hili..Hivi kwani haikuwezekana kumpa hiyo tuzo kwa staili nyingine?mpaka hafla iandaliwe?Pesa zinatumika hovyo wakati kuna wengine wanakufa kwa kukosa dawa mahospitalini...

Unaweza kugundua kuwa hela iliyoingia mkutanoni ni ndogo sana nyingi kwa wajanja hivi haiwezekani kuundwa kamati kama Uganda kuchunguza matumizi ya CHOGAM? Nina uhakika hafla hii haikuwa necessary under the circumstatnces.
 
jamani mnaumiza vichwa bure, hawa watu hawana akili kabisa kabisa dawa ni kumtoa kikwete automatically huyo katibu wake mamvi nae atatoka, mmeshamsema kwenye upendeleo, kaonekana kwenye kashfa zote, watapongezana vipi kabla ya ku assess kama kweli huo mkutano ulikua na mafanikio ama la, wametumia vigezo gani haswa? wezi wakubwa hao wasiwaumize kichwa dawa ni kama ile ya harambee ya Kilimanjaro. Cheap Roadshow government, hivi wameshaona Kenya, Uganda, Rwanda, hata marekani na uingereza wakifanya hivyo vituko? ndio tatizo ya kujaza ikulu watu wenye pass degrees kwa kupendelea kama ana ubavu hizo kazi zifanyiwe proper vetting ama kutangazwa tuone kama kuna atakaerudi, wanafanya mchezo na maisha ya watanzania wanataka tumwage damu hebu tuondoe huo uchafu haraka jamani.
 
Jamani mwee! ni lini mchango wa harusi ukatumika kujenga msingi wa nyumba?
 
Back
Top Bottom