Ni rasmi mechi za Yanga na Simba first leg kuchezwa usiku

vibertz

JF-Expert Member
Mar 15, 2022
1,365
2,501
Wawakilishi wa Tanzania katika mashindano ya CAF champions league Simba na Yanga, watakuwa na kibarua kigumu cha kumeenyana na miamba ya soka la Africa. Simba watatangulia kucheza siku ya Ijumaa tarehe 29 saa tatu usiku na Yanga kufuatia kucheza siku ya Jumamosi ya tarehe 30 muda wa saa tatu usiku.

Yanga kucheza usiku mechi ya kimataifa sio jambo ngeni kwasababu ni kawaida kwao kucheza mechi zao usiku, na hata Belouizdad alipigwa usiku ni tofauti na ilivyozoeleka kwa timu ya Simba ambapo jambo lake kwa mwarabu huwa ni jioni. Wydad, Soura, Al Ahly hawa wote walikutana na kipigo cha jioni ila safari hii Al Ahly anakuja kucheza na Simba saa tatu ya usiku

Kila la kheri Tanzania, atakayejipanga vyema ataondoka na matokeo mazuri, muda hauchezi mpira.
 
Hivi MASHABIKI wa YANGA mnatoaga hata sekunde kufanya kazi za ujenzi wa Taifa kutwa nzima mnawazaga YANGA tuuu
Umeumizwa na lipi? Mbona humu tokea droo itoke, mashabiki wenzio wa Simba wamefululiza minyuzi humu kuikatisha tamaa Yanga lakini mbona hukuandika hayo? Hasira zako peleka huko
 
Hivi MASHABIKI wa YANGA mnatoaga hata sekunde kufanya kazi za ujenzi wa Taifa kutwa nzima mnawazaga YANGA tuuu
Shida kubwa utakua nayo wewe manake kwanza umekua mchangiaji wa kwanza kwenye huu uzi hii Ina maana Kila baada ya dakika tano wewe unazurura humu kutazama nyuzi mpya.
 
Simba watatangulia kucheza siku ya Ijumaa tarehe 29 saa tatu usiku na Yanga kufuatia kucheza siku ya Jumamosi ya tarehe 30 muda wa saa tatu usiku.

Simba wasisahau kuroga dozi ya siku 2 iwasaidie Uto pia...
 
Na wachezaji wa timu ya taifa watarudi tare 27 baada ya kuungaunga ndege ,Wasimba watakuwa na siku moja ya kujiandaa tar 29 mechi huku Yanga wakiwa na siku mbili za kujiandaa tarehe 30 mechi.

Hapo ndipo muone awamu hii TFF wamezingua.
 
Na wachezaji wa timu ya taifa watarudi tare 27 baada ya kuungaunga ndege ,Wasimba watakuwa na siku moja ya kujiandaa tar 29 mechi huku Yanga wakiwa na siku mbili za kujiandaa tarehe 30 mechi.

Hapo ndipo muone awamu hii TFF wamezingua.
Vilabu viombe wachezaji wao wäbakizwe. Al Ahly mbona wameomba kule Misri
 
Timu tunayo ndo mana tunapata nguvu ya kuiwaza.

Sasa wewe kolo timu lako bovu lililosheheni wastaafu utapata wapi nguvu ya kuiwaza?
Timu unayo, ajira hauna, pesa hauna, unanuka ufukara Ila una Muda wa kuiwaza timu yako eti una timu..una timu wewe? Gsm na hersi ndio wenye timu, wao ndio.wanaifaidi kwa kupata mipesa. Pole Sana dogo.
 
Timu unayo, ajira hauna, pesa hauna, unanuka ufukara Ila una Muda wa kuiwaza timu yako eti una timu..una timu wewe? Gsm na hersi ndio wenye timu, wao ndio.wanaifaidi kwa kupata mipesa. Pole Sana dogo.
Kolo mbona umefura kwa hasira?
 
Wawakilishi wa Tanzania katika mashindano ya CAF champions league Simba na Yanga, watakuwa na kibarua kigumu cha kumeenyana na miamba ya soka la Africa. Simba watatangulia kucheza siku ya Ijumaa tarehe 29 saa tatu usiku na Yanga kufuatia kucheza siku ya Jumamosi ya tarehe 30 muda wa saa tatu usiku.

Yanga kucheza usiku mechi ya kimataifa sio jambo ngeni kwasababu ni kawaida kwao kucheza mechi zao usiku, na hata Belouizdad alipigwa usiku ni tofauti na ilivyozoeleka kwa timu ya Simba ambapo jambo lake kwa mwarabu huwa ni jioni. Wydad, Soura, Al Ahly hawa wote walikutana na kipigo cha jioni ila safari hii Al Ahly anakuja kucheza na Simba saa tatu ya usiku

Kila la kheri Tanzania, atakayejipanga vyema ataondoka na matokeo mazuri, muda hauchezi mpira.
mechi na Raja Casablanca walicheza usiku 0-3
 
Back
Top Bottom