Ni nini hasa uspesho wa iPhone?

Baada ya kupitia comment zote, nilichokiona wengi tunanunua matoleo ya simu kwa kufuata mkumbo tu. Wengi wetu matumizi yetu yanahitaji simu isiyozidi 100k, iwe na uwezo wa kupiga na kupokea, kutuma sms, kupiga picha, internet na isikose radio na calculator.

Kiduku Lilo atakuja kuwapa tofauti ya chombo cha mawasiliano na simu.
 

Mkuu tuwekee screenshot ya kua watumia iphone 7 kwanza...maana wakuta unaongeleaa na hujawai hata itumiaa
 
Niko na dunduliza visenti mwezi wa saba nijipatie kiapple na mm
Tuache masihara brand ya mUsa huwez kulinganisha na hiz brand za hovyo hovyo
Kwani Samsung ni brand ya MLatino?
 

leo nakutana na comment zinanizonivunja mbavu
 
af unakuta una iphone 5 sim inauzwa laki moja
 
leo nakutana na comment zinanizonivunja mbavu

Kweli lakini, mtu mbwembwe nyiiiiingi, kila toleo la simu likitoka yumo, unajiuliza huyu mtu anaitumia simu yake kwa mambo gani hasa hasa? Utakuta facebook, IG na magroup ya WhatsApp.

Sasa hivyo vitu si vinahimiliwa na simu ya 60,000/-. Tunapenda maisha ya kuigiza sana. Mie mradi nna mawasiliano sijali kabisa wengine wanasemaje kuhusu simu yangu.
 
Raha ya simu uicontrol.sio simu umenunua kwa pesa yako then.ukitaka kushea kitu via bluetooth inakataa na options nyengne nyengine kibao.hvo sion cha ajabu kwenye iphone zaid ya security system yake tu.poor iphone.
 
iPhone ni brand. Angalia sosho media macelebrity wametupia mirror selfie inaonyesha camera 3 pale nyuma. Simu inauzwa 4M kama huna pesa tulia tu. Hata wenye iphone 6, 7, 8 wanaonekana washamba tu. Saivi iphone sio lile tunda tu bali una camera ya muundo gani
.
Mimi natamba na S9+ yangu sina presha
 
I phone ni overrated brand na sioni kama wana ubunifu wowote nashangaa watu wanavyohaha kisa camera tatu wakat kuna simu ina camera tano na ilitoka tangu january


ila kwa iphone sijaona jipya kuhusu suala la camera tatu maana kafanya kitu ambacho wenzake wamefanya zaman sana

 
iCloud
Find IPhone
Sjui znapatkana kule? Manake mi nlitokea Alcatel nlipofika hapa skuamasika kubanduka.
 
Kuwakoga mademu na masela huko Twitter....
 
Sababu ya msingi ni na. 4 tuu the rest pumba tupu...
 
Kila mtu na vipaumbele vyake,mimi nina tecno w4 ila ninamiliki nyumba kali na mwenzangu ana iPhone ya milioni 4 ila anakula na kulala alipoolewa dada ake.SUALA NI VIPAUMBELE TUSILAUMINE!!

Sent from my TECNO_W4 using JamiiForums mobile app
 
Nikifikiria haya majukumu niliyonayo, hata nikipokea zawadi ya hiyo Iphone nitaiuza tu
 
Samsung matoleo 20? Unaota mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…