Ni nini Chanzo cha jina Tanganyika?

Ni nini Chanzo cha jina Tanganyika?

Matunda safi

Member
Joined
May 30, 2025
Posts
31
Reaction score
61
Ndugu wana JF na watanzania wote mliopo humu poleni na majukumu hasa ya kulijenga Taifa, naomba kuuliza maswali yafuatayo:

1/Je chanzo cha jina Tanganyika ni nini?

2/Je mgunduzi wa kwanza wa jina hili ni nani? Na alitokea nchi gani?

3/Wakati anagundua ilikuwa mwaka gani?

JF ni sehemu bora kwa elimu na maarifa hivo nawasilisha kwa wanahistoria kwaajiri yakuelimika zaidi
 
Chanzo chake ni kunya kisiwani uje ukute bara.
Ndio maana udongo umekosekana waliochimba choo hawapo.
 
Mkuu si nyika ya tanga! once upon a time wajuaji walikuwa tanga hivyo nisawa nakusema waliona kwingine ni nyika .basi usihangaike sana tumia mawazo yangu
 
Nahisi chanzo chake ni DANGANYIKA.
Maana yake watu wanaodanganywa Kila siku na viongozi walio madarakani.
 
Limeshakua discussed sana humu


Huo uzi kuna majibu mengi ila kifupi ni muunganiko wa Tanga na Nyika.

Mkoa wa Tanga miaka na miaka ni Town, Zamani Tanga ulikua mji mkubwa kuliko hata Dar, pia ukirudi historia nyuma toka Raphta eneo hilo lilikua ni mjini,

So Tanga Nyika ikimaanisha Tanga hapo mjini na Nyika zake yaani maeneo mengine ya bara.
 
Tanga+nyika
Tanga + Nyika, Maana yake kwanza kabisa ni viumbe aina ya samaki wanaopatikana katika ziwa Tanganyika hivyo Tanga ni samaki pia na Nyika ni samaki ila wana sifa ya kipekee na hawapikiki bila maagano kati ya hao mmoja anao umeme kama ulinzi wake na mwingine anayo nguvu ya ushambuliaji wa kupandisha kwa mbali kabla haujafikia ndiyo maana ziwa Tanganyika lilivyo na ndiyo chimbuko la nchi kuitwa Tanganyika
 
Ndugu wana JF na watanzania wote mliopo humu poleni na majukumu hasa ya kulijenga Taifa,naomba kuuliza maswali yafuatayo:

1/je chanzo cha jina Tanganyika ni nini?

2/je mgunduzi wa kwanza wa jina hili ni nani? na alitokea nchi gani?

3/wakati anagundua ilikuwa mwaka gani?

JF ni sehemu bora kwa elimu na maarifa hivo nawasilisha kwa wanahistoria kwaajiri yakuelimika zaidi
Mwaka 1885, Wajerumani walifika huku bongo na kuanza kuganda Tanga – pale ndipo walipoweka kambi yao kubwa, yaani headquarters. Basi m Tanga ikawa kama base yao ya operations.

Sasa walipokua wanapanua himaya yao kuelekea maeneo ya ndani ya nchi – yaani porini, vijijini, na kila kona – walikuwa wanaita hiyo sehemu yote kuwa ni "nyika", ambayo ni Kiswahili ya maeneo ya pori au ya bara.

Sasa weka pamoja:
🧠 Tanga (mji wao mkuu) + Nyika (maeneo ya porini yaliyowazunguka) = Tanganyika.

Kwa hiyo, jina Tanganyika lilikuwa kama kusema, “Tanga pamoja na maeneo yote ya bara yanayoizunguka.” Noma siyo?

Lakini pia kumbuka, kwa Wajerumani wao walikuwa wanaita hii sehemu yote kuwa ni:
🇩🇪 Deutsch-Ostafrika – yaani “German East Africa.”

Halafu ikaja Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, mwaka 1914–1918, Wajerumani walipigwa chini na Waingereza wakachukua hii himaya. Ila jina la Tanganyika likabaki hadi tulipopata uhuru mwaka 1961.
 
Back
Top Bottom