Ni mwanachama gani wa CCM anayeunga mkono UKAWA

Ni mwanachama gani wa CCM anayeunga mkono UKAWA

Ba E's

Senior Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
145
Reaction score
52
Hbr za leo wakuu,

Baada ya watetezi wa katiba ya wananchi (UKAWA) kujitoa jana baada ya kuchoshwa na mwenendo mzima wa matusi yanayoendelea bungeni yakitolewa na wanaotaka itengenezwe katiba ya CCM kwa mgongo wa katiba ya wananchi.

Napenda kujua kama baadhi ya wabunge wanaojitambua wa CCM akina Kangi Lugora, Deo Filikunjombe, Luhaga Mpina, Esther Bulaya, Abdala Mtutura, je na wao wameamua kuwasaliti wananchi au wamo bungeni kama passive listeners?
 
Mh. Makonda, Ezekiel maige, Michael laizer, Samwel Sitta, Ester Bulaya, Job Ndugai, Mbunge wa Mwibara, Mbunge wa Skonge, Abdul Jumbe, Pius Msekwa, Fulukunjombe, Adam Malima, Getrude Lwakatare, Fredrick Sumaye, hao kwa uchache
 
Napelile anaihusudu sana ukawa kwani haachi kuitajataja
 
Ili kupata mawazo yaliyo sawa, inabidi ututajie wabunge wa Chadema, NCCR Mageuzi na CUF ambao wamebaki Bungeni ili kuonesha demokrasia ya vyama hivi vinaruhusu mawazo kinzani au wanalazimishana? Mfano kuna chama kama DP Mtikila ametoka lakini mjumbe mmoja ambaye mawazo yake hayafungamani na Mtikila hakutoka pia kuna vya TPP maendeleo, TLP, NLD, nk hao hawakutoka. Sasa usione aibu kusema chama chako hakina demokrasia hata ktk maoni tu mtu anaitwa msaliti wakati CCM hao uliowataja wapo huru na kidemokrasia!
 
Back
Top Bottom