Ni migomo, maandamano bila kikomo

Ni migomo, maandamano bila kikomo

Itafika wakati mtakuwa wapinzani ndani ya nchi hii... huo wakati ukifika wengi wenu mtaishia jela na kupigwa mawe na wananchi! Lakini pia ushahidi wa kimazingira unaonesha kuwa CCM itasambaratika punde baada ya kung'atushwa madarakani!

Mafanikio hayo unayojivunia si sawa na utajiri wa nchi hii... mnapingwa na kukosolewa kwa sababu mmeshindwa kufanya makubwa ukilinganisha na dhamana mlopewa!

By the way; hapa napoteza muda tu make naongea na shabiki anayemsifia mchezaji kwa kupiga chenga na kufunga magoli... sijuhi alitegemea mchezaji wake alale usingizi uwanjani...???
Kusimamia maendeleo ni jukumu la serikali wala haitakiwi kupongezwa; ila inaposhindwa kusimamia vizuri rasilimali za taifa na kuendekeza/kubariki rushwa na ufisadi ni lazima wenye busara wapaze sauti!

Mungu anipe miaka mingi nije nikione kipindi chenu mkiwa wapinzani kama mtakuwa mnaisifia serikali kwa kila kitu.... sitegemei make hata sasa hivi mmeacha kazi yenu ya msingi mmebakia kuwakosoa wapinzani utadhani wao ndo wapo madarakani!
 
Wakuu habari,
Kama tujuavyo, Mh. Mbowe kaitisha maandamano nchi nzima na akavitaka vyama pinzani vifanye hivyo. Arusha na Arumeru nimeona wao tayari maandamano yasiyo na kikomo yataanza kesho tar 20.
Naomba tufahamishane huko kwenu (mikoa mingine) maandamano na migomo inaanza lini? Hii itasaidia kucreate awareness kwa wananchi wa maeneo husika ili wale waoga kama kunguru ambao ndio wanaoishi miaka mingi waanze kujiweka pembeni...!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
sisi huku wote sisimu
na je kuna mgomo wa wanachama wa ccm? na kama upo itakuwa lini.nawasilisha
 
Bunge la katiba mwisho tarehe 4, na maandamano ni kushinikiza lisitishwe, maandanano baada ya tarehe hiyo yatatakuwa ya agenda ipi?
 
sisi huku wote sisimu
na je kuna mgomo wa wanachama wa ccm? na kama upo itakuwa lini.nawasilisha
Mnisaidie kum- cc Msalani na Lizabon au cc Mingoi na Mwekundu waje wamjibu huyu ndg.


Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
CCM kesho nao wataandamana kupinga maandamano ya Chadema!!!!!

Sasa hapa yale ya Misri si ndo yanaanzaga hapa? Wana CDM walivo na hasira wakikutana uso kwa uso na CCM c patachimbika?


Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Ndugu mtu asiwahadae maandamano ni kupotezeana muda na polisi wako sahihi kulinda usalama wenu kuwaokolea na muda mnaohamasihwa mkaupoteze mshindwe kufanya shughuli zenu zinazowafanya muishi kwa amani na upendo. maandamano ni shida sana Syria waliandamana kiko wapiii lybia nk nk mumeona eee ndo hivyo mueleze na jirani yako aelewe
 
waacheni wamalizie kula hela zao,tarehe ya bmk ni kesho kutwa tu
 
Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikifikiria kuwa kushuka kwa kiwango kikubwa kwa CHADEMA kunatokana na migogoro ya ndani ya chama. ila nimegundua kwamba si hivyo, bali chama hicho kilikaa muda mrefu bila kufanya maandamano ambayo ndiyo nguzo kuu za chama hicho. Sasa naona muda umefika na chama sasa kinaimarika kwa kasi ya ajabu.
 
Idadi kubwa ya wananchi haiungi mkono kabisa maandamano ya chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) ,sasa kwanini waendelee na mchakato wao wa kuandamana?
 
Join Date : 5th September 2014
Posts : 4
Rep Power : 0
Likes Received 0
Likes Given 0

haha watu wengine wanapima Oil humu JF
 
Idadi kubwa ya wananchi haiungi mkono kabisa maandamano ya chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) ,sasa kwanini waendelee na mchakato wao wa kuandamana?

Hebu washauri polisi waache kutumia nguvu kuyazuia hayo maandamano ndo uone km wananchi wanaunga mkono ama lah!
 
Back
Top Bottom