Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Chuo Kikuu cha SMMUCo waingia katika mgomo
na Rodrick Mushi, Moshi
WIMBI la wanafunzi wa vyuo vikuu kuendelea kugoma limeendelea kushika kasi ambapo jana wanafunzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Tumaini cha kumbukumbu ya Askofu Stefano tawi la Moshi mjini (SMMUCo) wamegoma kuingia darasani kwa muda wa siku mbili wakilalamikia kutopatiwa fedha za kujikimu toka Bodi ya Mikopo.
Wakizungumza mbele ya Mkuu wa Chuo hicho, Arnold Temu, walisema wataendelea na mgomo wao hadi watakapohakikisha changamoto zilizopo chuoni hapo zinatatuliwa, ikiwemo tatizo la mawasiliano ya intaneti, ubovu wa miundombinu pamoja uhaba wa vitabu.
Hata hivyo kutokana na mgomo huo unaoendelea, Jeshi la Polisi mkoani hapa lililazimika kuweka kambi ya muda kuzunguka chuo hicho ili kuzuia vurugu ambazo zingeweza kutokea.
Walidai kuwa kuchelewa kukabidhiwa fedha zao kuna uwezekano wa uongozi wa chuo hicho kudiriki kutumia kiasi cha sh milioni 7 ambazo zinadaiwa kutoka bodi ya mikopo.
Wanafunzi hao ambao walionekana wakiimba nyimbo za muasisi wa Taifi Hayati Mwalimu Julius Nyerere walisema kuwa mazingira ya chuo hicho yamekuwa mabovu kiasi cha kuhatarisha maisha ya wanafunzi hao.
Tumekuwa tukiwasilisha matatizo haya mara kwa mara katika uongozi lakini wamekuwa hawatusikilizi na hivyo tutaendelea kugoma na hatuna imani na serikali ya wanafunzi..tutapiga kura ya kutokuwa na imani nao, walisema.
Kutokana na mgomo huo wanafunzi wa mwaka wa kwanza na wa tatu walishindwa kufanya mitihani ambayo ilikuwa ikiendelea chuoni hapo
na Rodrick Mushi, Moshi
Wakizungumza mbele ya Mkuu wa Chuo hicho, Arnold Temu, walisema wataendelea na mgomo wao hadi watakapohakikisha changamoto zilizopo chuoni hapo zinatatuliwa, ikiwemo tatizo la mawasiliano ya intaneti, ubovu wa miundombinu pamoja uhaba wa vitabu.
Hata hivyo kutokana na mgomo huo unaoendelea, Jeshi la Polisi mkoani hapa lililazimika kuweka kambi ya muda kuzunguka chuo hicho ili kuzuia vurugu ambazo zingeweza kutokea.
Walidai kuwa kuchelewa kukabidhiwa fedha zao kuna uwezekano wa uongozi wa chuo hicho kudiriki kutumia kiasi cha sh milioni 7 ambazo zinadaiwa kutoka bodi ya mikopo.
Wanafunzi hao ambao walionekana wakiimba nyimbo za muasisi wa Taifi Hayati Mwalimu Julius Nyerere walisema kuwa mazingira ya chuo hicho yamekuwa mabovu kiasi cha kuhatarisha maisha ya wanafunzi hao.
Tumekuwa tukiwasilisha matatizo haya mara kwa mara katika uongozi lakini wamekuwa hawatusikilizi na hivyo tutaendelea kugoma na hatuna imani na serikali ya wanafunzi..tutapiga kura ya kutokuwa na imani nao, walisema.
Kutokana na mgomo huo wanafunzi wa mwaka wa kwanza na wa tatu walishindwa kufanya mitihani ambayo ilikuwa ikiendelea chuoni hapo