Bara la Afrika lina janga kubwa linalolitesa kwa miaka mingi mno nalo ni la ugonjwa wa ukimwi. sina haja kabisa ya kusema ni chanzo kipi kinachochangia kuenea kwa gonjwa hili baya kwani kila muafrika sio tu anajua bali kwa njia moja au nyengine ameguswa na gonjwa hili. Kinachonitatiza mimi ni kuwepo na hii big brother africa ( ambayo jumba lenyewe liko south africa ambako gonjwa la ukimwi limekithiri) na kila kukicha kinachoonyeshwa kwenye site mbali mbali ni wanawake waliomo katika hilo jumba wakiwa uchi wa mnyama na pia watu waki sex. Yaani imefika mwaka huu kuna fee maalum ili uweze kuona parts ambazo hazikurushwa hewani, parts hizo zaidi ni wakati wakikoga na wakiingiliana. Suali langu ni kuwa hivi kweli watayarishaji wa kipindi hiki wanajua ni kiasi gani wanachangia kuhamasisha casual sex? Hivi program hii ina manufaa na elimu yeyote kwa jamii yetu? Kweli waafrika tunaiga mengi kutoka nje ya bara letu lakini hili kweli ni lazima?