Sumbaye
Member
- Apr 26, 2025
- 59
- 77
Mjadala kuhusu maendeleo ni mtambuka sana. Watu wamegawanyika juu ya dhana hii, wapo wanaodhani maendeleo ni upatikanaji wa huduma za kijamii kama vile hospitali, barabara, umeme, elimu nk inatosha kuwa kipimo cha maendeleo (maendeleo ya vitu). Wapo pia wanaodhani maendeleo uwezo wa watu kushiriki wenye shughuli za kiuchumi na uzalishaji na kujiongezea/kukuza kipato (maendeleo ya watu). Halikadhalika wapo wanaoamini uwepo wa vitu hivi vyote.
Je, ni kipi muhimu Kati ya maendeleo ya vitu na maendeleo ya watu? Je tunachopata Tanzania ni maendeleo ya vitu au ya watu? Au tunapata vyote?
Maendeleo ya vitu pale serikali inapotumia kodi na rasilimali zingine kujenga barabara, hospitali, reli, shule nk bila kugusa shughuli muhimu za kiuchumi za wananchi. Maendeleo ya watu ni pale serikali inapotumia kodi kuwekeza au kujenga mazingira rafiki ya kiuchumi kwa kugusa shughuli kuu za uzalishaji wananchi kama vile kilimo, ufugaji, biashara na viwanda.
Kuwekeza kwenye utoaji wa huduma za kijamii kama barabara, reli, nk bila kugusa shughuli zao za kiuchumi Kisera na uwekezaji haiwezi kuboresha Hali ya maisha ya wananchi. Uwekezaji unaogusa shughuli kuu za wananchi ndio njia pekee inayoleta maendeleo jumuishi kwa wananchi.
Ndio njia ambazo serikali zinaweza kukusanya kodi nyingi kwa sababu ya wananchi wengi kushiriki kwa asilimia kubwa kwenye uzalishaji. Hivyo serikali inaweza kutumia kodi hizo kutoa huduma za kijamii kama vile shule, barabara, umeme, nk
Je, ni kipi watanzania tunapata kwa asilimia kubwa Kati ya maendeleo ya vitu na maendeleo ya watu?
Tumeona serikali ikijinasibu kwa kujenga barabara, mashule, mahospitali, nk kwa kelele kubwa sana. Tukipita mitaani tunakutana na mabango yanayosema "Mama hana deni", mengine yakisomeka " Mama ametenda". Hivyo hivyo ukipita mitandaoni utakutana na kauli zenye viambatanisho vya picha za mashule, zahanati nk zikiwa na Jumbe " Mama yuko kazini" .
Je ni kweli Mama yuko kazini?
Ukiachana na hizo huduma ambazo zipo kwa uchache wake, ni kipi kingine Ametenda?
Shughuli kuu za watanzania ambazo zina mchango mkubwa kwenye uchumi ni kilimo, biashara na ufugaji.
Hebu tuangazie maisha ya wakulima. Je serikali imeyagusa maisha ya wakulima ? Serikali imewagusa vipi wakulima kwenye masoko? Bei za pembejeo za kilimo? Uchakataji na uongezeko la mnyororo wa thamani kwa mazao ya kilimo? Upatikanaji wa maji na miundo mbinu ya umwagiliaji?
Serikali imewawezeshaje wakulima wa Dodoma, Singida, Shinyanga, Tabora, Simiyu nk ambayo ni maeneo kame kuondokana na kilimo cha kutegemea mvua? Je serikali imekubali kwamba maeneo haya ni kame? Ni kweli kwamba maana ya neno ukame lilitokana na kiasi cha mvua lakini haimaanishi maeneo haya hakuna maji.
Mungu ameweka mabilioni ya Lita za ujazo kwenye ardhi yetu. Suala tu ni uwezo na uthubutu wa serikali kuweza kutumia maji yaliyopo ardhini kubadilisha maisha ya wananchi. Katika nchi ya Marekani, kuanzia mwaka 1940 kurudi nyuma majimbo Kama Florida, Nevada, New Mexico, Texas, nk ambayo yapo upande wa magharibi yalikuwa na ukame sana.
Mwaka 1910 walianza mkakati wa kuyabadili majimbo haya kame kuwa na tija kwenye kilimo, hivyo wakaanza mkakati za kuchimba mabwawa na visima kwa ajili ya wawezesha wananchi kupata maji kwa ajili ya kilimo. Kwa kuwa ili maji yawafikie wakulima lazima yasukumwe (Power/umeme),mwaka 1933 serikali ya Marekani ilianzisha program ya kuweka umeme katika vijiji vyote vilivyokuwa kwenye plan ya uzalishaji wa kilimo ambayo ilikamilika mwaka 1935.
Hadi kufikia 1940 hekta milion 21 zilipata maji ya umwagiliaji ambayo iliongeza uzalishaji kwa asilimia 35. Kufikia mwaka 1978, hekta milioni 43 zilifikiwa na maji kwa ajili ya umwagiliaji na kuongeza tija kwa asilimia 74 ya mauzo ya mazao yote ya kilimo. Asilimia zaidi ya 70 ya arable land ya China ipo chini ya kilimo cha umwagiliaji. Tunahitaji nini?
Tukihitaji kubadilisha maisha ya wananchi wetu hatuhitaji kugundua kitu kipya. Template ipo tayari, ni sisi kufuata njia ambazo mataifa yaliyopiga hatua yamepitia. As
Swali ni je, serikali yetu imekubali wananchi wake walime kilimo cha kutegemea mvua? Kati ya miezi 12 ya mwaka, kwa maeneo mengi ya Tanzania, miezi ya uzalishaji ni Minne tu. Miezi 7 shughuli za kilimo zinasimama? Je tunaweza kupata maendeleo kwa namna hii? Jibu tubaki nalo. Mama ametenda wapi? Mbona bado ana madeni au wanaodai hawamju mdeni wao?
Tukiangazia sekta ya mifugo, kwa mujibu wa sensa ya 2023, Tanzania ni nchi ya Pili kwa idadi kubwa ya mufugo takribali milioni 88. Idadi hii ya mifugo imesaidiaje taifa kukua kiuchumi? Serikali imeyagusaje maisha ya wafugaji kwa kuwatengea maeneo ya malisho? Kwa idadi hii ya mifugo, ukisoma mpango wa maendeo wa miaka 5 wa Wizara ya mifugo unaomalizika 2025/26 umetoa makadirio mahitaji ya eneo la malisho ya mifugo kuwa ni hekta milioni 103.
Mpaka Sasa hekta zilizotengwa kwa ajili ya malisho ya mifugo ni hekta milioni 3.6 tu. Mama hana deni? Ukiachana na malisho, vipi kuhusu masoko ya mazao ya mifugo? Uchakataji/usindikaji wa mazao ya mifugo? Uongezaji wa thamani? Hatumjui mdeni wetu.
Halikadhalika kuhusu wafanya biashara, tumeshuhudia migogoro mingi sana Kati ya serikali na wafanya biashara juu ya mrudindikano wa kodi. Tumeyaona ya kariakoo, Arusha, nk . Je maisha ya wafanyabiashara yameguswa kwa kiasi gani kwa mifumo rafiki ya kodi?
Namalizia kwa kusema, nikiona bango linasema "Mama hana deni", Nalazimila kufikiri kwamba watanzania hatumjui mdeni wetu.
Je, ni kipi muhimu Kati ya maendeleo ya vitu na maendeleo ya watu? Je tunachopata Tanzania ni maendeleo ya vitu au ya watu? Au tunapata vyote?
Maendeleo ya vitu pale serikali inapotumia kodi na rasilimali zingine kujenga barabara, hospitali, reli, shule nk bila kugusa shughuli muhimu za kiuchumi za wananchi. Maendeleo ya watu ni pale serikali inapotumia kodi kuwekeza au kujenga mazingira rafiki ya kiuchumi kwa kugusa shughuli kuu za uzalishaji wananchi kama vile kilimo, ufugaji, biashara na viwanda.
Kuwekeza kwenye utoaji wa huduma za kijamii kama barabara, reli, nk bila kugusa shughuli zao za kiuchumi Kisera na uwekezaji haiwezi kuboresha Hali ya maisha ya wananchi. Uwekezaji unaogusa shughuli kuu za wananchi ndio njia pekee inayoleta maendeleo jumuishi kwa wananchi.
Ndio njia ambazo serikali zinaweza kukusanya kodi nyingi kwa sababu ya wananchi wengi kushiriki kwa asilimia kubwa kwenye uzalishaji. Hivyo serikali inaweza kutumia kodi hizo kutoa huduma za kijamii kama vile shule, barabara, umeme, nk
Je, ni kipi watanzania tunapata kwa asilimia kubwa Kati ya maendeleo ya vitu na maendeleo ya watu?
Tumeona serikali ikijinasibu kwa kujenga barabara, mashule, mahospitali, nk kwa kelele kubwa sana. Tukipita mitaani tunakutana na mabango yanayosema "Mama hana deni", mengine yakisomeka " Mama ametenda". Hivyo hivyo ukipita mitandaoni utakutana na kauli zenye viambatanisho vya picha za mashule, zahanati nk zikiwa na Jumbe " Mama yuko kazini" .
Je ni kweli Mama yuko kazini?
Ukiachana na hizo huduma ambazo zipo kwa uchache wake, ni kipi kingine Ametenda?
Shughuli kuu za watanzania ambazo zina mchango mkubwa kwenye uchumi ni kilimo, biashara na ufugaji.
Hebu tuangazie maisha ya wakulima. Je serikali imeyagusa maisha ya wakulima ? Serikali imewagusa vipi wakulima kwenye masoko? Bei za pembejeo za kilimo? Uchakataji na uongezeko la mnyororo wa thamani kwa mazao ya kilimo? Upatikanaji wa maji na miundo mbinu ya umwagiliaji?
Serikali imewawezeshaje wakulima wa Dodoma, Singida, Shinyanga, Tabora, Simiyu nk ambayo ni maeneo kame kuondokana na kilimo cha kutegemea mvua? Je serikali imekubali kwamba maeneo haya ni kame? Ni kweli kwamba maana ya neno ukame lilitokana na kiasi cha mvua lakini haimaanishi maeneo haya hakuna maji.
Mungu ameweka mabilioni ya Lita za ujazo kwenye ardhi yetu. Suala tu ni uwezo na uthubutu wa serikali kuweza kutumia maji yaliyopo ardhini kubadilisha maisha ya wananchi. Katika nchi ya Marekani, kuanzia mwaka 1940 kurudi nyuma majimbo Kama Florida, Nevada, New Mexico, Texas, nk ambayo yapo upande wa magharibi yalikuwa na ukame sana.
Mwaka 1910 walianza mkakati wa kuyabadili majimbo haya kame kuwa na tija kwenye kilimo, hivyo wakaanza mkakati za kuchimba mabwawa na visima kwa ajili ya wawezesha wananchi kupata maji kwa ajili ya kilimo. Kwa kuwa ili maji yawafikie wakulima lazima yasukumwe (Power/umeme),mwaka 1933 serikali ya Marekani ilianzisha program ya kuweka umeme katika vijiji vyote vilivyokuwa kwenye plan ya uzalishaji wa kilimo ambayo ilikamilika mwaka 1935.
Hadi kufikia 1940 hekta milion 21 zilipata maji ya umwagiliaji ambayo iliongeza uzalishaji kwa asilimia 35. Kufikia mwaka 1978, hekta milioni 43 zilifikiwa na maji kwa ajili ya umwagiliaji na kuongeza tija kwa asilimia 74 ya mauzo ya mazao yote ya kilimo. Asilimia zaidi ya 70 ya arable land ya China ipo chini ya kilimo cha umwagiliaji. Tunahitaji nini?
Tukihitaji kubadilisha maisha ya wananchi wetu hatuhitaji kugundua kitu kipya. Template ipo tayari, ni sisi kufuata njia ambazo mataifa yaliyopiga hatua yamepitia. As
Swali ni je, serikali yetu imekubali wananchi wake walime kilimo cha kutegemea mvua? Kati ya miezi 12 ya mwaka, kwa maeneo mengi ya Tanzania, miezi ya uzalishaji ni Minne tu. Miezi 7 shughuli za kilimo zinasimama? Je tunaweza kupata maendeleo kwa namna hii? Jibu tubaki nalo. Mama ametenda wapi? Mbona bado ana madeni au wanaodai hawamju mdeni wao?
Tukiangazia sekta ya mifugo, kwa mujibu wa sensa ya 2023, Tanzania ni nchi ya Pili kwa idadi kubwa ya mufugo takribali milioni 88. Idadi hii ya mifugo imesaidiaje taifa kukua kiuchumi? Serikali imeyagusaje maisha ya wafugaji kwa kuwatengea maeneo ya malisho? Kwa idadi hii ya mifugo, ukisoma mpango wa maendeo wa miaka 5 wa Wizara ya mifugo unaomalizika 2025/26 umetoa makadirio mahitaji ya eneo la malisho ya mifugo kuwa ni hekta milioni 103.
Mpaka Sasa hekta zilizotengwa kwa ajili ya malisho ya mifugo ni hekta milioni 3.6 tu. Mama hana deni? Ukiachana na malisho, vipi kuhusu masoko ya mazao ya mifugo? Uchakataji/usindikaji wa mazao ya mifugo? Uongezaji wa thamani? Hatumjui mdeni wetu.
Halikadhalika kuhusu wafanya biashara, tumeshuhudia migogoro mingi sana Kati ya serikali na wafanya biashara juu ya mrudindikano wa kodi. Tumeyaona ya kariakoo, Arusha, nk . Je maisha ya wafanyabiashara yameguswa kwa kiasi gani kwa mifumo rafiki ya kodi?
Namalizia kwa kusema, nikiona bango linasema "Mama hana deni", Nalazimila kufikiri kwamba watanzania hatumjui mdeni wetu.