Ni madini gani ambayo yanauzika kwa haraka Dar. Naomba anayejua aniambie.

S.Liondo

JF-Expert Member
Apr 20, 2011
3,408
1,712
Wakuu, ningependa kupata kujua ni madini gani yanayouzika kwa haraka Dar kwa bei yenye tija. Ninauliza kwasababu jamaa yangu ana aina tofauti tofauti na ameniamini kwamba naweza kumsaidia kuuza kama nitaweza ambapo nami nitapata cha juu. Anayo aina nyingi tu ikiwemo Topaz, Ruby, Rhodolite, Sapphire, n.k. Anayejua naomba anisaidia maelekezo.
 
Ruby is number one ktk list yako. Lkn pia almas, dhahabu,tanzanite ni fast deals
Asante mkuu kwa jibu lako. Naona Almasi, dhahabu na Tanzanite jamaa hana, ila Ruby. Je Unawafahamu wanunuzi wowote.
 
Mnakujaga na thread kama hizi... Alafu muda tu mnaliza watu..
Mkuu mimi sio hao walizao watu, ninachokisema ninakimaanisha. Wewe kama unawajua wanunuzi niunganishe nao. Nitaonana nao kwanza tufahamiane vizuri kabla ya biashara ya aina yeyote. Kumbuka kulizwa si kwa anayeuziwa tu, hata anayeuza anaweza kulizwa.
 
Madini yanayouzika kwa haraka bongo ni
1. Maisilamu
2. Makristo
3. Malokole
4. Masabato
Hayo mengine kama Ruby, Rhodolite, Topaz hayana soko huku.
Wewe ni lazima utakuwa unaishi kwenye dunia yako tofauti na tunayoishi ambako madini hayo uliyoyataja yanapatikana. Ningependa uelewe kuwa ninauliza kwa kumaanisha na si mzaha kama wale wengine ambao pengine wamekuwa wakiwachezea humu JF.
 
mkuu labda kama ninataka kuingia kwenye mikono ya Bashite. Lakini ninatamani sana nipate mahali pa kuyauzia hayo madini niliyoulizia.
 

Attachments

  • IMG-20170301-WA0013.jpg
    IMG-20170301-WA0013.jpg
    108.3 KB · Views: 50
Back
Top Bottom