Ni lini Waziri wa Ardhi Jerry Silaa Utasikiliza Malalamiko ya Waliodhulumiwa Ardhi na CCM?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
119,069
221,755
Nimekuona ukifanya kazi nzuri kila ulikopita, japo wahusika kwenye ofisi yako hujawagusa, lakini kwa hatua angalau ya kuwarejeshea mali zao waliodhulumiwa si haba

Bali, wako wale waliodhulumiwa maeneo yao na Chama chako cha CCM, hawa wako wengi mno, na wengi walikisaidia tu Chama chako kujenga ile misingi ya Mashina ya Wakereketwa, kwenye maeneo yao, kukubali kwa watu hawa kujengwa kwa mashina ya Wakereketwa imegeuka kuwa laana, ccm ikapora viwanja hivyo vya watu na kujenga ofisi zao na maeneo mengine wakaweka na majengo ya Biashara za kupangisha.

Kwa vile serikali ni ya ccm hakuna mahali popote ambapo Wahanga hawa walienda kulalamika na kusikilizwa, ofisi zote zimewapuuza, Walioenda Mahakamani nao wanapigwa danadana kila siku ili wakate tamaa, Hawana pa kukimbilia wamebaki wakilalamika huku wengine wakifa kwa kisukari kupanda na shinikizo la damu.

Sasa kwa vile wewe ni Waziri na kwa vile umeonyesha uwezo angalau kwa kuwadaka Matapeli wa Ardhi, Akiwemo Alex Msama ambaye ni Tapeli papa namba 3, basi tunaamini hata hili dogo la ccm utaliweza.

Naomba Kuwasilisha
 
Mbona una haraka sana kamanda,
kuwa na subra, kua mstahimilivu. mambo mazuri hayahitaji haraka wala pupa....

Wajibu na jukumu la waziri mwenye dhamana, kuskiza na kutatua kero na changamoto za ardhi kwa waTanzania wote bila kujali dini, rangi, mrengo wa kisiasa au chama cha siasa n.k

Ni suala la muda tu atakufukia ulipo, usiwe na wasiwasi kabisa, haki na stahiki yako ya ardhi haitapotea mbele ya waziri makini sana Jery Slaa :NoGodNo:
 
Huo mgogoro nadhani atautatua mwishoni kabisa ukikaribia uchaguzi.

Itoshe kusema, kama Hadi umeandika thread kumhusu,

Ni dhahiri kuwa, Kuna kitu anafanya.

Jerry Slaa Abarikiwe!!
 
Kule mwanza machinga waliambiwa wanapewa maeneo ya biashara kumbe ni viwanja vya ccm, geita uwanja uliojengwa na wiliamson nao umekuwa wa ccm, katoro waliambiwa wanajengewa soko wakachangishwa mwisho wa siku ccm wanakuja kukusanya kodi, kama huwezi kupata kiwanja kura utapataje? Chalinze nusura wakatane makoleo wakigombea mashimo ya kuchimba mchanga
 
Kule mwanza machinga waliambiwa wanapewa maeneo ya biashara kumbe ni viwanja vya ccm, geita uwanja uliojengwa na wiliamson nao umekuwa wa ccm, katoro waliambiwa wanajengewa soko wakachangishwa mwisho wa siku ccm wanakuja kukusanya kodi, kama huwezi kupata kiwanja kura utapataje?
Swadakta
 
Ila kiherehere kinaponza sana! Na njaa yote hii mnawezaje kuwapa maeneo yenu hao watu wajenge ujinga wa mashina ya wakereketwa?
 
Back
Top Bottom