Habari inayolindima sasa hivi ni hili suala la wapiganaji wa Iraq wajulikanao kama ISIL. Ukiangalia historia ya ISIL utaona kwamba kama wamarekani wasingevamia Iraq 2003, ISIL isingekuwa kama ilivyo sasa hivi. Hebu tuangalie wamerakani wamesababisha vikundi vingapi vya ugaidi duniani.
1) Hamas- Miaka ile kulikuwa na machafuko kati ya Hamas na Fatah, wakati huo Hamas kilikuwa chama kidogo tu lakini Marekani ilisupport Hamas kwa kuipa silaha, mwisho wake sasa Hamas ni chama kikubwa cha kigaidi kwa mujibu wa wamarekani.
2) Inajulikana Alqaeda ilipata misaada lukuku kutoka marekani wakati wanapikana na warusi.
3) Wamarekani waliua viongozi wengi sana wa kikabila huko Somalia, hii ilisababisha vacuum ambayo iliupa mwanya alshabab kuchukua nchi.
Marekani ikiingilia mapigano nchi za nje inafanya mambo yawe mabaya Zaidi. Mimi sioni sababu ya mmarekani kuingilia mapigano ya ISIL na kurds. Kwanini? Kwa sababu nina uhakika kama wairaq wakichoka utawala wa ISIL watawafukuza tu? Hata Iran ina uwezo wa kuwasambaratisha ISIL bila kutaja Saudi Arabia ambayo ina mamia ya ndege na vifaru kutoka marekani. Kwanini Marekani iliyopo mbali hivyo na Iraq iwe na mapenzi na watu wa Iraq kuliko wairaq au hata nchi za jirani?
Kuwapa siraha Kurds ni mchezo wa hatari sana kwa sababu hawa jamaa wataanza kuwaua wasunni, wasunni watataka kulipiza kisasi halafu mwishowe tutaona mauaji ya wenyewe kwa wenyewe yakiendelea tena.
Sababu ya Marekani kuingilia vita isiyoihusu ni nia yake ya kucontrol middle east, haitaki kuona nchi yoyote sehemu hii ya dunia kuwa na nguvu.
Mimi sio mwislamu, lakini kuna ubaya gani kama waislamu wakiamua kufuata sharia katika nchi zao ambazo ni 99 percent Muslim? Kwa mfano Misri?
​
Wandugu, tabia za wamarekani na wamagharibi zinazua chuki za kidini ambazo hapo mbeleni zitasababisha vita vya kidini baina ya jamii ambazo hazijawahi kuwa na mikwaruzano.
1) Hamas- Miaka ile kulikuwa na machafuko kati ya Hamas na Fatah, wakati huo Hamas kilikuwa chama kidogo tu lakini Marekani ilisupport Hamas kwa kuipa silaha, mwisho wake sasa Hamas ni chama kikubwa cha kigaidi kwa mujibu wa wamarekani.
2) Inajulikana Alqaeda ilipata misaada lukuku kutoka marekani wakati wanapikana na warusi.
3) Wamarekani waliua viongozi wengi sana wa kikabila huko Somalia, hii ilisababisha vacuum ambayo iliupa mwanya alshabab kuchukua nchi.
Marekani ikiingilia mapigano nchi za nje inafanya mambo yawe mabaya Zaidi. Mimi sioni sababu ya mmarekani kuingilia mapigano ya ISIL na kurds. Kwanini? Kwa sababu nina uhakika kama wairaq wakichoka utawala wa ISIL watawafukuza tu? Hata Iran ina uwezo wa kuwasambaratisha ISIL bila kutaja Saudi Arabia ambayo ina mamia ya ndege na vifaru kutoka marekani. Kwanini Marekani iliyopo mbali hivyo na Iraq iwe na mapenzi na watu wa Iraq kuliko wairaq au hata nchi za jirani?
Kuwapa siraha Kurds ni mchezo wa hatari sana kwa sababu hawa jamaa wataanza kuwaua wasunni, wasunni watataka kulipiza kisasi halafu mwishowe tutaona mauaji ya wenyewe kwa wenyewe yakiendelea tena.
Sababu ya Marekani kuingilia vita isiyoihusu ni nia yake ya kucontrol middle east, haitaki kuona nchi yoyote sehemu hii ya dunia kuwa na nguvu.
Mimi sio mwislamu, lakini kuna ubaya gani kama waislamu wakiamua kufuata sharia katika nchi zao ambazo ni 99 percent Muslim? Kwa mfano Misri?
​
Wandugu, tabia za wamarekani na wamagharibi zinazua chuki za kidini ambazo hapo mbeleni zitasababisha vita vya kidini baina ya jamii ambazo hazijawahi kuwa na mikwaruzano.