Ni kweli kuhusu Rais Magufuli?

Ni kweli kuhusu Rais Magufuli?

Ulitaka kusema nini?
Kuviita vyombo vya habari ni vya kihuni na vinamilikiwa na wahuni ni uhuni usiomithilika wala kuvumiliwa. Kama una majina yake tuwekee hapa tuvijadili na kuubaini uhuni wake na kinyume chake unatumika visivyo.
Nikushauri uanzishe vyako ambavyo vitakuwa na kazi ya kusifu tu.
Umeharibia sikukuu.
 
Kwanza ni mpongeze kwa kazi nzuri inayoifanya ya kujenga taifa imara.

Swali, kuna nguvu Kubwa nyuma ya pazia kupitia vyombo vya habari, baadhi vinavyomilikiwa na wahuni wachache, ambao wanalengo la kukwamisha juhudi za mheshimiwa Magufuli, kwa kuamua kupotosha ukweli halisi wa hatua anazochukua dhidi ya uhalifu nchini dhidi ya raslimali zetu.

Je? Rais Magufuli atakwama kwa kua magazeti hayaandiki mazuri atendayo kwa taifa hili.
Je kwa Tanzania ya sasa source ya habari ni magazeti pekee?
Kama huna cha kupost kaa kimya, nenda pale ofisini wambie kwakweli leo nimekosa kabisa cha kupost nadhan watakufikiria hata robo ya ujira wa siku, kuliko kupost kitu ambacho hata hakieleweki hata wachangiaji hawajui wachangie nini.
 
Acha ujinga jomba, kama kuna sehemu wajinga wamejaa basi ni ndani ya jukwaa hili.
Toka matusi yalipoluhusiwa badala ya kushindana kwa hoja ndipo umaarufu ulianza kupotea.
Sasa kuna greater thinker wachache na wahuni wengi mithiri yako ambao huibuka kwa mistari miwili mpaka mitatu iliyojaa matusi.
Mnatumika nn?
 
Akiyaleta mambo ya maendeleo hata kidogo kama piritoni watu watayaona. Hana haja ya kungojea misifa. Fly over yake inahitaji kutangazwa?? Acha kuigiza, nenda theater kapange stage show yako huko.
Magazeti kutokuandika hayazuii maendeleo.
 
None of them, naona amekuja kutukana tu vyombo binafsi vya habari..

yy chombo kizuri cha habari ni kile kinachosifia serikali,

alafu jamaa anainekana kichwani kwake hamna kitu.. toka lini chombo cha habari kikaweza kukwamisha maendeleo yanayofanywa na Serikali

Mbaazi zikikosa maua husingizia JUA .
 
Kwanza ni mpongeze kwa kazi nzuri inayoifanya ya kujenga taifa imara.

Swali, kuna nguvu Kubwa nyuma ya pazia kupitia vyombo vya habari, baadhi vinavyomilikiwa na wahuni wachache, ambao wanalengo la kukwamisha juhudi za mheshimiwa Magufuli, kwa kuamua kupotosha ukweli halisi wa hatua anazochukua dhidi ya uhalifu nchini dhidi ya raslimali zetu.

Je? Rais Magufuli atakwama kwa kua magazeti hayaandiki mazuri atendayo kwa taifa hili.
Je kwa Tanzania ya sasa source ya habari ni magazeti pekee?
Kungekua hakuna chombo hata kimoja kinachoeleza tukio tungesema. Tbc1 hurusha tukio mubashara umma huangalia na kupata taarifa. Uhuru, Mzalendo, DailyNews na Habarileo kwa magazeti. Uhuru Fm,na Tbc Taifa na Tbc International zinarusha matukio yote.
Pia hivi vyombo uvisemavyo hurusha vitukio vidogo vilivyotokea kwenye tukio kubwa ambavyo huwafurahisha walaji wao na matajiri wao. Zaidi ya hayo magazeti hayo wateja wao ni wale waliozoea kulishwa maneo ya uongo kama vile ufisadi na udaku mwingine wao huita habari ya uchunguzi. Mfano gaseti la Jamhuri lilienda Mwanza mpaka Kolomije kuunadi umasikini wa wazazi wa Makonda na kushindwa kuja na habari za wanakolomije; wanavyopambana na mazingira yao ili kupata maisha bora. Sasa Magufuli kayakataa maudaku yao na yeye anataka kusema ukweli ambao si sera ya vyombo vyao. Kwa hali hii usitegemee waandike unavyofikiria.
 
Hii ndo inatakiwa humu jukwaani, hoja.
Si wale jamaa zetu, mpaka habari iwafurahishe Wao ndo habari.
Kama haikuwafurahisha ni matusi tu.
Wajifunze namna ya kutolea hoja ufafanuzi kama ulivyofanya.
Ndipo jukwaa tunalipa hadhi ya kuitwa greater thinker
 
Kama serikali ya JPM ni makini haiwezi kukwamishwa na na magazeti tena kwa maneno yako mwenyewe umesema magazeti haya ni ya wahuni.
 
Kwanza ni mpongeze kwa kazi nzuri inayoifanya ya kujenga taifa imara.

Swali, kuna nguvu Kubwa nyuma ya pazia kupitia vyombo vya habari, baadhi vinavyomilikiwa na wahuni wachache, ambao wanalengo la kukwamisha juhudi za mheshimiwa Magufuli, kwa kuamua kupotosha ukweli halisi wa hatua anazochukua dhidi ya uhalifu nchini dhidi ya raslimali zetu.

Je? Rais Magufuli atakwama kwa kua magazeti hayaandiki mazuri atendayo kwa taifa hili.
Je kwa Tanzania ya sasa source ya habari ni magazeti pekee?
Wakati mmoja kikwete alifanya mahojiano na swali aliloulizwa ilikuwa "Ungependa Watanzania wakukumbuke kwa lipi?" naye akajibu ya kuwa "wanikumbuke ya kuwa niliwatoa pale nikawaleta hapa".Naomba uitafakari kauli hiyo kwanza.Hakuweka ahadi ya mazuri wala mabaya na hii inaonyesha hekima kwani kwanza huwezi kumridhisha kila mtu.Jambo la pili na ambalo binafsi linanisumbua ni pale mtu aliyetoka chama kile kile ambacho kiko madarakani kwa zaidi ya miaka hamsini na mtu ambaye alikuwa katika serikali katika kipindi cha miaka 20 (ambayo ilivuruga mambo na kuifanya nchi kupinda) ndiye huyo huyo Masiah wetu kwa leo,kidogo napata kigugumizi.
Katika shida za Taifa yaliyofanyika mpaka leo ni kidogo mno ukilinganisha na rasilimali tulizokuwa nazo na wale tunaokumbuka vizuri tunapata shida kumlinganisha Raisi wetu wa sasa na Nyerere.Elimu bure ilikuwa elimu bure kweli,watu walihamishwa kwa nguvu na kuwa vijiji ingawa baadae ilifeli lakini ni kwa sababu ya unafiki wa waliokuwa jirani naye.Raisi wetu wa sasa amekuta nchi iliyotulia na watu waliokuwa na adabu na utii wa kutisha kwa viongozi,haikuja kama bahati kuna waliomtangulia ambao waliifanya kazi hiyo.
Binafsi namtakia kila la heri lakini aikumbuke kauli ya Kikwete "Niliwatoa pale nikawaleta hapa" inatosha.
 
44c45cbe92252cbf21df963627f8f2a9.jpg
 
Kwan nayo maendelea anayatekelezea kwenye vyombo vya habar??? Kwan TBC na Uhuru hazitoshi??
 
Back
Top Bottom