Ni kweli Dodoma ni katikati ya nchi?

Ni kweli Dodoma ni katikati ya nchi?

Kwenye ule mwamba kimechomekwa chuma kimetokelezea kwa juu hivi, pale opposite kuna vijumba vidogo vidogo kibao kila kijumba kimepandwa mwembe ile mifupi nasikia vilijengwa na wakoloni kipindi hicho
 
Katikat sio bahi bali ipo wilaya ya manyoni. Sehemu inaitwa Sukamahela ndio katkat mwa Tanzania

Upo sahihi mkuu, sukamahela mpaka kilimatinde ndo panapokadiliwa kuwa katkt ya nchi ndiyo maana kipind wanaanzisha redio tanzania kanda ya kati wakati huo walipendekeza iwe kilimatinde lkn wakaona ni vzr iwe dodoma mjini.
 
Alafu hiyo ramani siyo ya Tz,haiwezekani ziwa nyasa lote liwe Malawi na ziwa Tanganyika liwe Congo drc,tafuta ramani ya Tz nikupe jibu.Hii siyo kabisa.
 
wew huyo mchora ramani mbona kilaza selfish? kaikomba ziwa tanganyika na nyasa aisee
 
Katikati ya Nchi Ni sehemu moja inaitwa mhalala ambayo ipo ndani ya wilaya ya manyoni mkoa singida. Lakini sehemu yenyewe haiko mjini ni kijijini. Ni kilometer mia kutoka Dodoma mjini.

So walifanya approximation kwa mamia yaliyo karibu.

Uko sahihi, kijiji kinaitwa Sakamahela, kuna mnara juu ya mwamba. Mambo a Mjeruumani
 
Katikati ya nchi nia pale mbele kidogo ya Mlima Saranda
 
ni kweli katikati ya nchi haswa ipo bahi ipo dodoma wajerumani waliweka pini pale na faida ya wengine katikati ya dunia ni pale maka kwenye jiwe jeusi hili liliwekwa na nabii ibrahimu nchi za magharibi wethibitisha

hapana sio kweli katikati ya nchi ni mbele ya mlima saranda kabla ya kufika manyoni pale ilipo kuwa kambi ya wakoma na sio bahi dodoma
 
ni kweli katikati ya nchi haswa ipo bahi ipo dodoma wajerumani waliweka pini pale na faida ya wengine katikati ya dunia ni pale maka kwenye jiwe jeusi hili liliwekwa na nabii ibrahimu nchi za magharibi wethibitisha

Acha uongo.
Katikati mwa hii nchi ni Manyoni mkoani Singida, ila kwa sababu za kisiasa na kiusalama Nyerere aliamua kuhamishia Dodoma
 
Hahahaha,hili bonge la swali na jibu ndani yake.
Maana sijaelewa hata mleta uzi alitumia muda kiasi kufikiria hili au aliteka na yeye aboost
Watu wa Zanziberi bwana kwani wewe umefikilia nini au hilo neno katikati watu wa zanzibar na Mombasa mn maswali sana
 
eneo la tanzania halina umbo la mraba wala duara kusema kwamba utapata exactly katikati,hivyo basi makadirio ndio yametumika zaidi huku baadhi ya fact zikitumika kusogezea dodoma kama wajerumani walikubaliana ni hapo sukumahela!mfano mwanao akikuuliza katikati ya mwili wa binadamu ni wapi halafu kabla ya kumjibu ukaona kuwa katikati ni kwenye sehemu za siri si utaamua kumuonyesha kuwa katikati ni kwenye tumbo au kitovu?ndivyo busara ya kwamba ni dodoma ilivyotumika!
 
Katikati ya nchi hii ni manyoni eneo linaitwa sukamahela, ndio mjerumani kaweka alama pale hata ukipita unaiona ni kama kijinguzo kimewekwa juu ya kilima chenye mawe mengi.....ijumaa ntapita pale ntasimama niwapigieni picha
 
Kulingana na hiyo ramani Tanzania ndio ipo katikati ya Nchi sio Dom
 
Back
Top Bottom