Ni kweli CHADEMA watachukua nchi mwaka 2015

Ni kweli CHADEMA watachukua nchi mwaka 2015

Tuhamasishane mwaka huu tukapige kura ili kuindoa ccm madarakani
 
Hili sio swali, yaani usiulize majibu, kama unaswali ndio uulize!.

Pasco

Kati ya id ambazo huwa hazina mashaka humu ndani juu ya nin chaweza tokea au nin kifanyike mkuu upo juu
 
Nchi gani na viongozi mnaweza kabidhi nchı kwa magenge ya majambazı?Mbowe apewe nchi kabisaaa? Sahau, hawawezi shnda na wala hakutatakiwa gori la mkono!
 
Tukiangalia kwa jicho ndani ukawa wamejipaga sana na wanaonekana wako seriously kwenye kushika dola


QUOTE " Kwa kipindi chote cha kung’aa kwa Dk. Slaa katika majukwaa ya kisiasa, sambamba na kukua kwa siasa za upinzani nchini, Lowassa ametajwa kuwa miongoni mwa vinara wa tuhuma za ufisadi miongoni mwa wanaCCM.
Ujumbe uliokuwa ukitoka jukwaa la siasa za upinzani, hususan chama kikuu cha upinzani – Chadema, na hata viongozi wengine akiwamo Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba, ni kwamba CCM si wasafi – ni mafisadi na miongoni mwao ni Lowassa. Kwa mfano, tukio mojawapo lililoibua tuhuma hizo ni mkutano wa hadhara wa Mwembe Yanga jijini Dar es Salaam, Septemba 15, mwaka 2008.
Miaka saba baadaye tangu tukio hilo la Mwembe Yanga, mambo yanataka kugeuzwa. Vyovyote itakavyokuwa, ni kwamba sasa wanasiasa wa upinzani wanapaswa kuchagua moja kati ya mawili na kwa kweli, mojawapo wamekwishakuchagua na kubakiwa na jambo moja jingine tu. Jambo hilo ni kukana yale waliyowaeleza Watanzania kuhusu Lowassa.
Naam, sasa wanalojukumu la kukiri uwongo wao mbele ya umma kwamba Lowassa si fisadi, bali ni mtu safi na mwadilifu. Wasiishie kusema hayo tu, waruhusu maswali ya wananchi aliyetumia vizuri fedha za ujenzi wa ofisi ya ubunge katika Jimbo la Monduli.
Ni dhana dhaifu, kuamini kwamba jukumu la msingi ni kuiondoa CCM madarakani bila kutafakari timu inayoshiriki katika uondoaji huo imebeba taswira gani mbele ya jamii, taswira ambayo imetengenezwa na wanasiasa wenyeji ndani ya upinzani ambako Lowassa amejiunga. - See more at: Raia Mwema - Uko wapi uhalali wa Ukawa? " UNQUOTE
 
Lowasa anachukua nchi gani? Kenya au Uganda Rwanda? Naomba ufafanuzi please

Anachukua Tz utake usitake anakuwa rais wako humpend kale malimao hutaki badili uraia 25 Oct asubuh na mapema. Piiipoooooooz
 
Vyama ambavyo mtu mmoja anaweza akavichukua na kuvifinyangafinyanga kama ugali havifai kuongoza nchi.

Huna adabu gamba ww mwaka huu mnalo na limeng'ang'ania kwel kwel hamchomoi haki ya nan nawaambia mnawaza kuiba tuu
 
Thubutu kwa kipi ingewezekana ila kwa SSA hiwezekaniki tena ujue hiii figisu figisu watu na akili zao wamestuka walimpondaaa saaana Leo yy ndo anafaaa kwa hili wengi waliobaki ni vishabikii maandazi ila viti bungeni wanaweza kuongeza vingi so urais

Kafie mbali gamba ww mwaka huu mnalo na limeng'ang'ania kwel kwel hamchomoi haki ya nan nawaambia mnawaza kuiba tuu
 
Usiulize majibu ukawa wanachukua nchi acheni kushupaza shingo kuona mnaona lakini mnajifanya hamuoni
 
Back
Top Bottom