Dingswayo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 4,019
- 2,923
Kuna msemo unaosema, 'Ajali haina kinga'. Hata hivyo hapa Tanzania inaelekea kuwa msemo huo mara nyingine si sahihi. Ajali zingine zinaletwa na watu wenyewe, hasa ajali za barabarani. Hebu muangalieni huyu dereva anavyotaka kupita magari mengine wakati mbele yake kuna magari mengine yanakuja. Dereva kama huyu anatakiwa anyang'anywe leseni na kufunguliwa mashitaka kwa kuhatarisha maisha ya watu wengine.