Kwa hali ya kawaida kama ni kweli Bw.Lowasa ni mbaya hivyo na hana sifa za kuongoza TanZania basi kulikuwa hakuna haja yoyote ile ya kutumia nguvu kumponda, kumdhihaki na kumshusha chini namna hiyo kila siku, kwa hali ya kawaida angekataliwa tu na wananchi moja kwa moja, sasa ni kwanini nguvu kubwa sana inatumika kumpinga?
Kama ni kweli hayo mnayoyasema basi hata Wananchi wangeandamana kumpinga lakini kwangu mimi wanaompinga ni maelite tu na wala SIYO walala hoi sasa ni kwanini?
Ni kwanini kitu kibaya kionekane na maelite tu? Ni kwanini watu wanatoka mishipa kutaka kutuaminisha kwamba Lowasa hafai? Ni kwanini wasiache tuamue wenyewe? Na kama kuna anayefaa mbona hatumuoni? Mbona sijaona Mtu yoyote yule akienda kutangaza nia na kujaza watu masikini kama Lowasa?
Hii yote inaniambia ya kwamba kuna kitu hapa, kama ilivyo kawaida ya maelite wanataka kutuletea elite mwenzao asiyejua matatizo ya mwananchi wa kawaida, mimi nasema msitumie nguvu kumpinga Lowasa waachieni wananchi waamue!