Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Wakuu naomba msaada hii inshu mashimo sewage system ya vyoo yasiyojaa au wanasema hayana harufu sana. Haya mashimo ynayopigiwa pambio kila sehemu mitandaoni. Naomba experience ya aliyejenga.
Nasubr wajibu
 
Kwa upande wangu, najuta kutozingatia uhalisia wa mahitaji Vs. Ujenzi wenyewe. Naomba kutoa mifano:

1. Umuhimu wa swimming pool Vs. Uhalisia. Vilinganishi vya uhalisia:

a. Utitiri wa swimming pools, at your own choice,
b. Privacy, swimming pools za nyumbani ni changamoto hasa kama una familia,
c. High cost of maintenance etc.

2. Kujenga jengo kubwa Vs. Savings ambazo zingeenda kwenye uwekezaji mfano UTT,

3. Kujenga eneo ambalo barabara ni mbovu hasa kipindi cha mvua, eti kwa hoja; mji unakuwa.

4. Kutozingatia umbali toka kwenye kazi ya kudumu hadi nilipojenga. Hii ni issue.

5. Kuchelewa kupiga fensi kubwa ya ukuta.

6. Kujifananisha na mfadhili kwa mafundi au watu wanaofanya kazi site. Hii ni mission impossible: utaonekana bwege fulani tu mwishoni.

Mambo ni mengi ...
 
Kuweka nyumba ya wageni, kila shemeji zangu wanapokuja kutoka Usukumani-Mwanza lazma wakaniseme wanalaza kwenye "mabanda ya Uani"
 
Wakuu naomba msaada hii inshu mashimo sewage system ya vyoo yasiyojaa au wanasema hayana harufu sana. Haya mashimo ynayopigiwa pambio kila sehemu mitandaoni. Naomba experience ya aliyejenga.
harufu ipo bana kwani umeweka ubwabwa kwamba utanukia?

niliambiwa haitakiwi mtu atupie tishu, matambara au kitu chochote umo
kwa maana iyo haufai kuweka kwa nyumba unayoipangisha maana utaishia kugombana na wapangaji kila leo
 
Kuanza kujenga kwa pesa za pension baada ya kustaafu.
Mzee wangu baada ya kustaafu alifanya hicho kitu. Ni hatari kupita maelezo. Kwanini?

1. Mhusika hashauriki, anataka tu kujenga kwa sababu ana pesa mfukoni.

2. Anachokijenga huwa hakieleweki au hakikamiliki. Anaamini pesa yake ya pension inatosha kufanya chochote au kila kitu kitawezekana. Anaokota ramani popote anataka kujenga.
Mwisho wa siku kiinua mgongo kikaisha na jengo halijapauliwa au?
 
Kuamini mafundi nikiambiwa cement imeisha napiga simu tu inapelekwa bila kufatilia. Kuna siku fundi anapiga simu kuwa wamesimama kazi kwa kuwa cement imeisha inabidi ipelekwe haraka.

Ikabidi niende mwenyewe kuangalia kazi imefikiaje hadi cement kuisha hivo, nilivyofika mafundi wakastuka sana maana hawakutarajia kuniona kwa wakati huo. Ikawa kila ninapoingia kukagua jamaa kama ananizuga ili niache nimsikilize yeye. Nikahisi kitu nikaongeza umakini kuangalia chumba hadi chumba.

Bwana weee! Si nikakuta kuna mifuko 9 ya cement haijatumika wameificha kwenye chumba chooni. Asee jamaa alibabaika sana akakosa la kusema.
Ungemtimua shenzi kabisa huyo!!
 
Ujenzi unaanza na uchaguzi wa sehemu sahihi yani kiwanja utakapoweka iyo nyumba. usinunue tu kiwanja almradi ni kiwanja. kuna mambo muhimu madogomadogo ya kuzingatia kwa mfano namna eneo lenyewe lilivo-Je ni sehemu tambarare au miinuko. Hii ishu ni muhimu kwa sababu inaathari kwenye gharama ya ujenzi. Ujenzi wa kwenye miinuko una gharama zaidi kulinganisha na ule wa eneo tambarare na wkt mwingine mwinuko unaweza kukulazimisha ujenge basement au pengine kigorofa kabisa!

Ishu ingine ndogo lakini ya muhimu ni aina ya watu wanaokaa hapo (majirani). Hili wengi wanalifumbiaga macho lakini bdae linagharama zake. Wewe ni mtu wa kupenda utulivu lakini unajichomeka mitaa yenye watu wa kupenda vigoma/sherehe na matukio kila uchao, hapo lazima utakereka tu.

Kibaya zaidi majirani hawakwepeki, njia pekee ya kuwakwepa ni kuuza nyumba au kuipangisha hlf wewe utafute kwingine kwa kukaa, nje ya apo ukae kwa utulivu uku ukiwavumilia na kuwazoea!
 
Ujenzi unaanza na uchaguzi wa sehemu sahihi yani kiwanja utakapoweka iyo nyumba. usinunue tu kiwanja almradi ni kiwanja. kuna mambo muhimu madogomadogo ya kuzingatia kwa mfano namna eneo lenyewe lilivo-Je ni sehemu tambarare au miinuko. Hii ishu ni muhimu kwa sababu inaathari kwenye gharama ya ujenzi. Ujenzi wa kwenye miinuko una gharama zaidi kulinganisha na ule wa eneo tambarare na wkt mwingine mwinuko unaweza kukulazimisha ujenge basement au pengine kigorofa kabisa!

Ishu ingine ndogo lakini ya muhimu ni aina ya watu wanaokaa hapo (majirani). Hili wengi wanalifumbiaga macho lakini bdae linagharama zake. Wewe ni mtu wa kupenda utulivu lakini unajichomeka mitaa yenye watu wa kupenda vigoma/sherehe na matukio kila uchao, hapo lazima utakereka tu.

Kibaya zaidi majirani hawakwepeki, njia pekee ya kuwakwepa ni kuuza nyumba au kuipangisha hlf wewe utafute kwingine kwa kukaa, nje ya apo ukae kwa utulivu uku ukiwavumilia na kuwazoea!

"You cant choose a neighbor but u can choose neighborhood "
 
Amenunua bati za ALAF kwa wakala (katoro) lakini zimepauka hat mwaka hazina. Anaomba msaada nini akifanye!
 
Zamani nilikua naona wanaoacha viwanja muda mrefu hawajengi kama wajinga flani hivi.

ila nimekuja gundua kuna maana kubwa sana ya kuacha kiherehere cha kuanza ujenzi kisa una pesa na unaweza.

Kile kiwanja nilinunua enzi ni pori la maana tu,haraka haraka kimbilia jenga..

Tangu zamani nilishasema sitowahi jenga uswahilini, ila sikua najua wanaojenga uswahili hawakuwahi waza kama patakuja kuwa uswahilini.

Baada ya ujenzi miaka kadhaa mbele ule mtaa haukua na tofauti na tandale, ule uswahili,vile vijumba vilivyokua vikichipuka kama uyoga nikajikuta nimewekwa mtu kati, nmezungukwa na vijumba vingiiiiiii...

Nikaona hapa Usintanie,Madalali kazi yao nini? Nikapauza kama palivyo.

Hela yote nimenunulia kiwanja sehemu nyingine, Sijengi ng'o mpaka nihakikishe ule mtaa ni wanaojielewa.

Ntapanga hivi hivi ila siwezi jenga mtaa ambao sina uhakika nawataokuja.

Hii mambo ya kuharakisha kujenga sehemu nyumba ya maana ndio unaweza jikuta unajenga mtaa kama kwa mtogole...

Baadae watoto wanakuuliza baba ilikuaje ukaja kujenga huu mtaa... Unakosa majibu.
Pole sana kaka,, ila kwa sasa hv nashauri kabla hujanunua kiwanja pia angalia ukubwa wa viwanja vya eneo husika, ukiona viwanja ni square mita ndogo mfano 400 jua kabisa ilo eneo makazi yake yatabanana tu, so ni bora kutafuta eneo lingine, tena kwa sasa hv makampuni yakuuza viwanja yalivyo mengi makazi yambeleni yakuwa yakubanana sana
 
Back
Top Bottom