Ni 'Kitchen Party' au 'Bedroom Party'?

Habari ndo hiyo mamii... ni kweli siku hizi ushindani ni kiboko yaani natamani niendelee kuwa single for ever... and I think I will
 
Kizazi kimeuawa na wazazi tunaowategemea kama walinzi wetu. Kitchen party imeharibiwa maana na watu wachache wasiokwua na fikra. West africa kitchen party maana yake ni kumwandaa mwali kuyakabili maisha ya ndo katika nyanja zifuatazo. Kupika, analetwa mtalaam wa kupika anatoa somo, kufua, kufanya usafi, jinsi ya kuishi na watu, wakiwemo wakwe na familia kwa ujumla. Tena kitchen party hiyo siyo ya siku moja ni zaidi ya miezi 3

Huku kwetu wanavyopenda ngono mama watu wazima wanaanza kufundisha watoto vitu vya kipuuzi. Cha kushangaza zaidi anayetoa somo ameachika zaidi ya mara 3, unategema mtu kama huyo ataongea nini kumsaidia mwali.

Nfikiri tufikie hatua tukatae kufanyiwa kitchen party, tuishie kwenye mafundisho ya kanisani yanatosha. Hayo mengine tutayaona huko.


Kitchen Party ni mojawapo ya ishara ya kuonyesha ni kiasi gani jamii ya Watanzania inazidi kukumbwa na adha ya mmomonyoko wa maadili, halafu bado tunakumbatia mambo ya kipuuzi!

Ukweli mimi huwa nikisikia mipango ya kitchen party wakati wa maandalizi ya harusi, huwa napata wasiwasi na uwezo wa kufikiri na kuamua wa bibi harusi mtarajiwa! Wasichana wenye ujasiri huwa wanakataa kufanyiwa kitchen party, hata kama ndugu na wazazi na marafiki watashadadia namna gani!

Its a free World anyways!!!
 
Habari ndo hiyo mamii... ni kweli siku hizi ushindani ni kiboko yaani natamani niendelee kuwa single for ever... and I think I will

Usiwe single forever,huwi mpweke jamani? ha ha
Anyway, siyo lazima ufanye kitchen party zaidi siku muhimu ni ya harusi yako kama utaolewa ila vingine ni manjonjo..
Hata mimi nitafanya hivyo,shughuli yote harusi vingine hata visipokuwepo hakiharibiki kitu..
 
mie nazichukia hizo kitchen party, nilikuwa naendaga coz ni za watu wangu wa karibu lakini ya mwisho niliyoenda na nilisema sitoenda tena kwenye hizo party, hao makungwi walikuwa wanamuambia mtarajiwa" mafiga matatu mtoto wa kike ndio yanayohitajika ndani" "vigaloni ni muhimu kwa binti kama wewe, ndoo ya maji ikimwagika then una kigaloni,kulikuwa hakuna la maana, ni matusi mtindo mmoja, kuanzia hapo nilisitisha kwenda kwenye kitu kinachoitwa kichen party! kwa upande wangu hazisaidii, ni wamama watu wazima kabisa wanayaongea hayo badala ya kumjenga binti niliona wanambomolea kabla hata hajaingia ndani, kama alivyosema hapo juu shangazi na bibi wanatosha.

...eboo! ok, kuanzia sasa ni marufuku wife kwenda huko!
 
Mwee, kwa kweli hata mimi nilipoolewa katika hii karne ya dot com, nilikataa katukatu kitchen party na nikamwambia mama yangu aliyenizaa anipie hayo mambo yaongelewayo huko la sivyo nipige kona na speed 120 nianze zangu. Kwa kweli nilihudhuriaga only one kitchen party in my life and i did not see the meaning at all. Alafu hivi kwa sasa hivi mtu kweli na akili zake anakaa kabisa chini na kumfunda mwali sijui jinsi ya kuishi na mwanume...ukizingatia wameshapita idadi fulani ya wanaume. Booh! kweli watu wanahangaisha au wanawake wanatafuta sehemu tuu za kutokea maana wamezidi kuachwa majumbani na wakina baba.
 
Too late my dear...!lol
...wanawake wanatafuta sehemu tuu za kutokea maana wamezidi kuachwa majumbani na wakina baba.

...na kweli, maana kitchen party J'5 na J'2, ...na sare wanashonesha,...duh!
kitchen party gani zisoisha kila wiki?

...halafu kina mama mmekuja na mpya nyingine, eti Baby shower! khaaaaa!?
 
Mwee, kwa kweli hata mimi nilipoolewa katika hii karne ya dot com, nilikataa katukatu kitchen party na nikamwambia mama yangu aliyenizaa anipie hayo mambo yaongelewayo huko la sivyo nipige kona na speed 120 nianze zangu. Kwa kweli nilihudhuriaga only one kitchen party in my life and i did not see the meaning at all. Alafu hivi kwa sasa hivi mtu kweli na akili zake anakaa kabisa chini na kumfunda mwali sijui jinsi ya kuishi na mwanume...ukizingatia wameshapita idadi fulani ya wanaume. Booh! kweli watu wanahangaisha au wanawake wanatafuta sehemu tuu za kutokea maana wamezidi kuachwa majumbani na wakina baba.


kuna ma coleague hapa alikuwa anaolewa mwanzoni mwa mwaka, ameishi na man wake kama wachumba mpaka wakapata mtoto leo wanataka ndoa anadai mchango wa kitchen party nilimuuliza hivi yani hata wewe unapasha kiporo unahitaji kitchen party"?...sielew maana maalumu ya kitchen party za siku hizi! mtoto ana miaka 2 unahitaji hiyo kitu! mwehhh
 
...na kweli, maana kitchen party J'5 na J'2, ...na sare wanashonesha,...duh!
kitchen party gani zisoisha kila wiki?

...halafu kina mama mmekuja na mpya nyingine, eti Baby shower! khaaaaa!?


haaaa juzi nilikuwa kwenye baby shower! unaandikiwa kabisa kwenye card zawadi utakatomletea mtoto!....so usiende kinyume.
 
mie nazichukia hizo kitchen party, nilikuwa naendaga coz ni za watu wangu wa karibu lakini ya mwisho niliyoenda na nilisema sitoenda tena kwenye hizo party, hao makungwi walikuwa wanamuambia mtarajiwa" mafiga matatu mtoto wa kike ndio yanayohitajika ndani" "vigaloni ni muhimu kwa binti kama wewe, ndoo ya maji ikimwagika then una kigaloni,kulikuwa hakuna la maana, ni matusi mtindo mmoja, kuanzia hapo nilisitisha kwenda kwenye kitu kinachoitwa kichen party! kwa upande wangu hazisaidii, ni wamama watu wazima kabisa wanayaongea hayo badala ya kumjenga binti niliona wanambomolea kabla hata hajaingia ndani, kama alivyosema hapo juu shangazi na bibi wanatosha.


Mrs ndo maana nilikukataza ile ya juzi juzi hapa..zimepoteza mwelekeo kabisa
 
Ngoja nikaanze mwanzo. Hii Sred imenipita hapa sielewi kitu.
 
siku hizi mbona kila kitu kinguvu nguvu tu mantiki nzima ya zawadi haipo tena

Ndio maana watu wanaishia kupata glass nyingi kama mtaji wa kibanda cha Juice...ndio maana wamekuja na style mpya wee lete 30thou yako sisi tutaenda kutafuta zawadi....sasa jinsi panga linavyokatwa huko! Wee acha tu. Nusu kwa mhusika nusu wanunuzi. Wahusika nao wamekuja juu unakuta wao wanaenda kujinunulia zawadi! Mantiki kwishnehi!
 
Back
Top Bottom