Ni kazi rahisi sana kupata A ila ni vigumu sana kuitetea A yako

GedsellianTz

JF-Expert Member
Jul 5, 2016
1,335
1,778
Vyuoni kuna kila aina ya wanafunzi na baada ya graduation kuna product tofauti za wanafunzi tofauti toka vyuo tofauti sana hapa Tanzania,ukiona mtu ana copy post pasipo appreciation ya mtunzi wa post harafu ni msomi basi jua huyo ni product hii inaitwa Selfie-Graduate kupiga chabo,

Ukiona mtu msomi anatukana watu ,jua anatoka hii product ya selfie Graduate,Ukiona mwanaume msomi anampiga mwanamke basi jua ni Selfie -Graduate,ukiona mwanaume anavaa mlegezo na ni msomi wewe jua huyo ni Selfie Graduate,ukiona mwanaume anahonga sana kuliko kusaidia familia yake jua ni Selfie -Graduate.

Elimu yenye mashiko ni ile yenye tija na ufahamu wa kutosha kwa muhusika na jamii inayomzunguka .Sasa kama una degree ya kutizamia unawezaje kuwa na utashi wa kupambanua mambo kwa kina?Tafakari si kila msomi ni msomi wengine wana A za makaratasi na ubongo wao ni F za mawazo na matendo.Being quiet is fine, most people don’t listen anyways.
 
Back
Top Bottom