Ni kama ilivyoandikwa kwenye Biblia "wana macho lakini hawaoni"

Juliana Shonza

JF-Expert Member
Dec 19, 2012
2,009
1,607
"Wana macho lakini hawaoni" - Ni nukuu maarufu iliyopo katika vitabu mbalimbali vya dini, ipo katika Biblia na ipo katika Quran. Kwenye Biblia nukuu hiyo imetajwa maeneo mengi kama vile Mathayo 13, Ezekieli 12 n.k.....Kimsingi nukuu hii inawazungumzia BINADAMU ambao huwa HAWAFIKIRI sawasawa, binadamu waliofungwa fikra zao.

Kwa kuwa hii ni thread yangu kwa mwaka huu, na kwa kuwa nimekuwa kimya katika jukwaa hili kwa takribani miezi 3, shule imekaba kidogo. Naomba niitumie thread hii kutoa salamu zangu za heri ya mwaka mpya kwa wana jamvi wote na pia kutoa pole kwa Makamanda kwa kumpoteza mpambanaji muhimu ambaye KUBENEA anadai AMEJITEKA, rafiki yangu Bernard Rabiu Saanane.

Mwaka 2015 niliwahi kuandika CHADEMA kuna Ombwe la Uongozi na baadae mwezi wa nane mwaka jana 2016 nikaandika tena Msisitizo; CHADEMA kuna ombwe la uongozi leo kwa mara nyingine tena nalazimika kuandika mfano wa maneno hayo, hasa baada ya kusoma kilichoandikwa na Mhe Mbunge John Heche jana na baadae Mtatiro leo asubuhi. NI WAZI MANENO YAO YANDHIHIRISHA KUWA UPINZANI WA NCHI YETU UNA OMBWE KUBWA LA UONGOZI.

Ni ujinga tena upumbavu uliokomaa ambao wajuzi wa mambo wanaita "umbumbumbu" kwa wapinzani kuendelea kuvinyooshea kidole vyombo vya dola kila baada ya kushindwa uchaguzi.

MWENYEKITI Mtatiro anaposema CCM inaitumia DOLA, inatumia NEC, inatumia Rushwa, inatumia Hila, inatumia Mabavu wakati tunajua kuwa Mgombea wa CUF jimbo la Dimani hata fomu yake iliyopelekwa NEC haijapita kwenye ofisi ya Mwenyekiti wake, yaani kwa mgogoro mliouasisi wenyewe, mkaupalilia na kuuwekea mbolea kisha leo mgombea wenu anaposhindwa, bila aibu, bila hata soni unatoka mbele ya umma kusema umeshindwa uchaguzi kwa hila na kwa kuwa CCM inatumia Dola na kwamba NEC inatumika...tafadhali sana acha UJINGA wa namna hii. Ni kweli CUF ilitegemea USHINDI...seriously kabisa..???

Lakini ukweli ambao mmeendelea kuupuuza ni ule unaoendelea kudhihirika kuwa WATANZANIA sio WAJINGA...mlisimama na kumnadi Lowassa kuwa ni mwizi katika kila kona ya Nchi hii, leo ndio anasimama kwenye kila jukwaa lenu akinadi wagombea wenu wa Ubunge na Udiwani, na kila alipokanyaga Lowasa kwenye Kampeni mmeshindwa...mnasema CCM inatumia Dola...Watanzania sio wajinga.

Kimsingi Umaarufu wa UFIPA umepungua..,leo haitajwi tena UFIPA, inatajwa Lumumba, Haitajwi tena CHADEMA anatajwa LOWASSA, mmeendelea kumnawirisha mtu badala ya Chama, leo Mbowe hasikiki, Katibu Mkuu Mashinji ndio kabisa kama vile ni mfu, BAVICHA wanagombana na Vodacom na wanaidai Serikali iwarudishie Ben Saanane akiwa HAI tena asiwe hata na uvimbe wala mchubuko....then mnataka kushinda uchaguzi,,,HOW..? Hakuna hata hoja moja ya Wananchi mnayoisimamia, sio Rushwa, sio Ajira, sio Huduma za Maji, sio Umeme, sio Miundombinu, sio Bei za Vyakula/Mazao. CCM wanao ujasiri wa kutaja rushwa, wanaujasiri wa kuzungumzia maji, Waziri wa CCM anasema kuhusu bei ya Umeme, Rais anayetokana na CCM anaitengeneza upya TANESCO, CCM inawaneemesha wakulima kwa bei za mazao kupanda (kwa mara ya kwanza kwenye historia ya Nchi hii Korosho imeuzwa kufikia 5000 kwa kilo.)

Mnaposimamia na kupigania mambo ya kipuuzi kwenye mitandao na magazeti na kuyaacha mambo ya msingi, WANANCHI nao wanawaonesheni Upuuzi unaolingana na ule mliowaonesha.

Samahani sana nimetumia lugha kali kidogo, lakini ndivyo ilivyo Ujinga wa Mwafrika bila kiboko hautoki kirahisi..!!
 
haya wamekusikia ila bado una mahaba na chadema ,maana kila uchao wewe nikuandika habari za chadema tu kwanini hauandiki za ccm chama chako?
 
THANK YOU FOR THIS NOON BLAH-BLAH..../
HAKUNA ISSUE AU MANTIKI YOYOTE HAPO..!/
•HUKO CHUONI UNASOMEA FANI GANI?...
*Nasikitika sana na aina ya wasomi / TARAJIWA..
-->>eti hii ndio thread yako ya kwanza 2017...(makini)...!?
LORD GOD HAVE MERCYON US.
 
Bado unaiota CHADEMA.Jiulize umewafanyia nini wapigakura wako maana bado kidogo muda wako wa Ubunge maalum uishe.
 
Wanaugulia maumivu wanafikiria watanzania wote wapo JF kusoma vijembe vyao na kumtukana Magufuli, hizo ni rasharasha tu pigo linawajia 2020.
 
umesema unasoma,lakini naona yale yale ya maprofesa wetu,yani kweli ushindwe kujua kwamba watu kufanya siasa imekuwa ni kosa la jinai?yani wengine waruhusiwe kufanya mikutano popote wengine wapigwe virungu?waweke mazingira sawa ya kufanya siasa ndo tufanye tasmini sio kwa hali ilivyo hivi sasa.
 
umesema unasoma,lakini naona yale yale ya maprofesa wetu,yani kweli ushindwe kujua kwamba watu kufanya siasa imekuwa ni kosa la jinai?yani wengine waruhusiwe kufanya mikutano popote wengine wapigwe virungu?waweke mazingira sawa ya kufanya siasa ndo tufanye tasmini sio kwa hali ilivyo hivi sasa.
Inawezekana ni kweli kuwa tatizo la elimu yetu ni kubwa kuliko nilivyodhani hapo awali..
 
"Wana macho lakini hawaoni" - Ni nukuu maarufu iliyopo katika vitabu mbalimbali vya dini, ipo katika Biblia na ipo katika Quran. Kwenye Biblia nukuu hiyo imetajwa maeneo mengi kama vile Mathayo 13, Ezekieli 12 n.k.....Kimsingi nukuu hii inawazungumzia BINADAMU ambao huwa HAWAFIKIRI sawasawa, binadamu waliofungwa fikra zao.

Kwa kuwa hii ni thread yangu kwa mwaka huu, na kwa kuwa nimekuwa kimya katika jukwaa hili kwa takribani miezi 3, shule imekaba kidogo. Naomba niitumie thread hii kutoa salamu zangu za heri ya mwaka mpya kwa wana jamvi wote na pia kutoa pole kwa Makamanda kwa kumpoteza mpambanaji muhimu ambaye KUBENEA anadai AMEJITEKA, rafiki yangu Bernard Rabiu Saanane.

Mwaka 2015 niliwahi kuandika CHADEMA kuna Ombwe la Uongozi na baadae mwezi wa nane mwaka jana 2016 nikaandika tena Msisitizo; CHADEMA kuna ombwe la uongozi leo kwa mara nyingine tena nalazimika kuandika mfano wa maneno hayo, hasa baada ya kusoma kilichoandikwa na Mhe Mbunge John Heche jana na baadae Mtatiro leo asubuhi. NI WAZI MANENO YAO YANDHIHIRISHA KUWA UPINZANI WA NCHI YETU UNA OMBWE KUBWA LA UONGOZI.

Ni ujinga tena upumbavu uliokomaa ambao wajuzi wa mambo wanaita "umbumbumbu" kwa wapinzani kuendelea kuvinyooshea kidole vyombo vya dola kila baada ya kushindwa uchaguzi.

MWENYEKITI Mtatiro anaposema CCM inaitumia DOLA, inatumia NEC, inatumia Rushwa, inatumia Hila, inatumia Mabavu wakati tunajua kuwa Mgombea wa CUF jimbo la Dimani hata fomu yake iliyopelekwa NEC haijapita kwenye ofisi ya Mwenyekiti wake, yaani kwa mgogoro mliouasisi wenyewe, mkaupalilia na kuuwekea mbolea kisha leo mgombea wenu anaposhindwa, bila aibu, bila hata soni unatoka mbele ya umma kusema umeshindwa uchaguzi kwa hila na kwa kuwa CCM inatumia Dola na kwamba NEC inatumika...tafadhali sana acha UJINGA wa namna hii. Ni kweli CUF ilitegemea USHINDI...seriously kabisa..???

Lakini ukweli ambao mmeendelea kuupuuza ni ule unaoendelea kudhihirika kuwa WATANZANIA sio WAJINGA...mlisimama na kumnadi Lowassa kuwa ni mwizi katika kila kona ya Nchi hii, leo ndio anasimama kwenye kila jukwaa lenu akinadi wagombea wenu wa Ubunge na Udiwani, na kila alipokanyaga Lowasa kwenye Kampeni mmeshindwa...mnasema CCM inatumia Dola...Watanzania sio wajinga.

Kimsingi Umaarufu wa UFIPA umepungua..,leo haitajwi tena UFIPA, inatajwa Lumumba, Haitajwi tena CHADEMA anatajwa LOWASSA, mmeendelea kumnawirisha mtu badala ya Chama, leo Mbowe hasikiki, Katibu Mkuu Mashinji ndio kabisa kama vile ni mfu, BAVICHA wanagombana na Vodacom na wanaidai Serikali iwarudishie Ben Saanane akiwa HAI tena asiwe hata na uvimbe wala mchubuko....then mnataka kushinda uchaguzi,,,HOW..? Hakuna hata hoja moja ya Wananchi mnayoisimamia, sio Rushwa, sio Ajira, sio Huduma za Maji, sio Umeme, sio Miundombinu, sio Bei za Vyakula/Mazao. CCM wanao ujasiri wa kutaja rushwa, wanaujasiri wa kuzungumzia maji, Waziri wa CCM anasema kuhusu bei ya Umeme, Rais anayetokana na CCM anaitengeneza upya TANESCO, CCM inawaneemesha wakulima kwa bei za mazao kupanda (kwa mara ya kwanza kwenye historia ya Nchi hii Korosho imeuzwa kufikia 5000 kwa kilo.)

Mnaposimamia na kupigania mambo ya kipuuzi kwenye mitandao na magazeti na kuyaacha mambo ya msingi, WANANCHI nao wanawaonesheni Upuuzi unaolingana na ule mliowaonesha.

Samahani sana nimetumia lugha kali kidogo, lakini ndivyo ilivyo Ujinga wa Mwafrika bila kiboko hautoki kirahisi..!!
Kama tatizo la CDM kutofanya vizuri ni ombwe la uongozi, najiuliza vyama vya upinzani vipo Vingi tu inakuwaje CDM yenye ombwe la uongozi iko vizuri kuliko vingine vya upinzani ambavyo wewe hujawahi viongelea?
 
Wewe binti Juliana Shonza, hebu epuka sana kutumia vitabu vitakatifu vya dini kwenye porojo na propaganda zako. Jaribu kujenga hoja bila kuhusisha mambo ya kidini. Mara kwa mara najiuliza, na hata kuidharau CHADEMA, ilikuwaje mtu mwenye uelewa kama wako ulikuwa Makamu Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa?
Kama kipimo chako cha weledi/umakini wa mtu ni kuwa Kiongozi wa BAVICHA..,sishangai ni kwanini umeamua kuifanya JF ni sehemu ya ajira yako. Aliwazalo ...*...*...*...ndilo litakalomfika.
 
CHADEMA wametetea Kata yao Moja waliyokuwa nayo.
CCM haijaweza kuchukua Kata yoyote kutoka CHADEMA.
Sioni kama uchambuzi wako una lolote jipya.
Ni kweli hauna jipya, na kama umeusoma vizuri unaweza kuona kuwa nimenukuu yale ya zamani kutoka vitabu vya dini na niliyowahi kuyaandika binafsi..Uko sahihi kabisa.
 
Kama tatizo la CDM kutofanya vizuri ni ombwe la uongozi, najiuliza vyama vya upinzani vipo Vingi tu inakuwaje CDM yenye ombwe la uongozi iko vizuri kuliko vingine vya upinzani ambavyo wewe hujawahi viongelea?
Kwa Comparison rahisi tu..,ACT iko vizuri kuliko chama chochote cha Upinzani kwa sasa..Kasi ya ukuaji wake na kukubalika kwa watu inatosha kuelezea Chama kiko katika hali gani.
 
Bado unaiota CHADEMA.Jiulize umewafanyia nini wapigakura wako maana bado kidogo muda wako wa Ubunge maalum uishe.
Sina sababu ya kujiuliza wakati najua exactly nilichokifanya na ninachokifanya. Labda uniulize ili nikufafanulie.
 
"Wana macho lakini hawaoni" - Ni nukuu maarufu iliyopo katika vitabu mbalimbali vya dini, ipo katika Biblia na ipo katika Quran. Kwenye Biblia nukuu hiyo imetajwa maeneo mengi kama vile Mathayo 13, Ezekieli 12 n.k.....Kimsingi nukuu hii inawazungumzia BINADAMU ambao huwa HAWAFIKIRI sawasawa, binadamu waliofungwa fikra zao.

Kwa kuwa hii ni thread yangu kwa mwaka huu, na kwa kuwa nimekuwa kimya katika jukwaa hili kwa takribani miezi 3, shule imekaba kidogo. Naomba niitumie thread hii kutoa salamu zangu za heri ya mwaka mpya kwa wana jamvi wote na pia kutoa pole kwa Makamanda kwa kumpoteza mpambanaji muhimu ambaye KUBENEA anadai AMEJITEKA, rafiki yangu Bernard Rabiu Saanane.

Mwaka 2015 niliwahi kuandika CHADEMA kuna Ombwe la Uongozi na baadae mwezi wa nane mwaka jana 2016 nikaandika tena Msisitizo; CHADEMA kuna ombwe la uongozi leo kwa mara nyingine tena nalazimika kuandika mfano wa maneno hayo, hasa baada ya kusoma kilichoandikwa na Mhe Mbunge John Heche jana na baadae Mtatiro leo asubuhi. NI WAZI MANENO YAO YANDHIHIRISHA KUWA UPINZANI WA NCHI YETU UNA OMBWE KUBWA LA UONGOZI.

Ni ujinga tena upumbavu uliokomaa ambao wajuzi wa mambo wanaita "umbumbumbu" kwa wapinzani kuendelea kuvinyooshea kidole vyombo vya dola kila baada ya kushindwa uchaguzi.

MWENYEKITI Mtatiro anaposema CCM inaitumia DOLA, inatumia NEC, inatumia Rushwa, inatumia Hila, inatumia Mabavu wakati tunajua kuwa Mgombea wa CUF jimbo la Dimani hata fomu yake iliyopelekwa NEC haijapita kwenye ofisi ya Mwenyekiti wake, yaani kwa mgogoro mliouasisi wenyewe, mkaupalilia na kuuwekea mbolea kisha leo mgombea wenu anaposhindwa, bila aibu, bila hata soni unatoka mbele ya umma kusema umeshindwa uchaguzi kwa hila na kwa kuwa CCM inatumia Dola na kwamba NEC inatumika...tafadhali sana acha UJINGA wa namna hii. Ni kweli CUF ilitegemea USHINDI...seriously kabisa..???

Lakini ukweli ambao mmeendelea kuupuuza ni ule unaoendelea kudhihirika kuwa WATANZANIA sio WAJINGA...mlisimama na kumnadi Lowassa kuwa ni mwizi katika kila kona ya Nchi hii, leo ndio anasimama kwenye kila jukwaa lenu akinadi wagombea wenu wa Ubunge na Udiwani, na kila alipokanyaga Lowasa kwenye Kampeni mmeshindwa...mnasema CCM inatumia Dola...Watanzania sio wajinga.

Kimsingi Umaarufu wa UFIPA umepungua..,leo haitajwi tena UFIPA, inatajwa Lumumba, Haitajwi tena CHADEMA anatajwa LOWASSA, mmeendelea kumnawirisha mtu badala ya Chama, leo Mbowe hasikiki, Katibu Mkuu Mashinji ndio kabisa kama vile ni mfu, BAVICHA wanagombana na Vodacom na wanaidai Serikali iwarudishie Ben Saanane akiwa HAI tena asiwe hata na uvimbe wala mchubuko....then mnataka kushinda uchaguzi,,,HOW..? Hakuna hata hoja moja ya Wananchi mnayoisimamia, sio Rushwa, sio Ajira, sio Huduma za Maji, sio Umeme, sio Miundombinu, sio Bei za Vyakula/Mazao. CCM wanao ujasiri wa kutaja rushwa, wanaujasiri wa kuzungumzia maji, Waziri wa CCM anasema kuhusu bei ya Umeme, Rais anayetokana na CCM anaitengeneza upya TANESCO, CCM inawaneemesha wakulima kwa bei za mazao kupanda (kwa mara ya kwanza kwenye historia ya Nchi hii Korosho imeuzwa kufikia 5000 kwa kilo.)

Mnaposimamia na kupigania mambo ya kipuuzi kwenye mitandao na magazeti na kuyaacha mambo ya msingi, WANANCHI nao wanawaonesheni Upuuzi unaolingana na ule mliowaonesha.

Samahani sana nimetumia lugha kali kidogo, lakini ndivyo ilivyo Ujinga wa Mwafrika bila kiboko hautoki kirahisi..!!
Huyu mama mbona anaipenda sana chaema? Inamaana CCM upo kama kiwiliwili tu roho iko Chadwma?
 
Kama kipimo chako cha weledi/umakini wa mtu ni kuwa Kiongozi wa BAVICHA..,sishangai ni kwanini umeamua kuifanya JF ni sehemu ya ajira yako. Aliwazalo ...*...*...*...ndilo litakalomfika.
Na wewe binti umezidi, sasa kwa nini usitumie muda wako wa kutosha kukiandika na kukipiginia chama chako kinachokusaidia kupata mkate wako wa kila siku, na badala yake unakazana kukiandika chama chako cha zamani, kitu ambacho hakitakusaidia?
 
Back
Top Bottom