Tukirudi kwenye mada, lililo wazi ni kwamba role ya Karume kwenye mapinduzi ilikuwa ndogo sana!
Architects wakubwa wa Mapinduzi ya Zanzibar ni Umma Party chini ya Abdulrahman Babu. Ni hawa Umma Party ndio walipeleka vijana wao Cuba kuchukua mafunzo ya kijeshi na waliporudi Zanzibar walikuwa tayari wamekwiva kwa mapinduzi!
Si tu kwamba walirudi wakiwa wamekwiva kwelikweli kimapinduzi bali pia walikuwa wamekwiva na itikadi ya ukomunist!
REMEMBER, hii ilikuwa ni takribani miaka 5 tangu kutokea kwa mapinduzi ya Cuba na vugu vugu la ukomunist lilikuwa juu huko Cuba na ndio maana haikushangaza vijana wa Babu walirudi wakiwa ni wakomunist waliokwiva!!
Hata hivyo, Karume alikuwa na mtaji mkubwa zaidi wa watu kuliko Babu kwa sababu Karume alikuwa anaongoza ASP ambayo ilikuwa na ushawishi mkubwa sana Unguja ambako ndiko kwenye population kubwa. Kutokana na ukweli huo, hapakuwa na njia ya mkato zaidi ya Karume na Babu ku-team up ingawaje inasemekana Karume alifichwa suala zima la mapinduzi na kama alifahamu, basi alifahmu kinagaubaga tu!!!
To make story short, katika kufikia mapinduzi palitakiwa awepo kiongozi wa mapinduzi! Kwavile hapakuwa na uhakika wa kufanikiwa, ikaonekana Babu au hata Karume (kama alifahamu) wasiwe mstari wa mbele! Hii ni kwavile, endapo mapinduzi yange-fail na endapo mmoja wao au wote hao wangekuwa ndio viongozi wa mapinduzi; ambacho kingefuata hapo kila mmoja anafahamu na bila shaka harakati zote zingepunguzwa nguvu! Hapa ndipo alipoingia Okello.
Okello akapelekwa mstari wa mbele... ama kwa kufahamu au kutofahamu ili endapo mapinduzi yangeshidwa; jumba bovu lingemdondokea yeye na kuwaacha akina Babu, at least kwa muda!!
Hivyo basi, ambae aliongoza mapinduzi practically ni John Okello raia wa Uganda. Wakati haya yanatokea; si Abdulrahman Babu wala Karume walikuwa Zanzibar bila shaka kwa sababu ile ile kwamba endapo yangeshindwa; wasiweze kuhusishwa na kama wangehusishwa basi ingewawea rahisi kukwepa mkono wa serikali ya akina Shamte!!!!