thomas_360
JF-Expert Member
- Oct 11, 2015
- 1,458
- 1,436
Napenda kutanguliza shukrani kwa mwenyezi Mungu kwa kuweza kunipa pumzi ya uhai mpaka dakika hii, kuna waliotamani kuiona siku ya leo ila kwa neema yake wametangulia mbele za haki.
Napenda kutanguliza shukrani kwa kuweza kunipigania tangu naanza chuo mpaka nahitimu, haikuwa kazi rahisi ila yote ni kwa neema yake.
Hivyo napenda kuwaomba wadogo zangu, ndugu zangu ambao mwaka huu mnaingia mwaka wa kwanza, kwa wale waliobahatika kupata fursa hiyo basi ni vyema kumshukuru mungu iwe kwa ngazi ya Certificate, Diploma au Degree.
lakini pia Pia nawasihi mtumie fursa hiyo mliopata vizuri, muweze kuitendea haki na kuipigania. Usidharau kitu katika kusoma kwako kila kitu kichukilie kama chalenge katika mafanikio yako...siku zote tambua kuwa kuteleza sio kuanguka, hivyo basi pale unapoteleza hebu nyanyuka na ujipange upya.
Pia kwa wale ndugu zangu ambao wamefanikiwa kupata mkopo mwaka huu, tusishangilie sana bali tumshukuru Mungu kwa yote yaliyotendeka, lakini pia kwa wale ambao hawajabahatika kupata huo mkopo hebu tusikate tamaa kila jambo huwa linatendeka for reason...ila kwa wale waliopata mkopo siwezi kuwashauri namna ya kutumia mkopo wako bali ni jukumu lako kuamua namna utakavyolitumia maana wakati ukifika wa kulirudisha utapambana na hali yako kulirudisha ili na wengine wanufaike pie..
Kwa wale ndugu zangu tunaendelea na masomo hebu tujitizame tilipotoka na tunapoelekea kimasomo kama maendeleo yako sio mazuri hebu jaribu kujipanga kwa mwaka huu uongeze bidii..kudisco kwa mtu chuoni huja automatic na usipojipanga mapema utakuja kujutia..inauma sana mtu kudisco ukiwa mwaka wa kwanza au wa tatu...nina mifano hai na inaniuma sana..na wimbi kubwa la watu huwa wanadisco miaka hiyo kwa program za miaka mitatu...
Then kwa wale ambao tumehitimu mwaka huu na ambao tayari wapo kitaa tusikate tamaa kama bado hatujapata channel za maana ipo siku naamini tutakula matunda ya miche tuliyoipanda....nashukuru sana kwa wewe uliyeweza kusoma ujumbe huu na kama unachochote basi tusaidiane hii ni Tanzania yetu na sisi ndo Watanzania wenyewe...
Napenda kutanguliza shukrani kwa kuweza kunipigania tangu naanza chuo mpaka nahitimu, haikuwa kazi rahisi ila yote ni kwa neema yake.
Hivyo napenda kuwaomba wadogo zangu, ndugu zangu ambao mwaka huu mnaingia mwaka wa kwanza, kwa wale waliobahatika kupata fursa hiyo basi ni vyema kumshukuru mungu iwe kwa ngazi ya Certificate, Diploma au Degree.
lakini pia Pia nawasihi mtumie fursa hiyo mliopata vizuri, muweze kuitendea haki na kuipigania. Usidharau kitu katika kusoma kwako kila kitu kichukilie kama chalenge katika mafanikio yako...siku zote tambua kuwa kuteleza sio kuanguka, hivyo basi pale unapoteleza hebu nyanyuka na ujipange upya.
Pia kwa wale ndugu zangu ambao wamefanikiwa kupata mkopo mwaka huu, tusishangilie sana bali tumshukuru Mungu kwa yote yaliyotendeka, lakini pia kwa wale ambao hawajabahatika kupata huo mkopo hebu tusikate tamaa kila jambo huwa linatendeka for reason...ila kwa wale waliopata mkopo siwezi kuwashauri namna ya kutumia mkopo wako bali ni jukumu lako kuamua namna utakavyolitumia maana wakati ukifika wa kulirudisha utapambana na hali yako kulirudisha ili na wengine wanufaike pie..
Kwa wale ndugu zangu tunaendelea na masomo hebu tujitizame tilipotoka na tunapoelekea kimasomo kama maendeleo yako sio mazuri hebu jaribu kujipanga kwa mwaka huu uongeze bidii..kudisco kwa mtu chuoni huja automatic na usipojipanga mapema utakuja kujutia..inauma sana mtu kudisco ukiwa mwaka wa kwanza au wa tatu...nina mifano hai na inaniuma sana..na wimbi kubwa la watu huwa wanadisco miaka hiyo kwa program za miaka mitatu...
Then kwa wale ambao tumehitimu mwaka huu na ambao tayari wapo kitaa tusikate tamaa kama bado hatujapata channel za maana ipo siku naamini tutakula matunda ya miche tuliyoipanda....nashukuru sana kwa wewe uliyeweza kusoma ujumbe huu na kama unachochote basi tusaidiane hii ni Tanzania yetu na sisi ndo Watanzania wenyewe...