cutelove
JF-Expert Member
- Oct 3, 2017
- 3,317
- 7,509
Katika familia moja ya ndugu yangu,kuna ugomvi mkubwa umetokea
Katika mzozano huo wakaanza hadi kupigana ambapo mwanamke alianza kupiga kelele akiomba msaada kutokana na kipigo cha mmewe
Mwanaume jirani anafika,anataka kuamua ule ugomvi,lakini mume wa mwanamke anaanza kupigana na huyo mwanaume jirani yao kwa sababu ya hasira na kuingilia ugomvi
Mwanaume aliyekuja kusaidia anaona jamaa kama amehamishia hasira kwake,naye anaanza kujihami,anamkunja yule mwanaume na kipondo kikali anamzidi nguvu na kumkalia kifuani na kuanza kumniga
Mwanamke anaona kama mume wake anaumia,anamshika yule jirani amuache mumewe
Ugomvi unazidi na jamaa anazidi kumshambulia mumewe
Mwanamke anachukua kigoda anampiga kichwani yule mwanaume aliyekuja kusaidia hadi anazimia
Baadae watu wakawa wamesaidia pale na akarudisha fahamu na kumhoji,kwa nini uingilie ugomvi usiokuhusu hasa wa mke na mume
Kwani jaman ni vibaya kuamua ugomvi wa wanandoa
Katika mzozano huo wakaanza hadi kupigana ambapo mwanamke alianza kupiga kelele akiomba msaada kutokana na kipigo cha mmewe
Mwanaume jirani anafika,anataka kuamua ule ugomvi,lakini mume wa mwanamke anaanza kupigana na huyo mwanaume jirani yao kwa sababu ya hasira na kuingilia ugomvi
Mwanaume aliyekuja kusaidia anaona jamaa kama amehamishia hasira kwake,naye anaanza kujihami,anamkunja yule mwanaume na kipondo kikali anamzidi nguvu na kumkalia kifuani na kuanza kumniga
Mwanamke anaona kama mume wake anaumia,anamshika yule jirani amuache mumewe
Ugomvi unazidi na jamaa anazidi kumshambulia mumewe
Mwanamke anachukua kigoda anampiga kichwani yule mwanaume aliyekuja kusaidia hadi anazimia
Baadae watu wakawa wamesaidia pale na akarudisha fahamu na kumhoji,kwa nini uingilie ugomvi usiokuhusu hasa wa mke na mume
Kwani jaman ni vibaya kuamua ugomvi wa wanandoa