Hodi jamvini
Naomba ushauri wenu juu ya yatokanayo na mapenzi katika jamii yetu.
Juzi nilikuwa na wakati mgumu baada ya rafiki yangu wa karibu kuniletea nakala ya usia wa ?mali zake?. Yeye ni rafiki yangu wa karibu tumesoma wote sekondari na hata jeshini tulikuwa intake moja ?operesheni Nidhamu?. Ni baba wa familia ya watoto watatu na ni mpenda dini kwelikweli.
Mwanzoni nilidhani kuwa ule usia ulikuwa kwa nia njema ya kuuhifadhi lakini wakati namsindikiza (alikataa mke wangu asimsindikize) ndipo akaniambia kuwa amefikia uamuzi wa kujiua au kuua au vyote viwili. Baada ya kumhoji akadai kuwa kuna mpenzi (Mchepuko) ambaye amemkataa na juhudi zote za kumrejesha kundini kushindikana.
Mwanzoni nilidharau lakini tone na muanekano wake uliashiria kuwa aliimaanisha alichokiamua. Baada ya kumhoji sana niliamua kumpigia mchepuko na kukubaliana kukutana siku ilele jioni maeneo ya Kijichi. Kilichojiri wakati wa mahojiano ni pamoja na mchepuko ?mchepuko ulikuja unadrive ingawa sikuona kadi ya gari ina jina gani? kutamka waziwazi kuwa uwezo wa jamaa kuhudumia umefika mwisho na hawezi tena kuendelea na uhusiano.
Sababu ya pili ni kwamba mke wa rafiki yangu alishahisi mahusiano yao jambo ambalo jamaa alikiri kuwa alishaulizwa sana juu ya hilo. Isitoshe mchepuko ulieleza wazi bila chenga kuwa sasa kafunguliwa biashara duka la nguo maeneo ya msasani na ndio sababu ya kuhama kijichi.
Baada ya mazungumzo marefu tulikubaliana tupeane muda kila mtu akatafakari tukutane jumapili.Najua huenda uamuzi huu ni temporary solution.
Nini kifanyike waungwana? Ni haki kutoa roho ya binadamu yeyote kwa ajili ya mapenzi?
Naomba ushauri wenu juu ya yatokanayo na mapenzi katika jamii yetu.
Juzi nilikuwa na wakati mgumu baada ya rafiki yangu wa karibu kuniletea nakala ya usia wa ?mali zake?. Yeye ni rafiki yangu wa karibu tumesoma wote sekondari na hata jeshini tulikuwa intake moja ?operesheni Nidhamu?. Ni baba wa familia ya watoto watatu na ni mpenda dini kwelikweli.
Mwanzoni nilidhani kuwa ule usia ulikuwa kwa nia njema ya kuuhifadhi lakini wakati namsindikiza (alikataa mke wangu asimsindikize) ndipo akaniambia kuwa amefikia uamuzi wa kujiua au kuua au vyote viwili. Baada ya kumhoji akadai kuwa kuna mpenzi (Mchepuko) ambaye amemkataa na juhudi zote za kumrejesha kundini kushindikana.
Mwanzoni nilidharau lakini tone na muanekano wake uliashiria kuwa aliimaanisha alichokiamua. Baada ya kumhoji sana niliamua kumpigia mchepuko na kukubaliana kukutana siku ilele jioni maeneo ya Kijichi. Kilichojiri wakati wa mahojiano ni pamoja na mchepuko ?mchepuko ulikuja unadrive ingawa sikuona kadi ya gari ina jina gani? kutamka waziwazi kuwa uwezo wa jamaa kuhudumia umefika mwisho na hawezi tena kuendelea na uhusiano.
Sababu ya pili ni kwamba mke wa rafiki yangu alishahisi mahusiano yao jambo ambalo jamaa alikiri kuwa alishaulizwa sana juu ya hilo. Isitoshe mchepuko ulieleza wazi bila chenga kuwa sasa kafunguliwa biashara duka la nguo maeneo ya msasani na ndio sababu ya kuhama kijichi.
Baada ya mazungumzo marefu tulikubaliana tupeane muda kila mtu akatafakari tukutane jumapili.Najua huenda uamuzi huu ni temporary solution.
Nini kifanyike waungwana? Ni haki kutoa roho ya binadamu yeyote kwa ajili ya mapenzi?