Ni changamoto zipi umewahi kupitia ukiwa katika hali ya umasikini?

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,033
Kufulia wanakuita kwa kimombo "Broke", kwa kinaijeria "sapaa", kusikiage tu!

Nakumbuka niliwahi kuwa na bajeti ya 200 kwa siku, nakula mhogo wa kuchemsha imeisha hio hadi kesho, pesa ikakata nikawa nafunga safari natembea lisaa ni nje ya mji kidogo naenda kukwea miti ya mapera, nakula na huo ndo unakuwa mlo wangu wa siku nzima. (shughuli ya uwani haikuwa ndogo)

Nilikuwa napenda sana mambo ya simu na niliweza kuzichambua vizuri kwenye camera, ram, ubora, chaji, n.k, hii ilifanya watu wawe wanakuja kuniomba ushauri kununua simu ipi kwa bajeti waliyonayo ila mimi nilikuwa na kitochi kimechoka.

Nilianza kuhesabu majina kwa simu huku nikisema nani anaweza kuniazima bila kuanza kunipa darasa la maisha ama kunitangaza.

Sendo yangu ilikatika upande moja nikawa naipiga msumali ijishike, baada ya siku 3 inaachia napigilia tena, ilijaa matundu kibao.

Nilikuwa natoa nguo zote kwenye tenga na kuanza kusachi moja moja kama ina hela naambulia patupu, kesho narudia nazikunguta kwa nguvu, lakini wapi.
 
Ili kuimarika kuna mapitio mengine ni muhimu kuyapitia ili yawe ukumbusho wa kukosa pale ukipata.

Ila kiukweli kabisa hakuna faraja kwenye ufukara.

Nakumbuka kuna kipindi nilipigika ikawa natembelea washkaji mida ya misosi kiasi cha kujua ratiba ya mlo wa masela wote.

Kuna msela wangu (Mungu amlaze mahala pema) ilikuwa ikifika jioni ananipigia simu kuniita tukapige story, kumbe alishajua hali yangu na ule wito ulikuwa ni msaada indirectly maana alihakikisha nakula ndio naondoka.

Na kila nikiondoka mkewe ananipa kikontena cha msosi ananiambia shem naona chakula cha leo umekipenda beba na hiki utakula baadae.

Hawakujua jinsi gani walikuwa wakinisevu.
 
Namshukuru sana Mungu, sijawahi kupitia ufukaea wa kutisha.

Kuna vitu nimekosa ila swala la chakula, Alhamdulillah sijawahi.
Na hilo ni la kumshukuru Mungu hasa.

Haya maisha ukipata hata mlo mmoja uthamini mno maana kuna mtu anamaliza siku nzima hata kipande cha muhogo anakosa.

Asikwambie mtu, njaa inauma zaidi pale ukiwa huna hakika ya kula.

Ukiona mtu analalamika njaa na una uwezo wa kumpa hata kipande cha mkate usisite kufanya hivyo maana unaweza kuta ndio mlo pekee atakaoupata.

Waliosema adui yako muombee njaa walikuwa sahihi kabisa.
 
Heeee nyie mmetokea wapi mbona wanajf hatupo hivo
Hawa sijui wa wapi?! Hawana Ndinga Kali, hawana appartment kali na majirani wenye matacle makubwa!

Hawana Tv kubwa Nchi 55 UHD 4K ANDROID TV

Hawana kazi ya maana ya kuwaingizia kipato kizuri kwa mwezi kiasi cha kuweza kumiliki michepuko mitatu na kuendelea wakiwa wameinunulia magari, appartment nk.

Hawana hata Madanga wenye hela!

Hawa watakua sio wanajeiefu
 
Ili kuimarika kuna mapitio mengine ni muhimu kuyapitia ili yawe ukumbusho wa kukosa pale ukipata.

Ila kiukweli kabisa hakuna faraja kwenye ufukara.

Nakumbuka kuna kipindi nilipigika ikawa natembelea washkaji mida ya misosi kiasi cha kujua ratiba ya mlo wa masela wote.

Kuna msela wangu (Mungu amlaze mahala pema) ilikuwa ikifika jioni ananipigia simu kuniita tukapige story, kumbe alishajua hali yangu na ule wito ulikuwa ni msaada indirectly maana alihakikisha nakula ndio naondoka.

Na kila nikiondoka mkewe ananipa kikontena cha msosi ananiambia shem naona chakula cha leo umekipenda beba na hiki utakula baadae.
Hawakujua jinsi gani walikuwa wakinisevu.
MWENYEZI MUNGU awazidishie zaidi na zaidi ya walivyokufaa wakati wa shida zako 🙏🙏🙏
 
Nimeandika, nikafuta, nimeandika tena nikafuta…..aisee nikianza kueleza vile umasikini umenifanya server za JF zitajaa leo , ila umasikini usikie kwa watu tu nyie . Cvez Jobless mwenzangu una lolote la kuchangia hapa?
Kuna Mdau juu amesema mkewe mjamzito alikua anashindia Muwa. Nikaimajini wamama wajawazito wanavyopaswa kula mlo kamili na wasikae na njaa kisha nikaufikiria Muwa. Aiseh MAPITO NI MENGI.
 
Kipindi Nikiwa na miaka 16, niliwahi kutoroka mateso ya mama mkubwa na kutembea kuanzia Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha Hadi Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara, umbali wa kilometa zaidi ya 400 kwa muda wa siku 19 kukatisha kipande cha mbuga ya Tarangire. Kulikuwa na wanyama wengi isipokuwa simba, tembo na chui. Nilikutana na kundi kubwa la mbwa mwitu lakini Kama siku yako haijafika, haijafika tu.
 
Back
Top Bottom