Ni aibu kulazimisha kuchangisha fedha toka kwa wananchi kwa ajili ya ujenzi wa maabara

Kuchangiana harusi mnaweza tena kwa maelfu na malaki mingi sana ambayo yanachomwa moto kwa siku moja, mbili au tatu tu. Lakini kuchangia kwenye mambo ya maana ya elimu yanayodumu kwenye vichwa vya watu maisha yao yote mnaona tabu!

Amma kwa hakika Tanzania tuna kazi kubwa sana.

Kwanza kuchanga ni suala la utashi.
Pili, binadamu ana sura nyingi (human being, social being, political being, spiritual being, intellectual being, sexual being, nk) na idara zote hizo anawajibika kuzitimiliza kwa namna moja au nyingine. Anapochangia harusi ni mojawapo ya majukumu yake as a social being. Bwana harusi hajamkwapulia cho chote kwa njia ya kodi!
Anapokataa kuchangia maabara pia napo ni wajibu wake kama political being kwa sababu mchangishaji (serikali) ameisha kusanya kodi kutoka kwake na hajampatia taarifa ya mapato na matumizi ili aone kama achangie au la, au achangie wapi.
Kama Kikwete anatumia hiyo psychology ya kwamba kwa vile watu wanachangia harusi basi watachangia maabara, inabidi uprofesa wa kichina amrejeshee jing wang.
 
Kuchangiana harusi mnaweza tena kwa maelfu na malaki mingi sana ambayo yanachomwa moto kwa siku moja, mbili au tatu tu. Lakini kuchangia kwenye mambo ya maana ya elimu yanayodumu kwenye vichwa vya watu maisha yao yote mnaona tabu!

Amma kwa hakika Tanzania tuna kazi kubwa sana.
Hivi kodi mbalimbali zinazotolewa na wananchi zinafanya kazi gani? Binafsi ninaamini kazi ya kodi hizo ni kushughulikia mambo ya maendeleo kama hilo la ujenzi wa maabara. Viongozi wetu wanatakiwa kuacha wizi na ufisadi na pesa zielekezwe kwenye shughuli za maendeleo badala ya kusumbua wananchi wasio na hatia.
 
Huko vijijini wananchi wenye uwezo wa kuchangia wapo wengi tu hata mijini wapo ila ndio hivyo watanzani kwa mambo ya muhimu kama haya hawataki wanataka serikali ibebe huo mzigo lakini angalia watu wanavokunywa pombe nchi hii utasema viwanda vinataka kufungwa.
 
Kuchangiana harusi mnaweza tena kwa maelfu na malaki mingi sana ambayo yanachomwa moto kwa siku moja, mbili au tatu tu. Lakini kuchangia kwenye mambo ya maana ya elimu yanayodumu kwenye vichwa vya watu maisha yao yote mnaona tabu!

Amma kwa hakika Tanzania tuna kazi kubwa sana.

Hivi wewe kungwi hela za kujenga shule walizipata wapi?na kujenga shule ni gharama kuliko maabara ila kujenga maabara yaani jengo moja tu na vifaa vyake ndio wananchi wachangishwe?
 
Faiza ebu jaribu kuwa neutral kidogo. kuchangia maendeleo siyo jambo baya hata kidgo.
Jaribu kuelewa wakati mwingine, siyo wote wanaishi mjini wengine wanaishi vijijini, michango ya harusi huwa ni ndoto kwao.
Serekali inataka watu wachangie ujenzi wa maabara wakati serekali yenyewe imeshindwa kusimamia pesa na miradi vizuri. rejea ripoti ya CAG watu wanavyokula pesa kwenye manispaa,na majiji mabilioni, na hata wanazopereka kwenye ujenzi watu wanajenga kwa viwango duni. LEO UNATAKA WATU WACHANGIE UJENZI ILI ZIKALIWE TENA NA WENYEMENO????? HAPANA!!!!
 
Kuchangiana harusi mnaweza tena kwa maelfu na malaki mingi sana ambayo yanachomwa moto kwa siku moja, mbili au tatu tu. Lakini kuchangia kwenye mambo ya maana ya elimu yanayodumu kwenye vichwa vya watu maisha yao yote mnaona tabu!

Amma kwa hakika Tanzania tuna kazi kubwa sana.

Hapa hoja ya watu kulalamika sio kama hawapendi kuchangia kwenye mambo ya maana ila kinachoonekana ni hivi:
1. Serikali inawabana watu kuchangia wakati ina uwezo wa kujenga hizo maabara kama itakua makini na matumizi yake, kwa mfano fikiria ni miradi mingapi imepoteza mabilioni ya pesa na bado miradi hiyo ikajengwa chini ya kiwango, mara nyingi pesa hizo huishia mikononi mwa wajanja tu.
2.kwa rasilimali tulizonazo zinatuwezesha kutatua matatizo mengi ya kijamii, kwa mfano tuna migodi mingi sana ya dhahabu mikoa mbali mbali, tuna Tanzanite, tuna misitu, mbuga, vyanzo vingi vya maji, na vivutio vingi vya kitalii ambavyo mara nyingi huishia mikononi mwa vigogo na mwananchi hanufaiki.
3. Siku chache tumeshuhudia BMK ikitafuna pesa nyingi sana kwa kulipana posho nyingi kana kwamba hii nchi ni nchi iliyoendelea sana wakati hata hospitali hakuna dawa, watumishi wengi wa sekta ya elimu wanateseka! Wakati huo kuna mtu kama mhe. Komba na wengineo wanapokea laki 3 per day?? Na mwanzo mwisho wanasinzia tu, wakisikia makofi kwenye meza nao wanashtuka na kupiga makofi mezani kuunga mkono hoja wasiyo ijua.
4.Mkuu wa nchi anatafuna fedha nyingi kwa safari zingine za kisiasa tu kwa maslahi ya ccm tena mabilioni mengi tu wakati tuna shida nyingi tu.
Watawala wanahujumu mabilioni ambayo yangeboresha maendeleo ya mwananchi kwa kuboresha huduma za kijamii.
Mkuu inauma sana usiseme hatupendi maendeleo
 
Hivi huyo mwalimu unaelipishwa mchango wa maabara si analipa kodi?? hiyo pesa huwa inafanya kazi?? Jamani chonde chonde waalimu muamke usingizini mtaonewa mpaka lini?? kwanni nyie tu??

Mkuu nani kakuambia wanaotozwa ni walimu tu?

Hivi sasa ni nyumba kwa nyumba yaani mtaa kwa mtaa.

Kama hujafikiwa anza kujiandaa.
 
Hapa hoja ya watu kulalamika sio kama hawapendi kuchangia kwenye mambo ya maana ila kinachoonekana ni hivi:
1. Serikali inawabana watu kuchangia wakati ina uwezo wa kujenga hizo maabara kama itakua makini na matumizi yake, kwa mfano fikiria ni miradi mingapi imepoteza mabilioni ya pesa na bado miradi hiyo ikajengwa chini ya kiwango, mara nyingi pesa hizo huishia mikononi mwa wajanja tu.
2.kwa rasilimali tulizonazo zinatuwezesha kutatua matatizo mengi ya kijamii, kwa mfano tuna migodi mingi sana ya dhahabu mikoa mbali mbali, tuna Tanzanite, tuna misitu, mbuga, vyanzo vingi vya maji, na vivutio vingi vya kitalii ambavyo mara nyingi huishia mikononi mwa vigogo na mwananchi hanufaiki.
3. Siku chache tumeshuhudia BMK ikitafuna pesa nyingi sana kwa kulipana posho nyingi kana kwamba hii nchi ni nchi iliyoendelea sana wakati hata hospitali hakuna dawa, watumishi wengi wa sekta ya elimu wanateseka! Wakati huo kuna mtu kama mhe. Komba na wengineo wanapokea laki 3 per day?? Na mwanzo mwisho wanasinzia tu, wakisikia makofi kwenye meza nao wanashtuka na kupiga makofi mezani kuunga mkono hoja wasiyo ijua.
4.Mkuu wa nchi anatafuna fedha nyingi kwa safari zingine za kisiasa tu kwa maslahi ya ccm tena mabilioni mengi tu wakati tuna shida nyingi tu.
Watawala wanahujumu mabilioni ambayo yangeboresha maendeleo ya mwananchi kwa kuboresha huduma za kijamii.
Mkuu inauma sana usiseme hatupendi maendeleo

mkuu usimuulize maswali huyo bibi hawezi kujibu maswali
 
Kuchangiana harusi mnaweza tena kwa maelfu na malaki mingi sana ambayo yanachomwa moto kwa siku moja, mbili au tatu tu. Lakini kuchangia kwenye mambo ya maana ya elimu yanayodumu kwenye vichwa vya watu maisha yao yote mnaona tabu!

Amma kwa hakika Tanzania tuna kazi kubwa sana.
Wewe umeshachangia shilingi ngapi kujenga maabara FaizaFoxy?
 
Wacha porojo, kama unalipa hiyo kodi yote ni lazima utakuwa unakatwa NSSF na ukikatwa hiyo tu Hospitali bure. Au hujuwi hilo?

Ulipe kodi seven figures kila mwezi halafu ulalamike?

Hivi mtaacha lini kulalamika? hamjui kuwa mpaka leo fedhaa yenu yote ya kodi haitoshi kuendesha Serikali? huwa hamsikilizi bajeti ya kila mwaka? Kikwete ndio kajitahidi kuitoa katika tegemezi ya zaidi ya 60% kaishusha mpaka 30% au hilo nalo ni shida kulijuwa?

Kama unaweza kuchangia hiyo 10,000 unachangia kama huwezi unamtoa mtoto shule, kwani maabara ina faida gani kwa mwanao?

Nyie ndio wale mkiambiwa mchango wa graduation elfu hamsini amsini mwanao akakate viuno mnachangia mbio mbio, lakini ikija kwenye vitu vya maana lazima mnung'unike.

Tunawajuwa, kukaa baa na kulewa pesa zipo, kuchangia maabara kwa faida ya mwanao na wengine hauna pesa!
Nani kakudanganya kuwa ukikatwa NSSF basi unapata matibabu bure???? Are you serious au unataka ku-mislead watu wengine?
 
Kakodi kako hata hakakidhi mahitaji ya bajeti au huwa husomi bajeti ya nchi?

Halafu kumbuka, kodi inalipwa na wachache sana Tanzania, jisomee.
Dada FaizaFoxy, unaweza kueleza sababu ni kwa nini kwenye nchi ambayo ina watu zaidi ya million 15 ambao wanatakiwa kulipa kodi, lakini ni "wachache sana wanaolipa?" Na hao wachache unaosema ni wangapi kwa kiwango chako?
 
mkuu usimuulize maswali huyo bibi hawezi kujibu maswali
Amebakia kusema tu "kama hutaki mtoe mwanao shule" Upuuzi mtupu. Anashikilia kusema michango ya arusi utadhani inachangwa na wananchi wote!!!!
 
kwendeni huko mnaokumbuka shuka kumekucha!mnakandamizA wananchi kwa sababu ya uchaguzi mpate ya kujitetea.mlikua wapi kujenga maabara mnakuja kutoa vioder vya kishenzi eti mwisho mwz wa 11.km niko chuo naombwa na wazaz mchango niwasaidie wakati hata boom cjapata.elfu 40 mzaz wangu aipate wapi?shame on u!
 
Niwashukuru wote mliochangia mada hii hadi sasa.... Zaidi ya upotoshaji unaofanywa na FaizaFoxy; hatujapata sababu ya kujitosheleza ya kwa nini michango hiyo inalazimishwa tena kwa nini iwe vijijini ambako kiasili ufuatiliaji/uelewa wa watu ni mdogo?!

Tumieni maswali haya kutafuta ukweli.... ukweli utawaweka huru!!
1. Wewe ni msafiri (aina yoyote ile ya usafiri); je, upo tayari kuchangishwa fedha zaidi ya nauli kwa ajili ya mafunzo wafanyakazi wa chombo husika au hata matengenezo ya engine?
2. Wewe ni mwanafunzi (ngazi yoyote ile ya elimu); je, upo tayari kuchangishwa fedha zaidi kwa ajili ya kusomesha walimu wanaonekana kupwaya?
3. Wewe ni askari; je upo tayari kulipishwa michango kwa ajili ya magwanda au huduma nyingine ambazo ni stahiki yako?
4. Wewe ni mgonjwa; je upo tayari kulipishwa fedha zaidi ya kawaida kwa kisingizio cha kuboresha mafunzo ya waaguzi wasiojali wagonjwa?
5. Wewe ni mchangiaji mzuri sana wa harusi, kitchen, n.k; je, upo tayari kulazimishiwa mchango zaidi ya uwezo wako huku ukijua wazi kuwa pale hamna cha harusi wala sherehe bali watu wanaenda kufanya yao?
6. Wewe ziko nyingi sana hapa.... lakini nambieni mpo tayari kulazimishwa kuchangia shughuli ambazo kwa namna moja au nyingine tulishazichangia; ni haki yetu ila wajanja wachache ndo wananufaika?
7. Hivi mnapoenda kutembeza mabakuli huko Ughaibuni uwa mnawalazimisha badala ya kujenga ushawishi? Hivi hamuwaambii mna nini tayari na mnakwama wapi?

Kama nina nia na uwezo wa kuchangia nitafanya hivyo kupitia NGOs na si viongozi wa serikali! Zipo NGOs makini sana; hawapokei kodi yangu lakini watatumia michango kusimamia miradi kwa ufanisi wa hali ya juu!! Viongozi wa serekali ni wapuuzi sana; hawachelewi kutumia michango kubadilishia maumbo yao!

Sipo na sitakuwa tayari kuichangia serekali zaidi ya kodi na tozo halali kisheria! Hizi za kukurupuka wachangie wale wale waliokunywa damu za bendera ya chama!!
 
kwendeni huko mnaokumbuka shuka kumekucha!mnakandamizA wananchi kwa sababu ya uchaguzi mpate ya kujitetea.mlikua wapi kujenga maabara mnakuja kutoa vioder vya kishenzi eti mwisho mwz wa 11.km niko chuo naombwa na wazaz mchango niwasaidie wakati hata boom cjapata.elfu 40 mzaz wangu aipate wapi?shame on u!

Pole sana Mkuu! I know the pain you are going through; most of us are or have been in a similar situation! Hold on just a little bit longer till we make noises to wake everybody up!!

FaizaFoxy et al; mnasikia haya?? Msijifanye mnapenda saña maabara ziwepo ndani mwaka mmoja wa mwisho ilhali miaka yote mlikuwepo!!!
Mkiambiwa watu wengi mnaumia mnakurupusha majibu kama vile mpo labour!!
 
Back
Top Bottom