nyundo2017
JF-Expert Member
- Sep 7, 2017
- 1,439
- 859
Habarini,
NHIF wekeni uwiano wa matibabu kwa watumishi na watu binafsi wote wachangie sawa na wapate huduma sawa.
NHIF mnapotoa vifurushi vya TUNAJALI,TIMIZA,n.k na kuondoa malipo ya vipino kama vile OGD na kadharika wananchi tunashindwa kuwaelewa kabisa.
Mtu analipia kifurushi cha TIMIZA anasafiri kuja kwenye matibabu MNH Dar Es Salaam anafika anaambiwa apime vipimo ikiwemo OGD halafu anaambiwa alipie kwani haviko kwenye vifurushi vya binafsi sasa kipimo cha OGD tu ni Tshs. 260,000/= ukiacha vinginevyo ambavyo haviko kwenye kifurushi cha TIMIZA.
Kifurushi cha TIMIZA ni Tshs. 1,188,000/= kwa mwaka na mtumishi wa chini analipa Tshs.18,000/= kwa mwezi ukizidisha kwa mwaka/miezi 12 ni Tshs. 216,000/= kwa mwaka.
Sasa mtumishi wa serikali analipia Tshs. 216,000/= kwa mwaka na anapata vipimo vyote na wategemezi 6 iweje mtu binafsi anayelipia Tshs. 1,188,000/= kwa mme na mke tu kwa mwaka asipate vipimo vyote?
Huu ni unyonyaji kwani ni wazi watu binafsi wanaumizwa zaidi na kuwa wabebaji wa gharama za watumishi wa serikali.
Ni wazo langu kuwa kuwe na kifurushi sawa kwa watumishi wa umma na watu binafsi kwa kuchangia gharama sawa na kupata huduma sawa,kama ni kulipia hiyo 1,188,000/= kwa mwaka basi wote walipie kiasi hicho eidha kwa awamu au kwa mkupuo.
Nawasilisha
NHIF wekeni uwiano wa matibabu kwa watumishi na watu binafsi wote wachangie sawa na wapate huduma sawa.
NHIF mnapotoa vifurushi vya TUNAJALI,TIMIZA,n.k na kuondoa malipo ya vipino kama vile OGD na kadharika wananchi tunashindwa kuwaelewa kabisa.
Mtu analipia kifurushi cha TIMIZA anasafiri kuja kwenye matibabu MNH Dar Es Salaam anafika anaambiwa apime vipimo ikiwemo OGD halafu anaambiwa alipie kwani haviko kwenye vifurushi vya binafsi sasa kipimo cha OGD tu ni Tshs. 260,000/= ukiacha vinginevyo ambavyo haviko kwenye kifurushi cha TIMIZA.
Kifurushi cha TIMIZA ni Tshs. 1,188,000/= kwa mwaka na mtumishi wa chini analipa Tshs.18,000/= kwa mwezi ukizidisha kwa mwaka/miezi 12 ni Tshs. 216,000/= kwa mwaka.
Sasa mtumishi wa serikali analipia Tshs. 216,000/= kwa mwaka na anapata vipimo vyote na wategemezi 6 iweje mtu binafsi anayelipia Tshs. 1,188,000/= kwa mme na mke tu kwa mwaka asipate vipimo vyote?
Huu ni unyonyaji kwani ni wazi watu binafsi wanaumizwa zaidi na kuwa wabebaji wa gharama za watumishi wa serikali.
Ni wazo langu kuwa kuwe na kifurushi sawa kwa watumishi wa umma na watu binafsi kwa kuchangia gharama sawa na kupata huduma sawa,kama ni kulipia hiyo 1,188,000/= kwa mwaka basi wote walipie kiasi hicho eidha kwa awamu au kwa mkupuo.
Nawasilisha