NHIF mnaumiza wanachama wenu

NHIF mnaumiza wanachama wenu

Status
Not open for further replies.
Hivi unatumia bima ya NHIF kweli wewe? Umewahi kuugua ugonjwa unaokuhitaji kuchukua dawa kila mwezi hivi karibuni mkuu?
Huyo ni mfanyakazi wa NHIF, wanaona ni sifa kukaa ofisini na kuendesha madaktari kwa rimoti. Wengi wamesoma kozi za afya lakini hawajawahi ku practice. Ni theory tu anayozungumza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuondoa huu usumbufu na hizi kero ni bora serikali ikaondoa ukiritimba wa Nhif ikawaruhusu wafanyakazi wake kujiunga katika mfuko wanaoutaka wao
Hili ndilo suluhisho la kudumu. Mtu akiajiriwa tu kabla hajapata hata kadi ya Bima wao tayari wanakata Chao.
Ilitakiwa iwe hiari hapo mashirika/mifuko binafsi itaimarika na kuweka ushindani kuliko hali iliyopo sasa. NHIF na kila siku Wanaweka masharti ili watu wasiweze kuweka wanufaika katika Bima zao na wanatoa baadhi ya huduma kwa mnufaika wa Bima.
 
Juzi katika kufuatilia niliona Bima ya Afya wakizingumzia dawa zilizoongezwa katika kitita na
Mimi kama mtanzania wa hali ya chini naomba nitumie fursa ya kuwasilisha machache kuhusu NHIF -mfuko wa bima. Ni jambo la kushangaza na kusikitisha NHIF kuondoa baadhi ya dawa katika orodha yenu ya madawa kwa wanachama huku mkijua gharama ya dawa ni kubwa mno mtaani lakini ajabu zaidi michango ya wanachama iko pale pale.

Mfano mmoja wa hizo dawa ni injection iron sulphate, ambayo bei ya mtaani ni Tshs 9,000 mpaka 15,000. Hii inaumiza mno. Tu naomba liangaliwe.
Nilifuatilia juzi kwenye kipindi Bima ya Afya wameiongeza hii dawa kwenye orodha ya dawa 71 zilizoongezwa.
 
Hili ndilo suluhisho la kudumu. Mtu akiajiriwa tu kabla hajapata hata kadi ya Bima wao tayari wanakata Chao.
Ilitakiwa iwe hiari hapo mashirika/mifuko binafsi itaimarika na kuweka ushindani kuliko hali iliyopo sasa. NHIF na kila siku Wanaweka masharti ili watu wasiweze kuweka wanufaika katika Bima zao na wanatoa baadhi ya huduma kwa mnufaika wa Bima.
Wakugoogle unayasema hayo labda kwa sababu hujawahi kupata shida kubwa ya matibabu katika familia yako.

Nataka nikuhakikishie kwamba katika utaratibu wa Bima ya Afya ndani ya AFRICA.......NHIF-TANZANIA inaweza kuwa the best compared na mifumo ya Bima iliyopo Nchi nyingine zote.

Mtumishi wa umma ambaye ni mwanachama wa NHIF ana uhakika wa kupata urahisi wa matibabu kama ifuatavyo:-
1. kwanza anatibiwa yeye mwenza wake na wategemezi 4.
2. Mtumishi anaruhusiwa kuwabeba wazazi na wakwe kama wategemezi .....hili hakuna kwa insurance yoyote hapa nchini
3. Mwanachama anapata huduma kwenye vituo zaidi ya 8,000 vilivyosajiliwa nchi nzima yeye na wategemezi wake
4. pamoja na huduma za kawaida .....mwanachama atapata huduma za matibabu ya cancer, dialysis, pamoja na huduma za magonjwa yasiyo ambukiza kama vile kisukari, pressure n.k na hii wanapewa dawa kila mwezi kwa kutumia NHIF.

Mambo mengi hapo huwezi kuyapata kwenye Bima binafsi kwa sababu wao wanajiendesha kibiashara.....They are doing FUND MANAGEMENT yaani unawapa fedha yako wakushikie ukipata shida ya Afya wanakulipia then zikiisha unaambiwa ongeza nyingine BUT

NHIF ni social health insurance ambayo unachangia kulingana na uwezo wako.... na unapata huduma za matibabu kulingana na janga lililokupata bila kujali ulichangia nini. .....Ndani ya NHIF UNATUMIA kulingana na kilichoandikwa na daktari.

HIVYO NI MUHIMU WATANZANIA tukawa tunapenda vitu vyetu......nikimaanisha kwamba kama kuna shida tutoe maoni yashughulikiwe lakini tusilalamike kana kwamba hakuna linalofanyika. Watanzania wengi waliopata matatizo wanajua umuhimu wa NHIF.
 
Juzi katika kufuatilia niliona Bima ya Afya wakizingumzia dawa zilizoongezwa katika kitita na

Nilifuatilia juzi kwenye kipindi Bima ya Afya wameiongeza hii dawa kwenye orodha ya dawa 71 zilizoongezwa.
Wangesema na walizozitoa, vifaa tiba vyote "removed". Hadi crepe bandage ukiteguka ununue.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jana nimekua nafanya research mimi na familia tujiunge NHIF kile kifurushi cha bei ya juu kabisa. Inatakiwa km milioni moja na laki hivi. Nikacheki AAR kifurushi cha dizaini hiyo ila cha chini kidoogo ni mara mbili yake.
Sasa kuokoa cost nika make conclusion ngoja nikate NHIF ila mimi nimezoea sana kwenda Agakhan hospital. Sasa nikasema ngoja niwapigie Agakhan kuwauliza vp mnapokea wenye bima za NHIF.
Nikajutaa. Eti wenye bima za NHIF wanaopokewa hapa Agakhan ni wafanyakaz wa TRA, Benki Kuu sijui na kampuni gani nimesahau jina. Wengine wote hatupokei labda uende kwenye vile vijibranch vya Agakhan.
Nilichoka kwa kweli.
Uzalendo utanishinda itabidi nijichange nikate tu AAR sasa.
Tena na watu hapa wanakatisha tamaa sijui dawa gani hupewi duh!
fanya research ya jubilee mkuu na britam pia..
 
fanya research ya jubilee mkuu na britam pia..
Ooh sawa sawa ntafanya hivyo aisee. Kwa kuanzia tu ntashukuru sana chochote unachokijua kuhusu hawa jamaa jubilee na britam kabla sijaanza research
 
MGURUGENZI WA NHIF MULIKA WATUMISHI WA NHIF HOSPITALI YA WILAYA YA NZEGA.

- Kwanza muda mwingi hawapo kazini.Mfano, JUMAMOSI,JUMAPILI,na nyakati zs USIKU!!! Je WAGONJWA WA BINA NYAKATI HIZO HUWA HAWAUMWI?? NDIVYO MLIVYOAGANA NAO KWAMBA NYAKATI HIZO WAGONJWA WANAOTUMIA BIMA HAWAPASWI KUUMWA NA IKITOKEA WAMEUMWA NYAKATI HIZO WANAPASWA WAJIGHARAMIE MATIBABU ILIHALI WANABI A KISA MJAZAJI WA FORMU HAYUPO KAZINI?????????


-Kadi la Mgonjwa Lile gumu ,Unaambiwa kanunue dafutari dogo hapo getini kwao!!! Huo huenda ni mradi wa mtu.!!

- Dawa nyingi Unaambiwa hazipo kanunueNi wajibu wenu kuhakikisha Dawa zote zipo kwa wagonjwa wa Bima.Vinginevyo mtupage na hela za kununulia HIZO Dawa maduka ya Phamarcy.

MKURUGENZI HAKIKISHA WATUMISHI WAPO MUDA WOTE HASA NYAKATI ZA USIKU NA WIKENDI.HILI NI KEROOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO
Mkurugenzi hana pesa ya kumlipa MD aingie weekend na usiku, unamuonea bure tu mkuu
 
Lingine unapokata bima kuna magonjwa yanatakiwa usiugue ndani ya mwaka mzima wa wanachama wako ukiugua bima hailipi hizo gharama!
 
Mimi kama mtanzania wa hali ya chini naomba nitumie fursa ya kuwasilisha machache kuhusu NHIF -mfuko wa bima. Ni jambo la kushangaza na kusikitisha NHIF kuondoa baadhi ya dawa katika orodha yenu ya madawa kwa wanachama huku mkijua gharama ya dawa ni kubwa mno mtaani lakini ajabu zaidi michango ya wanachama iko pale pale.

Mfano mmoja wa hizo dawa ni injection iron sulphate, ambayo bei ya mtaani ni Tshs 9,000 mpaka 15,000. Hii inaumiza mno. Tu naomba liangaliwe.
Hii Ni kweli kabisa karibu Kila mwezi Kuna Dawa zinatolewa kwenye bima. Inasikitisha kuona wanachama Wanavyoongezeka Huduma zinadorora. Wahusika watoe maelezo humu humu. Uwazi unatakiwa kwenye suala hili!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom