NHIF mnaumiza wanachama wenu

NHIF mnaumiza wanachama wenu

Status
Not open for further replies.

uncle

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2007
Posts
325
Reaction score
184
Mimi kama mtanzania wa hali ya chini naomba nitumie fursa ya kuwasilisha machache kuhusu NHIF -mfuko wa bima. Ni jambo la kushangaza na kusikitisha NHIF kuondoa baadhi ya dawa katika orodha yenu ya madawa kwa wanachama huku mkijua gharama ya dawa ni kubwa mno mtaani lakini ajabu zaidi michango ya wanachama iko pale pale.

Mfano mmoja wa hizo dawa ni injection iron sulphate, ambayo bei ya mtaani ni Tshs 9,000 mpaka 15,000. Hii inaumiza mno. Tu naomba liangaliwe.
 
Hili linaumiza sana. Madawa ni ghali mno. Nhif msikae kimya kwani hela inayochangiwa ni nyingi wanachama wenu hatustahili haya magumu
 
Nhif Ni wezi walio thibitishwa kisheria...

Huo ndio ukweli kuwa NHIF ni wezi wa mchana kwani mtu kama mie nimechangia kwa zaidi ya miaka 35 na nilikuwa siugui kijingajinga leo nimekuwa mzee na kustaafu napatwa na magonjwa yanayoendana na uzee eg Hypertension naandikiwa dawa na specialist ambayo anaona inanifaa lakini ajabu NHIF wametoa waraka kisirisiri kuwa tusipewe hizo dawa na badala yake tupewe dawa za hali yachini zenye low Quality sijui lengo lao tufe mapema? ukirudi kwa Dr anakwambia kuwa bora ununue dawa ambayo amekuandikia kuliko kukupatia dawa zilizopendekezwa na NHIF ....sasa nini hasa maana ya Bima kama hawawezi kufuata maagizo ya Drs wetu? kilichobaki NHIF ni kuibia wateja mchana kweupe
 
Mimi kama mtanzania wa hali ya chini naomba nitumie fursa ya kuwasilisha machache kuhusu NHIF -mfuko wa bima ,chakushangaza na kusikitisha nhif umeondoa baadhi ya dawa katika orodha yenu ya madawa kwa wanachama huku mkijua gharama ya dawa ni kubwa mno mtaani lakini ajabu zaidi michango ya wanachama iko pale pale. Mfano mmoja wa hizo dawa ni injection iron sulphate, ambayo bei ya mtaani ni Tshs 9000 mpk 15000. Hii inaumiza mno. Tu naomba liangaliwe
Wanaboa kwa kweli. Wanajua magonjwa yanayowaandama wastaafu wengi, wamezuia fawa muhimu nyingi. Mfano dawa Za kisukari nyingi, Za hypertensjon nk unaenda dukani wanakwambia dose ya mwezi ni 170,000na hiyo ni moja. Daktari anasema wafanyakazi wadi TRA. Benki wanaruhisiwa bilar shida. Ubaguzi gani huo. Au ninyi hamtazeeka na kustaafu?
 
Wanaboa kwa kweli. Wanajua magonjwa yanayowaandama wastaafu wengi, wamezuia fawa muhimu nyingi. Mfano dawa Za kisukari nyingi, Za hypertensjon nk unaenda dukani wanakwambia dose ya mwezi ni 170,000na hiyo ni moja. Daktari anasema wafanyakazi wadi TRA. Benki wanaruhisiwa bilar shida. Ubaguzi gani huo. Au ninyi hamtazeeka na kustaafu?
Hapo uliposema wafanyakazi wa TRA,Benki wanaruhusiwa sijakuelewa ,naomba ufafanue
 
Wanaboa kwa kweli. Wanajua magonjwa yanayowaandama wastaafu wengi, wamezuia fawa muhimu nyingi. Mfano dawa Za kisukari nyingi, Za hypertensjon nk unaenda dukani wanakwambia dose ya mwezi ni 170,000na hiyo ni moja. Daktari anasema wafanyakazi wadi TRA. Benki wanaruhisiwa bilar shida. Ubaguzi gani huo. Au ninyi hamtazeeka na kustaafu?
Uchumi wa Kati
 
Hapo uliposema wafanyakazi wa TRA,Benki wanaruhusiwa sijakuelewa ,naomba ufafanue

Nahisi anamaamisha namba zao za kadi ya nhif zimepewa upendeleo na nhif sabab wana mishahara mikubwa hivyo wanachangia hela nyingi kila mwezi wanazokatwa kwenda nhif

Wao wakiandikiwa dawa na daktari mtu wa phamarcy akiziingiza kwenye stystem ya nhif zinapitishwa apewe.. wafanyakazi wenye mishahara midogo zinagoma kupita hizo dawa
 
Nahisi anamaamisha namba zao za kadi ya nhif zimepewa upendeleo na nhif sabab wana mishahara mikubwa hivyo wanachangia hela nyingi kila mwezi wanazokatwa kwenda nhif

Wao wakiandikiwa dawa na daktari mtu wa phamarcy akiziingiza kwenye stystem ya nhif zinapitishwa apewe.. wafanyakazi wenye mishahara midogo zinagoma kupita hizo dawa


Mmh kama ndio hivyo basi huo uchawi sasa yani unanyimwa kisa unachangia kidogo🙄
 
Hapo uliposema wafanyakazi wa TRA,Benki wanaruhusiwa sijakuelewa ,naomba ufafanue
Jana nimekua nafanya research mimi na familia tujiunge NHIF kile kifurushi cha bei ya juu kabisa. Inatakiwa km milioni moja na laki hivi. Nikacheki AAR kifurushi cha dizaini hiyo ila cha chini kidoogo ni mara mbili yake.
Sasa kuokoa cost nika make conclusion ngoja nikate NHIF ila mimi nimezoea sana kwenda Agakhan hospital. Sasa nikasema ngoja niwapigie Agakhan kuwauliza vp mnapokea wenye bima za NHIF.
Nikajutaa. Eti wenye bima za NHIF wanaopokewa hapa Agakhan ni wafanyakaz wa TRA, Benki Kuu sijui na kampuni gani nimesahau jina. Wengine wote hatupokei labda uende kwenye vile vijibranch vya Agakhan.
Nilichoka kwa kweli.
Uzalendo utanishinda itabidi nijichange nikate tu AAR sasa.
Tena na watu hapa wanakatisha tamaa sijui dawa gani hupewi duh!
 
Jana nimekua nafanya research mimi na familia tujiunge NHIF kile kifurushi cha bei ya juu kabisa. Inatakiwa km milioni moja na laki hivi. Nikacheki AAR kifurushi cha dizaini hiyo ila cha chini kidoogo ni mara mbili yake.
Sasa kuokoa cost nika make conclusion ngoja nikate NHIF ila mimi nimezoea sana kwenda Agakhan hospital. Sasa nikasema ngoja niwapigie Agakhan kuwauliza vp mnapokea wenye bima za NHIF.
Nikajutaa. Eti wenye bima za NHIF wanaopokewa hapa Agakhan ni wafanyakaz wa TRA, Benki Kuu sijui na kampuni gani nimesahau jina. Wengine wote hatupokei labda uende kwenye vile vijibranch vya Agakhan.
Nilichoka kwa kweli.
Uzalendo utanishinda itabidi nijichange nikate tu AAR sasa.
Tena na watu hapa wanakatisha tamaa sijui dawa gani hupewi duh!
Mkuu hao AAR walikwambia bei gani kifurushi chao?na je hicho kifurushi kinacover familia nzima au ni kwa mtu mmoja tu?
Na je ulijaribu kwenda kuulizia kwenye kampuni zingine za bima kama Jubilee,Metropolitan na zingine mfano wa hizo?
 
Mkuu hao AAR walikwambia bei gani kifurushi chao?na je hicho kifurushi kinacover familia nzima au ni kwa mtu mmoja tu?
Na je ulijaribu kwenda kuulizia kwenye kampuni zingine za bima kama Jubilee,Metropolitan na zingine mfano wa hizo?
Mkuu kifurushi kinategemea mko wangapi kwenye familia.
Lakini kama mko watatu gharama yake inacheza kuanzia milioni 2.4 kwa class ya chini .......milioni 2.6 kwa class ya katikati .........na milioni 2.9 kwa class ya juu.
Maana kuna sijui bronze, silver na sijui nini.
Tofauti ya hizo bei ni kwamba unataka kwa mfano kwenye sector flani mfano meno coverage iwe kubwa, ya kati au ya chini na vitu vingine vingine
Lakini hicho cha 2.4 sio mbaya kwa maoni yangu.

Kuhusu hao wengine kwa kweli wala sikuhangaika kuwacheki. Tangu napata fahamu zangu nimekua na AAR nimeingiwa taamaa ya NHIF kwa kua mwaka jana waliboresha huduma na mambo nikahisi yatakua ya mamtoni kumbe utopolo juu ya utopolo.
Hao wengine kwa kweli itanibidi niwacheki nikipata mda. Uzuri wa AAR unaingia popote pale. I'm sure Jubilee lazima kina hospital hawataikubali sijui lkn.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom