NHC kuuza nyumba Arusha / Dar es salaam

Jethro

JF-Expert Member
Mar 23, 2009
2,219
370
Wana JF,

Nimechukuwa muda huu kupenda kujua vyema kuhusu NHC Shirika la nyumba Taifa pale lilipo tangaza kuwa lina uza nyumba zake katika mikoa ya Arusha na Dar -Es-Salaam.

Kweli katika tangazo lao la wananchi kuandika barua ili kuomba kununua nyumba hapo sawa ila wao NHC hawajatuambia nyumba hizo zinazo uzwa Dar ziko eneo gani au huko Arusha hizo nyumba ziko eneo lipi ni mpya au za zamani?.

Mashaka yangu makubwa ni kuwa tangazo hilo limetangazwa ni kukidhi majukumu ya kazi kuwa walitangaza nyuma zinauzwa au?

Tetesi zimeanza kutokeza kuwa nyumba husika zinazo tangazwa kuuzwa tayari kuna vigogo walisha jinyakulia nyumba ili wao waje kuzipangisha kwa raia wengine

Ni mashaka yangu makubwa kuwa NHC watakuwa hawajatenda haki kwa raia (wakazi wa maeneo husika esp wa kipato cha chini kabisa) kwani siku zote mashirika yetu ya umma yauzapo vitu huwapa vigogo issue then utasikia wametangaza ukifuatiria its toooo late kumbe walisha gawana zamani huko.

Karibuni kwenye Hoja tujadili
 
Wana JF,

Nimechukuwa muda huu kupenda kujua vyema kuhusu NHC Shirika la nyumba Taifa pale lilipo tangaza kuwa lina uza nyumba zake katika mikoa ya Arusha na Dar -Es-Salaam.

Kweli katika tangazo lao la wananchi kuandika barua ili kuomba kununua nyumba hapo sawa ila wao NHC hawajatuambia nyumba hizo zinazo uzwa Dar ziko eneo gani au huko Arusha hizo nyumba ziko eneo lipi ni mpya au za zamani?.

Mashaka yangu makubwa ni kuwa tangazo hilo limetangazwa ni kukidhi majukumu ya kazi kuwa walitangaza nyuma zinauzwa au?

Tetesi zimeanza kutokeza kuwa nyumba husika zinazo tangazwa kuuzwa tayari kuna vigogo walisha jinyakulia nyumba ili wao waje kuzipangisha kwa raia wengine

Ni mashaka yangu makubwa kuwa NHC watakuwa hawajatenda haki kwa raia (wakazi wa maeneo husika esp wa kipato cha chini kabisa) kwani siku zote mashirika yetu ya umma yauzapo vitu huwapa vigogo issue then utasikia wametangaza ukifuatiria its toooo late kumbe walisha gawana zamani huko.

Karibuni kwenye Hoja tujadili

Ndiyo Bongo hiyo Mkuu jamaa wanataka kujilimbikizia kila kitu wao kama vile Watanzania wengine hawana haki ya kuzinunua nyumba hizo.
 
Ndiyo Bongo hiyo Mkuu jamaa wanataka kujilimbikizia kila kitu wao kama vile Watanzania wengine hawana haki ya kuzinunua nyumba hizo.

Kuna mtu alinijuza huko arusha kuna baadhi ya matajiri tayari walisha pewa nyumba wanasubili tu vibali ili wazimiliki
 
Shirika la nyumba la Taifa ( NHC ) linahitajika kuuza nyumba mpya ambazo imezijenga na kuzirudisha kwa
kwa wenyewe nyumba zote zilizotaifishwa wakati wa azimio la Arusha lilipotangazwa mwaka 1966.
Na kwa ujumla Shirika zima livunjwe, Kwa mfumo tulionao sasa serikali aina dhamana ya kuendesha biashara
ya aina yeyote ile zaidi ya kuwaongoza wananchi kupanga na kutoa maamuzi ya maendeleo kwa nchi.
Lakini inashangaza ni kwa nini serikali ya Ccm inang'ang'ania kuwa wakala wa ( Reale Estate )
Zaidi ya hapo ni ufisadi ambao unaouzidi kuwatia mashaka Watanzania.
 
Shirika la nyumba la Taifa ( NHC ) linahitajika kuuza nyumba mpya ambazo imezijenga na kuzirudisha kwa
kwa wenyewe nyumba zote zilizotaifishwa wakati wa azimio la Arusha lilipotangazwa mwaka 1966.
Na kwa ujumla Shirika zima livunjwe, Kwa mfumo tulionao sasa serikali aina dhamana ya kuendesha biashara
ya aina yeyote ile zaidi ya kuwaongoza wananchi kupanga na kutoa maamuzi ya maendeleo kwa nchi
.
Lakini inashangaza ni kwa nini serikali ya Ccm inang'ang'ania kuwa wakala wa ( Reale Estate )
Zaidi ya hapo ni ufisadi ambao unaouzidi kuwatia mashaka Watanzania.

Hapo ndipo watu wanashindwa kuelewa serikali yao inashindwa kuhudumia wananchi wake na badala yake imejikita kufanya biashara na kupotea mantiki nzima ya utumishi.

Mwl. Nyerere Alisema 1995 Mei Mosi - Mbeya "Umaskini wa kufikili ndio umasikini mbaya kuliko umasikini wowote ule dunia" Hicho ndicho chanzo cha matatizo ya viongozi wetu hapa nchini kutokufikili na kujenga hoja na wanatupa majibu mepesi mepesi tuu bora siku ziende
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nyumba zinauzwa milioni 175 na hiyo ni solid cash, je wananchi masikini watawezaje kupata? NHC ni kwa ajili ya wenye nazo hamna sehemu ambayo wanasema watakopesha hizi nyumba kwa wananchi ambao the majority ni masikini, it's just a notion expressed to the mass that NHC housing project is for all tanzanians bila kubagua tajiri ama maskini. In actual sense maskini mil 175 atapatia wapi hiyo ni mshahara wa zaidi ya miaka kumi. NHC msitudanganye
 
Sasa tuone watakaonunua nyumba hizo, maana humu jamvini munasema Wahindi ndio wenye kumiliki NHC. Na tungoje, tuangalie huyu mfanyakazi anaeonewa huruma , atazitoa wapi hizo 175m+18% vat, watanunua wafanyakazi wa TRA, tISCAN, Na makamanda katika vita dhidi ya Ufisadi.
Nyumba zinauzwa milioni 175 na hiyo ni solid cash, je wananchi masikini watawezaje kupata? NHC ni kwa ajili ya wenye nazo hamna sehemu ambayo wanasema watakopesha hizi nyumba kwa wananchi ambao the majority ni masikini, it's just a notion expressed to the mass that NHC housing project is for all tanzanians bila kubagua tajiri ama maskini. In actual sense maskini mil 175 atapatia wapi hiyo ni mshahara wa zaidi ya miaka kumi. NHC msitudanganye
 
Nyumba zinauzwa milioni 175 na hiyo ni solid cash, je wananchi masikini watawezaje kupata? NHC ni kwa ajili ya wenye nazo hamna sehemu ambayo wanasema watakopesha hizi nyumba kwa wananchi ambao the majority ni masikini, it's just a notion expressed to the mass that NHC housing project is for all tanzanians bila kubagua tajiri ama maskini. In actual sense maskini mil 175 atapatia wapi hiyo ni mshahara wa zaidi ya miaka kumi. NHC msitudanganye

NHC ni wezii, tena ni mafisadi wa kubwa, wanauza nyumba milioni 114 pale Dodoma nyuma ya CBE na hizi nyingine arusha milion 175 tena wanataka cash, hivi ni mlalahoi gani atanunua hizo nyumba? hata kama ni mkuu wa wilaya na kimshahara chake cha milion 4 hawezi pata hii cash unless ni mwizi. hapa kuna janja ya nyani yaani naskia hasira sana. kwanin wasiweke mpango wa kuwajengea walim na wafanyakazi wa serikali na kisha kuwakopesha ili kila mmoja apate yake?

Ivi kama hili toto la JK likiamua kuja kununua nyumba zote anashindwa nn wakati anamiliki bilions of money? hapa wanyonge wanazidi
kunyongwa na haki zao hawapewi, ipo siku tutajificha porini afu wakipita barabarani tuwatungue na magobore yetu ya asili, inauma sana! anyway Tusizidi kuimbea Tanzania hakika Mungu si athuman anaweza kufanya miujiza wanyonge wakawaongoza wenye nayo.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nakumbuka kwenye nyumba za Serikali ambazo Mkapa aliamua wauaziane kwa bei ya kutupa baadhi ya Watanzania walitaka kuwe kufanyike mnada ili nyumba zile ziuzwe kwa faida kubwa kwa Serikali, lakini Mkapa na Baraza lake la Mawaziri wakakataa hili kwa kujua kwa kupitia mnada bei ya nyumba zile zingepaa sana na hivyo wengi wao kushindwa kuzinunua. Kama hizi nyumba za NHC zikifanyiwa tathmini sidhani nyingi ya nyumba hizo kutokana na uchakavu zitafika bei hiyo wanayoitaka NHC.

Kihalali Wafanyakazi wa umma watakaonunua nyumba hizo na kuweza kulipa cash wanatakiwa wachunguzwe wamepata wapi pesa hizo, lakini hili halitatokea pamoja na kauli ya hivi karibuni ya Mkuu wa Kaya kwamba hata watu binafsi wenye mapesa mengi inabidi wachunguzwe kwa kuwa na mapesa mengi, labda wameyapa kupitia biashara ya unga, lakini kama tujuavyo kauli za msanii huwa ni kauli ambazo zinaishia hewani tu na kusahaulika.
 
Jamani naona kwa style hii NHC inamalengo mazuri tu,kwa taarifa zilizo rasmi NHC wanataka wauze nyumba zao kwa gharama kubwa ili wapate faida ambayo itawawezesha kutimiza malengo yao ya kujenga majumba maeneo ya dodoma,kigoma na mwanza,na wanataka wao wawe real estate developer wakubwa kwa kujenga nyumba za kisasa....tuendane na mabadiriko ya dunia achaneni na ujamaa.
 
Back
Top Bottom