Nguvu ya uchawi/zindiko la benki

Nguvu ya uchawi/zindiko la benki

Sueky

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2017
Posts
320
Reaction score
204
Wana JF salaam sana.
Kiukweli kitaa huwa kuna maneno na maswali mengine hayapati majibu.

NIANZE HIVI;Jamii ya waAfrika imetawaliwa na imani za Ushirikina na Uchawi. Kwa nchi kama yangu Tanzania na Mozambiqe imani ya uchawi imeshika kasi sana.

Kwa Hapa Tz Mikoa kama, Kigoma, Tanga, Katavi, Ukerewe, Shinyanga-Gamboshi, Kilimanjaro,n.k kiukweli hofu ya ushirikina (Kurogwa)imetawala sana.

Kwa Nchi maskini kama Tanzania Uchawi /Ushirikina ndiyo habari ya kitaa.

Si wasomi, si watawala, dini, hata humu ndani ya JF utakuta hisia za kurogwa zimo kichwani mwa mtu.

Kuna Mbunge mmoja alistua Taifa aliposema Wabunge asilimia 99 wamepitishwa na wachawi kuja Bungeni.

Kitaani mengi huzungumzwa kuhusiana na haya mambo.

Swali ili Linaulizwa sana kitaani"kama wachawi wananguvu ya kupenya kwenye milango na wakafanya wayatakayo nakuondoka salama, Kwanini hawaingii kwenye mabenki wakachukua mshiko?

Wengine husema benki wanalo zindiko kali(lenye nguvu ) kuliko la hawa wachawi wa Katavi a.k.a sumbawanga.

Unafahamu nini kuhusiana na haya mambo?
 
Wachawi hawawezi kuiba fedha na vitu vya kawaida kwa mimi ninavyoona

kwa sababu gani unajua we chukulia tu hapo nyumbani kwako ulishawahi kuweka hela mezani usiku alafu asubuhi ukakuta hamna!!!! Au kusikia mahala mchawi kaingia ndani na kuiba

ingekuwa hivyo watu wote tungekuwa wachawi nafikiri hawana uwezo huo
 
Wachawi hawawezi kuiba fedha na vitu vya kawaida kwa mimi ninavyoona

kwa sababu gani unajua we chukulia tu hapo nyumbani kwako ulishawahi kuweka hela mezani usiku alafu asubuhi ukakuta hamna!!!! Au kusikia mahala mchawi kaingia ndani na kuiba

ingekuwa hivyo watu wote tungekuwa wachawi nafikiri hawana uwezo huo
Wachawi fahari yao kuchuru na kutesa,mambo ya pesa wakiwa kwenye ulimwengu Wa urozi hayana nafasi kwao
 
Kati ya maeneo ambayo kuna zindiko kali sana huko Bongo basi inasemekana ni white house/jumba jeupe feri kivukoni hapo ndio top unaambiwa mageti yote kuanzia geti kuu karibu na ofisi za Ndalichako Profesa mpaka kule nyuma baharini (geti jeusi) basi kama we ni mtu mbaya utaviona kama kuna geti vimepangana kama sita hivi (hizi siyo story za kwenye kahawa ila ni ukweli)

Yote kenda kumi sasa ule ukuta usiuone tu hivo watu wasiojulikana wanaranda randa hapo kuna kuta kama nne hivi moja ni man made na zingine tatu ni (supernatural made fences) so ukiwa na mambo yako hakika utaaibika na kupelekwa kule wasikorudi watu.

Note that serikali aitambui uchawi (wala haina dini) ila serikali ipo vizuri sana katika suala hili tena ina kamati yake ya ufundi sema kafara yao ndo kubwa mno na lazima ifanye kafara kuanzia Tanga-Sahare, kigoma , Sumbawanga, Shinyanga, Ukerewe, Lindi-Mtwara Na Wazee wa Dar-Bwagamoyo kote huku Kuna kamati za ufundi na wapo kwenye payrolls za sirikali . Ngoja niachie hapa wanaojua angalau wataongezea .
 
Kwa jinsi vyuma vilivyokaza nadhani kama ni kweli benki zingekua mufilisi ila kiukweli hizo ni iman tu kama huamini then hakuna matata
 
Back
Top Bottom