Ngumu kumeza kwa CHADEMA

Ngumu kumeza kwa CHADEMA

Isaac JK

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2012
Posts
563
Reaction score
92
VIONGOZI

ngumu kumeza
Kwanza nianze kusema ndani ya chama kuna viongozi hasa baadhi ya viongozi wa juu wa chama wanaokiharibu chama wakiamini kabisa wanakijenga chama. Kiukweli dhamira yao si kukiharibu chama ila maamuzi yao katika shughuli za kichama ndiyo yanachokitia doa chama. Narudia kusema imani yao ya kweli toka moyoni ni kukijenga chama lakini outcome yake ni doa ndani ya chama

mfano 1: Kuna viongozi wapo radhi wavunje sheria za chama ili kukisaidia chama ila mwisho wa siku tunajua sheria tumeziweka ili tuzifate na siyo kuzivunja hata kama ni kwa maslai ya chama la sivyo tutakuwa tunabaka democrasia tunayoiasisi kama chama.Kama sheria ni mbovu haina budi kuibadilisha kwa utaratibu maalum na siyo kuivunja

mfano 2:Kuidhinisha malipo kwa mtu asiyestahili kulipwa hata kama anakisaidia chama ni uvunjaji wa sheria. Kama sheria ilionekana mbovu ni heri ilekebishwe na siyo kuvunjwa na huu ndio utawala wa sheria na ndiyo democrasia makini tunayoiasisi wana chadema

mfano 3:Maamuzi ya kupitisha kauli, malipo au bajeti za chama yafanywe kwa misingi na taratibu za chama na isiwe shinikizo la mtu mmoja. Tusifanya maamuzi ya kumfurahisha mtu mmoja au watu wachache kwa kuhofia uwepo wao ndani ya chama ( chadema ni nguvu ya umma ikibeba dhima ya kusikiliza sauti za wengi ) Tutumie kikao vya chama kupitisha maadhimio kwa misingi ya sheria tulizoziasisi ndani ya chama

WANACHAMA NA WAPENZI WA CHAMA
Wanachama na wapenzi wa chama wajibu wetu namba moja ni kukitetea na kukipigania chama kwa hali na mali huku tukiongeza wigo na kukipanua chama kwa idadi ya wanachama kwani mtaji wa chama ni wanachama. Na hii ndiyo itakayokufanya utimize wajibu ulioainishwa kwenye kadi yako ya chama

ngumu kumeza
kuna wanachama na wapenzi wa chama wapo radhi kukitetea chama kwa hali na mali bila hata kuhoji baadhi ya hoja wanazoulizwa. Kuna baadhi ya mambo ya ukweli kabisa chama kinaonekana kimekosea badala ya kukili tatizo na kujiuliza ni vipi tutalitatua wenyewe ni kutetea tu bila hata ya kukili udhaifu. Ndugu wanachama kukili udhaifu siyo kukubali kushindwa bali ni kujiuliza wapi tumekosea. Tunapokitetea chama tuwe na hoja za msingi na siyo tu kukitetea chama wakati tatizo linaendelea kuwa palepale
mfano1; Huwezi kusema kero zilizotolewa zinafanyiwa kazi wakati wakati miaka inaenda tu hayo siyo majibu ya kutulizisha wanachama tunahitaji utekelezaji uonekane kwa macho juu ya kero zilizotolewa na si maneno

HITIMISHO
Tusiongozwe na fikra za kukitetea tu chama bila kukiambia ukweli tutakuwa tunakiua bila kujua. Umma umetambua kuwa chadema ndiyo chama mkombozi na hivyo basi chadema inatakiwa irudishe fadhira kwa imani iliyopewa na umma. Na mwisho wito wangu kwa wanasiasa wa chadema hasa wabunge wajue kuwa siasa siyo maneno tu bali na vitendo (yaani waegemee kwenye kusema na kutenda )

Kila la heri chadema kwenye ukombozi wa pili na wa kweli wa taifa hili teule lenye utajiri wa rasilimari
 
Kama uko serious na hii, na unahitaji solutions,
nadhani utakuwa umepeleka orijino kwa blog/wesite/vikao/ofisi husika, hapa umeleta kopi kwa sie tusiohusika - (malengo?) nadhani ni mazuri tu
 
Isaac JK;
Haya maoni ungekuwa vyema sana kama ungeyapeleka kwenye vikao husika; hapa JF sio mahala pake kabisa; zaidi utatukanwana kuitwa masalia au umetumwa na CCM; Chadema ni private entity inayoendeshwa kwa misingi ya kujuana; katiba ipo tu kwa ajili ya kumzuga msajili wa vyama; labda wsaliana na watu kama akina Ben Saanane watakupa maelekezo nini cha kufanya ili ujumbe wako ufike.

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
Huyu jamaa michango yake huwa naikubali ,lakini huu uzi wa leo ni mashaka makubwa. Kama hakudhulumiwa basi kuna namna
 
Changamoto popote zipo, Chamsingi ni kutumia mbinu bora na thabiti ktk kuzitatua bila kuathiri unachopigania kisiathiriwe."Ya ndani yajadiliwe ndani" na "ya nje yajadiliwe nje."
 
mfano 2:Kuidhinisha malipo kwa mtu asiyestahili kulipwa hata kama anakisaidia chama ni uvunjaji wa sheria. Kama sheria ilionekana mbovu ni heri ilekebishwe na siyo kuvunjwa na huu ndio utawala wa sheria na ndiyo democrasia makini tunayoiasisi wana chadema

Hapo kwenye red, can som,eone explain to me ni nani katika chadema analipwa ambaye hastahili? Mtoa mada hebu kuwa specific katika hilo.
 
mfano 1: Kuna viongozi wapo radhi wavunje sheria za chama ili kukisaidia chama ila mwisho wa siku tunajua sheria tumeziweka ili tuzifate na siyo kuzivunja hata kama ni kwa maslai ya chama la sivyo tutakuwa tunabaka democrasia tunayoiasisi kama chama.Kama sheria ni mbovu haina budi kuibadilisha kwa utaratibu maalum na siyo kuivunja

mfano 2:Kuidhinisha malipo kwa mtu asiyestahili kulipwa hata kama anakisaidia chama ni uvunjaji wa sheria. Kama sheria ilionekana mbovu ni heri ilekebishwe na siyo kuvunjwa na huu ndio utawala wa sheria na ndiyo democrasia makini tunayoiasisi wana chadema

mfano 3:Maamuzi ya kupitisha kauli, malipo au bajeti za chama yafanywe kwa misingi na taratibu za chama na isiwe shinikizo la mtu mmoja. Tusifanya maamuzi ya kumfurahisha mtu mmoja au watu wachache kwa kuhofia uwepo wao ndani ya chama ( chadema ni nguvu ya umma ikibeba dhima ya kusikiliza sauti za wengi ) Tutumie kikao vya chama kupitisha maadhimio kwa misingi ya sheria tulizoziasisi ndani ya chama

Mifano uliyotoa yote ni halisi:

Mfano wa kwanza - Mbowe kukataza chadema kuchukua wanachama wanaohamia toka CCM. Hakuna kipengele cha katiba ya chadema kinachohalalisha maamuzi haya ya Mbowe.

Watu kukatazwa kugombea uongozi kwa kigezo kwamba "they are from nowhere".

Mfano wa pili - Josephine Mushumbusi kulipwa mamilioni kwa kisingizio cha kujitolea.

Heche kuidhinishiwa mshahara mnono wakati nafasi yake ni ya kujitolea na wasaidizi wake wote hawalipwi kitu.

Mfano wa tatu - Chama kuuziwa magari chakavu ya viongozi

Tenda za kununua magari ya M4C kuchukuliwa kinyemela na viongozi.

Hapo kwa uchache katika kila mfano ulioweka nimeweka mifano halisi miwili, lakini ipo mingi sana.

Chadema ni chama kinachoendeshwa kwa misingi ya ulaghai...
 
umeongea kimafumbo zaidi, labda nia yako uwapatie kula kina chama maana contribution kwenye mada kama hizi inawaingizia siku. zaidi ungesema na kutoa mfano japokuwa pia tungekuona mnafiki, ukiwa na mapenzi mema mahali pa kupeleka ushauri pako. mmewahi kuishauri ccm wakati wowote hadharani au hawana mapungufu?
 
Hii kweli ngumu kumeza. Ukitaka kujua hilo subiri likes utakazopewa na Machadema!

Hawa ni watakatifu hawastahili kukosolewa.
 
Isaac JK inaonyesha ni mchanga sana katika ulingo wa siasa , hivi unataka kuniambia CHADEMA mahali wanapokosea hawana muda wa kujirekebisha ? wewe unataka wanachama wa CHADEMA wawe wanakishambulia chama chao humu jukwaani, mtu anaitwa mwanachama wa chama fulani alfu anakishambulia humu jukwaani uanachama wake huyo mtu unamashaka mengi

Mwenye mapenzi mema na chama ushauri upeleka ofisi husika
 
Mficha maradhi.............?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
VIONGOZI

ngumu kumeza
Kwanza nianze kusema ndani ya chama kuna viongozi hasa baadhi ya viongozi wa juu wa chama wanaokiharibu chama wakiamini kabisa wanakijenga chama. Kiukweli dhamira yao si kukiharibu chama ila maamuzi yao katika shughuli za kichama ndiyo yanachokitia doa chama. Narudia kusema imani yao ya kweli toka moyoni ni kukijenga chama lakini outcome yake ni doa ndani ya chama

mfano 1: Kuna viongozi wapo radhi wavunje sheria za chama ili kukisaidia chama ila mwisho wa siku tunajua sheria tumeziweka ili tuzifate na siyo kuzivunja hata kama ni kwa maslai ya chama la sivyo tutakuwa tunabaka democrasia tunayoiasisi kama chama.Kama sheria ni mbovu haina budi kuibadilisha kwa utaratibu maalum na siyo kuivunja

mfano 2:Kuidhinisha malipo kwa mtu asiyestahili kulipwa hata kama anakisaidia chama ni uvunjaji wa sheria. Kama sheria ilionekana mbovu ni heri ilekebishwe na siyo kuvunjwa na huu ndio utawala wa sheria na ndiyo democrasia makini tunayoiasisi wana chadema

mfano 3:Maamuzi ya kupitisha kauli, malipo au bajeti za chama yafanywe kwa misingi na taratibu za chama na isiwe shinikizo la mtu mmoja. Tusifanya maamuzi ya kumfurahisha mtu mmoja au watu wachache kwa kuhofia uwepo wao ndani ya chama ( chadema ni nguvu ya umma ikibeba dhima ya kusikiliza sauti za wengi ) Tutumie kikao vya chama kupitisha maadhimio kwa misingi ya sheria tulizoziasisi ndani ya chama

WANACHAMA NA WAPENZI WA CHAMA
Wanachama na wapenzi wa chama wajibu wetu namba moja ni kukitetea na kukipigania chama kwa hali na mali huku tukiongeza wigo na kukipanua chama kwa idadi ya wanachama kwani mtaji wa chama ni wanachama. Na hii ndiyo itakayokufanya utimize wajibu ulioainishwa kwenye kadi yako ya chama

ngumu kumeza
kuna wanachama na wapenzi wa chama wapo radhi kukitetea chama kwa hali na mali bila hata kuhoji baadhi ya hoja wanazoulizwa. Kuna baadhi ya mambo ya ukweli kabisa chama kinaonekana kimekosea badala ya kukili tatizo na kujiuliza ni vipi tutalitatua wenyewe ni kutetea tu bila hata ya kukili udhaifu. Ndugu wanachama kukili udhaifu siyo kukubali kushindwa bali ni kujiuliza wapi tumekosea. Tunapokitetea chama tuwe na hoja za msingi na siyo tu kukitetea chama wakati tatizo linaendelea kuwa palepale
mfano1; Huwezi kusema kero zilizotolewa zinafanyiwa kazi wakati wakati miaka inaenda tu hayo siyo majibu ya kutulizisha wanachama tunahitaji utekelezaji uonekane kwa macho juu ya kero zilizotolewa na si maneno

HITIMISHO
Tusiongozwe na fikra za kukitetea tu chama bila kukiambia ukweli tutakuwa tunakiua bila kujua. Umma umetambua kuwa chadema ndiyo chama mkombozi na hivyo basi chadema inatakiwa irudishe fadhira kwa imani iliyopewa na umma. Na mwisho wito wangu kwa wanasiasa wa chadema hasa wabunge wajue kuwa siasa siyo maneno tu bali na vitendo (yaani waegemee kwenye kusema na kutenda )

Kila la heri chadema kwenye ukombozi wa pili na wa kweli wa taifa hili teule lenye utajiri wa rasilimari


Haina ugumu wowote wa kumeza ni ushauri wa kawaida tu huo. naunga mkono hoja
 
Siku zote pale binadamu anapokosa ujasiri wa kupokea hoja za wengine na kubakia kubeza na kujiaminisha tayari ni udhaifu mkubwa,na kwa maana nyingine ni "WOGA"........Ukweli huuma lakini mtu jasiri huupokea na kuufanyia kazi. Naunga mkono hoja.
 
Huo ushauri upeleke kwa mzee wa tembo! Ni mangapi yanafanywa na serikali yako na umekaa kimya? Wewe umeliona hilo tu?
 
Back
Top Bottom