Mjusi Sharobalo
JF-Expert Member
- Sep 4, 2025
- 8,279
- 14,566
Leo kwenye pitapita zangu za kufukuzia shiling mjini, nikakutana na jamaa yangu mmoja wa kitambo hivi, Akawa amenipatia dili la maana na kushitua moyo kidogo.
Hivyo raha kunizidi moyoni, nikaamua nijivute sehemu nipate soda kidogo nimwagilie moyo. Nimemkuta binti wa zamani kidogo hayo maeneo, nimeagiza zangu soda imefika mezani, kaifungua nikapiga funda moja kwanza halafu nikauliza hii soda si jero? Kumbe nikawa nimekosea akaniona mimi wa kuja mjini hapa, akanijibu inauzwa buku. Ikabidi nivunge, nikamwambia sawa huku nashushia taratibu. Badae chupa kuisha nikavuta pochi nikamchomolea buku nikampatia nione atafanyaje kapokea kakausha, badae kidigo kanyanyuka kaingia ndani ananichungulia mlangoni aone kama naondoka au vipi, Kuona nimemshitukia kageuza na soda moja kaifungua kaanza kuishushIa taratibu. Dadeki roho imeniuma kishenzi, nashuhudia jero langu limekuwa ofa bila kibali changu mbele ya macho yangu. Anyway niliamua kukausha tu, maana amenifundisha kitu kipya, Ng'ombe hazeeki maini jambazi ni jambazi tu.
Hivyo raha kunizidi moyoni, nikaamua nijivute sehemu nipate soda kidogo nimwagilie moyo. Nimemkuta binti wa zamani kidogo hayo maeneo, nimeagiza zangu soda imefika mezani, kaifungua nikapiga funda moja kwanza halafu nikauliza hii soda si jero? Kumbe nikawa nimekosea akaniona mimi wa kuja mjini hapa, akanijibu inauzwa buku. Ikabidi nivunge, nikamwambia sawa huku nashushia taratibu. Badae chupa kuisha nikavuta pochi nikamchomolea buku nikampatia nione atafanyaje kapokea kakausha, badae kidigo kanyanyuka kaingia ndani ananichungulia mlangoni aone kama naondoka au vipi, Kuona nimemshitukia kageuza na soda moja kaifungua kaanza kuishushIa taratibu. Dadeki roho imeniuma kishenzi, nashuhudia jero langu limekuwa ofa bila kibali changu mbele ya macho yangu. Anyway niliamua kukausha tu, maana amenifundisha kitu kipya, Ng'ombe hazeeki maini jambazi ni jambazi tu.