Ngoma ya escrow kumbe ni standard chartered

Ngoma ya escrow kumbe ni standard chartered

Sawa. Basi toa ya kwako.
.......usikasirike; wewe weka hoja hapa uone tutakavyoidadavua sio propaganda za kienyeji; kaja na mwenzio hapaa, "fedha za ESCROW sio za umma," well, hata kama, ndio zichotwe tu vile!!!!
 
Maelezo marefu ya kutetea wizi, wizi ni wizi. Hatuwezi kujustify wizi kwa kigezo cha kumuendeleza mtoto wa kike.
 
Hao Standard Chartered walitakiwa wakaidai Mechmar walioikopesha na si IPTL wala TANESCO. N akisheria Mechmar imefilisika, STANDARD CHARTERS wanaatakiwa wadai Insurance lakini badala yake wanakuja kuidai TANESCO kwa kuwa tu TANESCO wamelala doro.

Wamelala doro kwa kuwa wangenunua wao wenyewe kwa mkopo mitambo mizuri zaidi ya hiyo na mpaka sasa deni lingekuwa limekwisha zzamani na umeme kushuka bei.

TANESCO walikuwa wanajifikiria matumbo yao tu mpaka Kikwete alipokuja na kubadilisha mambo kwa kuamua kununuwa mitambo yetu wenyewe na si kukodisha tena, Kinyerezi I, II, III na IV.

Kudos Kikwete.
Mitambo yenu wenyewe kwa ile 50% ya hisa za PAP, wacha TANESCO na watanzania waendelee kulala doro. Like you said, kudos Kikwete.
 
Hii drama ina episode na twists ngapi jamani? Subiri niongeze popcorn.
 
Zungusheni tuuuu, hakuna wizi halali, waweke hadhari tujue mbivu na mbichi wakiamua kuwasamehe sawa, wakiwawajibisha poa. Tunachojua wameiba haaaaaaaaa.
 


ni jambo jema kabisa kuwa umeanzisha mjadala kuhusu shule ya babro johansen, hii shule ni ya kifisadi tokea siku ya kwanza. Eneo ilipojengwa lilikuwa ni shamba la wizara ya kilimo kituo cha utafiti wa mifugo luguruni.

Wananchi wa mtaa wa luguuni waliomba kupitia eneo kwa ajili ya kujenga
shule ya msingi na maombi hayo kupelekwa kwa mkuu wa wilaya wa wakati huo mhe ritha mlaki. Kwa kutumia maombi hayo ya waanchi ndipo shule ya babro johansen ikakatiwa ekari 50 toka shamba la serikali kwa kutumia kutumia maombi ya wananchi

ufisadi mwingine wa mama tibaijuka na shule yake na katika kupata maji.

Mwaka 1998 kijiji cha kwembe ilipo shule hiyo kiliomba msaada toka ubalozi wa japani kwa ajili ya mradi wa maji, kijiji kilipopata msaada wa milioni 95; mwaka 1999 shule ya barbro johansen nayo pia ikaomba msaada toka ubalozi wa japani kwa ajili ya mradi wa maji na kufanikiwa kupata kiasi kama hicho pia.

Matokeo yake mama tibaijuka na uongozi wa shule ukawahonga watumishi wa dawasa waliokuwa wakitekeleza miradi hii miwili ile ya kijiji cha kwembe na shule na kufanikiwa kujichukulia tolea la maji toka bomba kuu lililokuwa limeandaliwa maalau kwa ajili ya kijiji cha kwembe kwa ajili ya kijiji cha kwembe na kusababisha wanakaijiji kukosa huduma ya maji tokea mwaka 1999 hadi 2012, kwa zaidi ya miaka 20 huku shule hiyo ikiwanyima wanakajiji huduma ya maji hata ya kuchota kwa ndoo.

Kibaya zaidi kwa kutumia vibaya madaraka yake mama tibaijuka ili shule yake iweze kuwa katika maeneo yenye thamani kubwa akanzisha mradi wa kutwaa ardhi za wananchi wanaozunguka shule hiyo ili ardhi hiyo ipimwe viwanja huku wananchi wakilipwa fidia kiduchu sana.

Cha ajabu licha ya mama tibaijuka kupokjea fidia ya ardhi yake takribani ekari 4 akatumia madaraka yake ya uwaziri wa ardhi vibaya kuzuia viwanja vilivyopimwa katika shamba hilo visigawiwe kwa wananchi wengine na hivyo mashamba ya wananchi wanyonge tu ndio yakagawiwa viwanja watu wengine na yeye kujipatia viwanja zaidi kuliko ardhi aliyokuwa nayo hapo awali.

Kwa kifui huyu mama ni fisadi tu!!!!!!

Mama Tiba naye yumo! Huyu ndo alikuwa anawekwa kwenye orodha ya Wagombea Urais! Kweli CCM kila mtu kaoza.
 
ok. tumekuelewa, lakini bring back our money you fisadi wa escrow and allies.
 
Na hata shinikizo la Serikali ya Tanzania kukatiwa misaada ya bajeti na hao wanaoitwa washirika wa maendeleo ni shinikizo kutoka serikali ya uingereza kupitia balozi wake nchini Tanzania,hawa watu ni hodari sana hasa linapokuja kuja suala la masilahi ya nchi zao,si unakumbuka suala la rada?walinyamaza kimya wote mpaka waziri mkuu wao Tony Blair,wakati yule Mama Claire Short alipokuwa anapiga kelele kwamba nchi masikini ya Tanzania inanyonywa kwa kkuuziwa rada kwa bei ghali,mpaka mahakama ilipokuja kuamua vingine.Hao jamaa kwa ni maslahi tu.

kumbe ndani jm kuna kundi kubwa la majuha watu wasiokubali ukweli sasa naelewa tz tunachezewa kwa sababu ni wazembe wa kufukiri
 
Msituchoshe! Hii habari iko kwenye magazeti ya leo kama "MAKALA YA MTANGAZAJI". Nmeiona ktk Mwananchi na Jamhuri. Kwa ufupi tu, Mtajisafisha sana mwaka huu, ila angalieni msitoke wachafu!
 
Na hata ukikiuzia chama chako mafuso chakavu mawili kwa millioni mia sita, bei ambayo unaweza kununuwa kumi na mawili, wewe unaonekana wa maana tu.

Kwani huwa unajisikiaje ukiambiwa ukweli we niambie tu usiogope.
 
ImageUploadedByJamiiForums1416909865.697643.jpg
Ifupishe tuweze kuisoma
 
Hao Standard Chartered walitakiwa wakaidai Mechmar walioikopesha na si IPTL wala TANESCO. N akisheria Mechmar imefilisika, STANDARD CHARTERS wanaatakiwa wadai Insurance lakini badala yake wanakuja kuidai TANESCO kwa kuwa tu TANESCO wamelala doro.

Wamelala doro kwa kuwa wangenunua wao wenyewe kwa mkopo mitambo mizuri zaidi ya hiyo na mpaka sasa deni lingekuwa limekwisha zzamani na umeme kushuka bei.

TANESCO walikuwa wanajifikiria matumbo yao tu mpaka Kikwete alipokuja na kubadilisha mambo kwa kuamua kununuwa mitambo yetu wenyewe na si kukodisha tena, Kinyerezi I, II, III na IV.

Kudos Kikwete.

Pendekezo la kununu mitambo Mipya ya Mafuta lilikuwepo na lilipelekwa wizarani kwa Waziri wa NISHATI NA MADINI wa wakati huo, Ndugu JAKaYA MRiSHO KiKWETE, Akalikataa hilo pendekezo kwa maelezo kwamba Raisi ALHjI ALLy HaSSAN MwINYI amepata mwekezaji IPTL
 
Faiza you are better than this......ni vipi kama ukinyamaza kutojibu issues kama hizi

Mwee bora na wewe umeliona hili tatizo halafu msomi na nje kakaa hivi faiza fox huwa unafanya kusudiii au dharauu ? Manake huwa sikusomi ujue mbili haumo wala tatu.
 
Mama Tiba naye yumo! Huyu ndo alikuwa anawekwa kwenye orodha ya Wagombea Urais! Kweli CCM kila mtu kaoza.

Hapo ndio maandiko yanapotimia Mungu humuumbua mnafiki na wapo wengi tu tuombeane uzima.
 
Back
Top Bottom