Mkuu hilo jina lako...!!!Umeambiwa ngano, masuala ya viazi na migoho yanatokea wapi?;
katika nafaka, ngano ni nafaka hatari sana. Ikiwemo na wenzake kama shayiri. Si lazima iueAngalia headline ya habari yako.Imefanya ulichoandika kikose ukweli.Huwezi kufa kwa kula vinavyotokana na ngano.Ukiwa na gluten intolerance haifanyi ngano iwe "nafaka hatari sana".
Ni jina la kawaida huku Japan Mkuu
Inaokwa kawaida tu kwa kutumia unga wa dona. Lakini hawatumii hamira, wanatumia tu baking powder.Mikate ya mahindi ipoje??, juu ya yote unga wa sembe siku hizi unatiwa virutubisho (fortification chemicals), sina hakika kama hizo fortifications zina usalama gani!!.
Hapana, kwa upande wangu nakuwa nahisi kushiba mda woteHivi kujaa gas maana yake ndio kila saa unakua unajamba au?Hua sielewi vzr hio sentence mkuu
Pole Sana mkuu.Hapana, kwa upande wangu nakuwa nahisi kushiba mda wote
Kwa hii life ya ki TZ ngano ni pagumu mtu kukuelewa athari maana ndiyo mlo mkuuNgano ni nafaka hatari sana na watz wengi hatufahamu. Tofauti na nafaka zingine kama mahindi, ulezi, mtama na mchele, ngano ina aina fulani ya protin inayoitwa Gluten. Protin hii ndiyo hufanya ngano ikikandwa iwe kama banzoka wakati ukikanda unga wa mahindi hauwi namna ile.
Sasa hii protin inaweza kusababisha mzio(allergy/autoimmune reaction) ya hatari sana. Kifupi inaweza sababisha mwili ujishambulie. Maeneo yanayoathirika zaidi ni utumbo mdogo. Hili linaweza sababisha kuharisha bila kukoma, tumbo kujaa gesi, udumavu na afya dhaifu.
Pia inaweza athiri ngozi na mtu kutoka mapele ya kuwasha kama mwenye ugonjwa mkali wa ngozi.
Pia inaweza sababisha matatizo kwenye ubongo na kusababisha mtu atembee kama aliyelewa.
Inasemwa kuwa matatizo haya hutokea hadi kwa asilimia 2 ya watu wote.
Ni vyema tukatumia mikate ya mahindi, ulezi nk. Ngano ni hatari sana.