Basi Nenda
JF-Expert Member
- Jul 29, 2017
- 20,184
- 45,910
Michael anatajwa kuwa moja kati ya watumbuizaji bora zaidi kuwahi kutokea hapa duniani,lakini pia watu wengi humfahamu kama mwanamuziki aliyekuwa na visa vingi zaidi duniani.
Moja kati ya sifa zake kubwa ni kwamba mtu huyu alikuwa ni mtoto aliyekataa kukuwa kama PETER PAN ambaye ni muhusika katika stori za watoto ambaye yeye aliishi kwenye kisiwa ambacho watoto hawakuwi ,hawazeeki na hawafi,kisiwa hicho ni never land
Michael jackson aliipenda sana stori hii ya peter pan, huenda kwa sababu alikuwa na mambo na matendo ya kitoto wakati ni mtu mzima,mapenzi yake hayo kwa hadithi hiyo ilipelekea naye ajijengee never land yake mwenyewe kama ya peter pan
Basi akanunua eneo lenye ukubwa wa ekari 12,700 huko California kwa USD 19.5 million, mwaka 1987 na kulifanya makazi binafsi,vifuatavyo ni vitu alivyoweka humo ndani
1.TRAIN STATION
Michael jackson alinunua train mbili za mvuke na kujenga reli ( three railroads: one 3 ft (914 mm) narrow gauge named "Neverland Valley Railroad) kwake pamoja na train station kubwa kuliko ile ya kigoma,train hizo zilifanya kazi ya kumzungusha tu homo ndani yeye na wageni wake ambao wengi ni watoto
Na palikuwa na wahudumu kabisa waliogawa ice cream ,pipi nk kwa wageni,
Baadae aliongeza treni moja ya umeme kwa ajili ya watoto wake
2.ZOO (bustani ya wanyama)
Michael jackson alikua ni mtu mpenda wanyama sana,kwa mfano alinunua sokwe kwa usd 65,000 sokwe mmoja tu aliyeitwa bubble,alisafiri nae kote duniani alipokwenda na alipandishwa first class kwenye ndege,
Kwenye zoo yake aliweka wanyama kama tiger,simba,tembo,twiga ,swala,mbuni nk
3. AMUSEMENT PARK
Michael alipenda sana michezo ya kitoto hivyo alijenga nyumbani kwake hapo sehemu ya kuchezea na kuweka vitu kama. Ferris wheel ,
Carousel, Zipper , Octopus, Pirate Ship ,
Wave Swinger, Super Slide, roller coaster, bumper cars (gari za umeme) na
amusement arcade
4.ARTIFICIAL LAKE (ziwa bandia)
Mj hakuishia hapo alijenga ziwa bandia lenye ukubwa wa heka nne likiwa na maporomoko ya maji,
5.VIWANJA VYA MICHEZO
michael aliweka viwanja vya basketball , tennis nk
6.NYUMBA ZA MAKAZI NA WAGENI
nyumba aliyoishi ilikua na vyumba 6 vya kulala na bafu 9
-kulikuwa na nyumba ya wafanyakazi
-nyumba ya zimamoto (fire department)
-nyumba za wageni
-jumba la cinema la kutosha watu 50
Neveland iliendelea kuwa makazi ya michael mpaka mwanzoni mwa miaka ya 2000 ambapo alikataa kurudi kuishi hapo kwa sababu police walipafanyia uchunguzi juu ya tuhuma zake za kubaka watoto,alidai wamepadhalilisha hivyo hawezi tena kurudi,na hakurudi kuishi hapo mpaka anakufa
NB: Kwa sasa makazi hayo yanauzwa kwa dau la USD 100 million
Moja kati ya sifa zake kubwa ni kwamba mtu huyu alikuwa ni mtoto aliyekataa kukuwa kama PETER PAN ambaye ni muhusika katika stori za watoto ambaye yeye aliishi kwenye kisiwa ambacho watoto hawakuwi ,hawazeeki na hawafi,kisiwa hicho ni never land
Michael jackson aliipenda sana stori hii ya peter pan, huenda kwa sababu alikuwa na mambo na matendo ya kitoto wakati ni mtu mzima,mapenzi yake hayo kwa hadithi hiyo ilipelekea naye ajijengee never land yake mwenyewe kama ya peter pan
Basi akanunua eneo lenye ukubwa wa ekari 12,700 huko California kwa USD 19.5 million, mwaka 1987 na kulifanya makazi binafsi,vifuatavyo ni vitu alivyoweka humo ndani
1.TRAIN STATION
Michael jackson alinunua train mbili za mvuke na kujenga reli ( three railroads: one 3 ft (914 mm) narrow gauge named "Neverland Valley Railroad) kwake pamoja na train station kubwa kuliko ile ya kigoma,train hizo zilifanya kazi ya kumzungusha tu homo ndani yeye na wageni wake ambao wengi ni watoto
Na palikuwa na wahudumu kabisa waliogawa ice cream ,pipi nk kwa wageni,
Baadae aliongeza treni moja ya umeme kwa ajili ya watoto wake
2.ZOO (bustani ya wanyama)
Michael jackson alikua ni mtu mpenda wanyama sana,kwa mfano alinunua sokwe kwa usd 65,000 sokwe mmoja tu aliyeitwa bubble,alisafiri nae kote duniani alipokwenda na alipandishwa first class kwenye ndege,
Kwenye zoo yake aliweka wanyama kama tiger,simba,tembo,twiga ,swala,mbuni nk
3. AMUSEMENT PARK
Michael alipenda sana michezo ya kitoto hivyo alijenga nyumbani kwake hapo sehemu ya kuchezea na kuweka vitu kama. Ferris wheel ,
Carousel, Zipper , Octopus, Pirate Ship ,
Wave Swinger, Super Slide, roller coaster, bumper cars (gari za umeme) na
amusement arcade
4.ARTIFICIAL LAKE (ziwa bandia)
Mj hakuishia hapo alijenga ziwa bandia lenye ukubwa wa heka nne likiwa na maporomoko ya maji,
5.VIWANJA VYA MICHEZO
michael aliweka viwanja vya basketball , tennis nk
6.NYUMBA ZA MAKAZI NA WAGENI
nyumba aliyoishi ilikua na vyumba 6 vya kulala na bafu 9
-kulikuwa na nyumba ya wafanyakazi
-nyumba ya zimamoto (fire department)
-nyumba za wageni
-jumba la cinema la kutosha watu 50
Neveland iliendelea kuwa makazi ya michael mpaka mwanzoni mwa miaka ya 2000 ambapo alikataa kurudi kuishi hapo kwa sababu police walipafanyia uchunguzi juu ya tuhuma zake za kubaka watoto,alidai wamepadhalilisha hivyo hawezi tena kurudi,na hakurudi kuishi hapo mpaka anakufa
NB: Kwa sasa makazi hayo yanauzwa kwa dau la USD 100 million