PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,724
Nilitembelea familia fulani, lakini katika maongezi tukaishia kuongelea suala la Neti za mbu zenye dawa maalum(viwatilifu) inayodumu kwa miaka 3 hadi 5, maarufu kama neti za George Bush.
Huyo mwenyeji wangu alinambia kuwa hathubutu, na hatajaribisha kutumia neti za mbu zenye dawa, akidai kuwa anajua kwa uhakika kuwa zimeletwa Africa na Wamarekani kwa lengo la kupunguza nguvu za uzazi kwa jinsia zote(ke na me) kwa taratibu sana, lakini pia kuleta hali fulani ya uzezeta, in a long-run, na kuwa WAZUNGU HAWAZITUMII KABISA, na kuwa kwao hawatumii viwatilifu!
Akaendelea kueleza kuwa Wazungu hawa ni wajanja sana, wanaona fedheha sana kwa Africa kuwa na malighafi nyingi namna hii, na hivyo walichofanya ni kubuni utaratibu wa kuwadumaza akili polepole na hatimaye ndani ya miaka takriban 50 ijayo, basi kizazi chote cha Africa kiwe na mtindio, na waweze kujiingilia Africa kama kwao na kuchukua kila kilichobaki wakikisombea kwao!
Na kwa kukazia hilo, alisema Neti hizi ni 'FOR AFRICA ONLY!'
Lakini mbali ya huyu jamaa, kuna sehemu kibao tumezisikia kwenye newz wakizitumia hizi net za Bush kwa uvuvi au kama chekeche, madai yao ni kwamba zinaua nguvu ya uzazi.
Wakuu, hizi ni kama stories, lakini huenda kukawa na substance ndani yake!...Je kuna anayejua content ya hiyo kemikali inayowekwa, huenda na maelezo kidogo ya kuridhisha?
Nawasilisha kwa mjadala.
Huyo mwenyeji wangu alinambia kuwa hathubutu, na hatajaribisha kutumia neti za mbu zenye dawa, akidai kuwa anajua kwa uhakika kuwa zimeletwa Africa na Wamarekani kwa lengo la kupunguza nguvu za uzazi kwa jinsia zote(ke na me) kwa taratibu sana, lakini pia kuleta hali fulani ya uzezeta, in a long-run, na kuwa WAZUNGU HAWAZITUMII KABISA, na kuwa kwao hawatumii viwatilifu!
Akaendelea kueleza kuwa Wazungu hawa ni wajanja sana, wanaona fedheha sana kwa Africa kuwa na malighafi nyingi namna hii, na hivyo walichofanya ni kubuni utaratibu wa kuwadumaza akili polepole na hatimaye ndani ya miaka takriban 50 ijayo, basi kizazi chote cha Africa kiwe na mtindio, na waweze kujiingilia Africa kama kwao na kuchukua kila kilichobaki wakikisombea kwao!
Na kwa kukazia hilo, alisema Neti hizi ni 'FOR AFRICA ONLY!'
Lakini mbali ya huyu jamaa, kuna sehemu kibao tumezisikia kwenye newz wakizitumia hizi net za Bush kwa uvuvi au kama chekeche, madai yao ni kwamba zinaua nguvu ya uzazi.
Wakuu, hizi ni kama stories, lakini huenda kukawa na substance ndani yake!...Je kuna anayejua content ya hiyo kemikali inayowekwa, huenda na maelezo kidogo ya kuridhisha?
Nawasilisha kwa mjadala.