Nenda mpenzi wangu

Nenda mpenzi wangu

Surupwenye

Member
Joined
Jan 29, 2015
Posts
7
Reaction score
2
Habari wana Jf?

Ni siku nzuri na ya pekee sana huwa tuna iita jumapili .

Kiukweli nimeamini kweli mapenzi yana nguvu sana pale tu unapo tokea kumpenda mtu kwa dhati pasi kujiegemeza kwa uzuri wa sura, mavazi , pesa , nk .

Tarehe kama ya leo mwaka jana ni siku ambayo katu sitokuja kuisahau ni siku ambayo mpenzi wangu ninaye mpenda alinikubalia ombi langu na hii tarehe ndipo nilipo ambiwa neno zuri ambalo kwa sasa hata siitaji kulisikia kutokana na huyu mwanamke niliye mpenda kuto taka kunipenda tena na hii imetokana na umbali tuliokuwa nao nahisi hili ndio tatizo kubwa kwa upande wake .

Na ameniomba tubaki marafiki tu sina jinsi ya kufanya na sijawahi kuumizwa au kuhisi kuumia juu ya mapenzi na kwa mala ya kwanza sasa kupatwa na haya maumivu na kikubwa zaidi kinacho niumiza ni kutokuniheshimu napigia simu anakata sms hazijibiwi na nimepata taarifa kuwa kunajamaa anafanya yake na soon wanafunga ndoa .

Ujumla wa haya niliyo yaandika ni moja ya njia ya kupunguza msongo wa mawazo najua Mungu yu pamoja nami na kiroho safi mpenzi wangu D.... We nenda tu .
 
Yamoyoni Hayo Kaka...Pole sana maana ndiyo ukubwa huo mkuu.
 
Usijali we sio wa kwanza kuachwa. Mlango mmoja ukifungwa Mungu anakufungulia mamilango kibao...achana nae
 
Diana Dorini Digna Dorothea Demetria Debora Delila Dativa Deonisia
Dorkas Dolorosa
Pole Mtu Wangu
 
Pole sana mkuu.Ulimpenda na ukamheshimu ukashindwa kubaki ktk ukawaida wako.Alipata mtu ambae hayuko emotional kama wewe alie kwenye ukawaida wake..Tulia anza tena na zingatia mapungufu yako yasiwe kikwazo tena katika kuwa na mapenzi yenye kudumu..
 
Habari wana jf? Ni siku nzuri na ya pekee sana huwa tuna iita jumapili . Kiukweli nimeamini kweli mapenzi yana nguvu sana pale tu unapo tokea kumpenda mtu kwa dhati pasi kujiegemeza kwa uzuri wa sura, mavazi , pesa , nk . Tarehe kama ya leo mwaka jana ni siku ambayo katu sitokuja kuisahau ni siku ambayo mpenzi wangu ninaye mpenda alinikubalia ombi langu na hii tarehe ndipo nilipo ambiwa neno zuri ambalo kwa sasa hata siitaji kulisikia kutokana na huyu mwanamke niliye mpenda kuto taka kunipenda tena na hii imetokana na umbali tuliokuwa nao nahisi hili ndio tatizo kubwa kwa upande wake . Na ameniomba tubaki marafiki tu sina jinsi ya kufanya na sijawahi kuumizwa au kuhisi kuumia juu ya mapenzi na kwa mala ya kwanza sasa kupatwa na haya maumivu na kikubwa zaidi kinacho niumiza ni kutokuniheshimu napigia simu anakata sms hazijibiwi na nimepata taarifa kuwa kunajamaa anafanya yake na soon wanafunga ndoa . Ujumla wa haya niliyo yaandika ni moja ya njia ya kupunguza msongo wa mawazo najua mungu yu pamoja nami na kiroho safi mpenzi wangu D.... We nenda tu .

Pole Mkuu
 
Kiroho safi muache aolewe utampata na wewe wako umuoe maana kila jambo linatokea mie huwa naamini ni mipango ya Mungu
 
Wanawake nao wakati mwingine hawapendi ving'ang'anizi sana.

Pole mkuu. Nenda D, hakuna namna nyingine.
 
mpe shukrani kwa kuniumiza moyo wangu, mwambie mi bado mahututi nauguza kidonda changu,
 
Tatizo me bado nilipoteleza nikakosa sipajui, hadi akafunga virago na akaamua kuondoka sitambui

kibaya kinachoniumiza maneno, neno, maneno,
mara kwa ndugu marafiki kutwa kuwapa misemo
 
Hahahaha njoo kwangu mimi nitakutuliza moyoni na akilini. Ameamua kwenda mimi ninakuja kuweka nanga.

Mie na matozi mbali kabisaaa, so jaribu fukwe nyingine teh!
 
Back
Top Bottom