Ni kweli umekaa/umetutumikia muda mrefu,sasa ni wakati wako wa kupumzika,wala usijisikie vibaya kushindwa. Hata kama hakuna tafrija ya kukuaga,mimi nitakuaga kwa kukushukuru kwa machache mazuri uliyofanya.
Ulijitahidi sana kuhakikisha Njombe inakuwa na shule nyingi ( NDDT),hata kama ulishirikiana na wenzako,vijana wengi tulisoma ktk shule zile. Sijui kama ilikuwa ni juhudi yako au la,nakumbuka ulikuja kufungua RTC kijijini kwetu,porini kwelikweli. Na vituo vya afya vikawa vingi,kilimo kikawa juu,nk.
Nilikuona 1979 ukienda Makete kuweka jiwe la msingi ili eneo hilo liwe Wilaya pamoja na Ludewa ukiongozana na Sokoine (RIP),ukiwa mbunge wa wilaya yetu. Baadaye Njombe ikawa na wabunge watatu,wewe upo. Na baadae Njombe imekuwa Mkoa, wewe upo ktk usukani,hapana sasa mzee nenda kapumzike.
Wewe ndiye Mbunge pekee uliyewahi kuongoza wilaya iliyozaa wilaya mbili,bado eneo lako likazaa majimbo mawili mapya,na bado eneo lako ulilowakilisha kwa kipindi chote ukiwa Mbunge likawa mkoa. Wewe ni mzee wetu wa mkoa,nenda kapumzike kwa amani.
Ulijitahidi sana kuhakikisha Njombe inakuwa na shule nyingi ( NDDT),hata kama ulishirikiana na wenzako,vijana wengi tulisoma ktk shule zile. Sijui kama ilikuwa ni juhudi yako au la,nakumbuka ulikuja kufungua RTC kijijini kwetu,porini kwelikweli. Na vituo vya afya vikawa vingi,kilimo kikawa juu,nk.
Nilikuona 1979 ukienda Makete kuweka jiwe la msingi ili eneo hilo liwe Wilaya pamoja na Ludewa ukiongozana na Sokoine (RIP),ukiwa mbunge wa wilaya yetu. Baadaye Njombe ikawa na wabunge watatu,wewe upo. Na baadae Njombe imekuwa Mkoa, wewe upo ktk usukani,hapana sasa mzee nenda kapumzike.
Wewe ndiye Mbunge pekee uliyewahi kuongoza wilaya iliyozaa wilaya mbili,bado eneo lako likazaa majimbo mawili mapya,na bado eneo lako ulilowakilisha kwa kipindi chote ukiwa Mbunge likawa mkoa. Wewe ni mzee wetu wa mkoa,nenda kapumzike kwa amani.