Neema kwa walimu, kulipwa malimbikizo

Neema kwa walimu, kulipwa malimbikizo

Mpalakugenda

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2015
Posts
4,649
Reaction score
5,074
Hatimae serikali imeamua kuwa lipa watumishi hao madai yao yasiyokuwa malimbikizo ya mashahara. Hii ni pamoja na hela za likizo. Takribani 10bn zinatarajiwa kulipwa muda wowote kuanzia sasa.

Je, hii ni kuwalegeza walimu waichague CCM ama ni utekelezaji wa serikali yetu sikivu baada ya kujionea hali ngumu za walimu huko ktk kampeni?

Mungu ibariki Tanzania.
 
Watanzania wanamuamini Magufuli, na chini ya uongozi wake mambo yatakuwa sawa na poa sana. wanaombeza narudia tena wanaombeza, iko siku watamkubali na kumpigia saruti. TUMAINI JIPYA LINAKUJA KWA WATANZANIA
 
Kwamba inawalipa 'madai yasiyokuwa malimbikizo ya mishahara'!?
Mbona kama hawajafanya kitu hapo.Maana kwa kadri nijuavyo malimbikizo ya mishahara(areas) ni pasua kichwa.
 
Watanzania wanamuamini Magufuli, na chini ya uongozi wake mambo yatakuwa sawa na poa sana. wanaombeza narudia tena wanaombeza, iko siku watamkubali na kumpigia saruti. TUMAINI JIPYA LINAKUJA KWA WATANZANIA
Magufuli hapigiwi saruti ila pushup kama hii:

JIMAMA PUSHUP.jpg
 
Kuna WALIMU wako chini ya WIZARA yaani KATIBU MKUU WIZARA YA ELIMU.hao waandikie MAUMIVU hawa mafaili yao yapo Ktk Halmashauri Ila MISHAHARA inatoka WIZARANI. HUWA ni walimu wa MWISHO kupata MISHAHARA yao.
 
Mtoa mada ameweka kichwa habari kwa mtazamo wa Neema, na amesahua kama ni haki yao, sasa tokeo lini stahiki yako ukilipwa inakuwa neema, mie ningeshauri wangedai na fidia ya ucheleweshwaji wa stahiki zao.
 
Kwamba inawalipa 'madai yasiyokuwa malimbikizo ya mishahara'!?
Mbona kama hawajafanya kitu hapo.Maana kwa kadri nijuavyo malimbikizo ya mishahara(areas) ni pasua kichwa.

hapo kwenye mabano ni double r siyo single r (arreas) tunakumbushana tu mkuu usijari
 
Mtoa mada ameweka kichwa habari kwa mtazamo wa Neema, na amesahua kama ni haki yao, sasa tokeo lini stahiki yako ukilipwa inakuwa neema, mie ningeshauri wangedai na fidia ya ucheleweshwaji wa stahiki zao.

Eti pamoja na kucheleweshewa haki zao kwa miaka mingi wanapoamua kuwalipa kwa sababu za kisiasa inaitwa "neema".
 
Hatimae serikali imeamua kuwa lipa watumishi hao madai yao yasiyokuwa malimbikizo ya mashahara. Hii ni pamoja na hela za likizo. Takribani 10bn zinatarajiwa kulipwa muda wowote kuanzia sasa.

Je, hii ni kuwalegeza walimu waichague CCM ama ni utekelezaji wa serikali yetu sikivu baada ya kujionea hali ngumu za walimu huko ktk kampeni?

Mungu ibariki Tanzania.

Tulipwe kabla ya uchaguzi bila ivo raisi ni lowasa
 
hapo kwenye mabano ni double r siyo single r (arreas) tunakumbushana tu mkuu usijari

Ni kweli kabisa kusahihishana ni jambo jema mno maana kujifunza hakuna mwisho, hapo kwenye red hiyo herufi r ingekuwa l :eyeroll1:
 
Watanzania wanamuamini Magufuli, na chini ya uongozi wake mambo yatakuwa sawa na poa sana. wanaombeza narudia tena wanaombeza, iko siku watamkubali na kumpigia saruti. TUMAINI JIPYA LINAKUJA KWA WATANZANIA

Kwani hata kikwete mwenyewe si tulimuamini,na leo hii anatuachia ajira ya kuokota makopo
 
hapo kwenye mabano ni double r siyo single r (arreas) tunakumbushana tu mkuu usijari

Mkuu katika muendelezo huo huo wa kukumbushana ni kwamba "areas" na "arreas" vyote siyo sahihi. Sahihi ni "arrears". Kama ni katika umoja ni "arrear" na wingi inakuwa "arrears".
 
Back
Top Bottom