Elections 2010 Nec wakane hili mbele ya watanzania kama wanaweza.................

urasa

JF-Expert Member
Aug 12, 2010
434
2
baada ya kusikia taarifa nyingi juu ya nec kutaka kuchakachua matokeo ya mwaka huu,kwa roho ya kizalendo na yenye kupenda mabadiliko nimeamua kuzunguka mikoa yote ya tz yenye historia ya kuipa ccm kura nyingi,nimeanzia kanda ya kati,mikoa ya dodoma na singida,jamani tuamke na tusaidiane kwenye uhuru wa kweli mwaka huu,nilipofika manyoni kabla ya kwenda singida mjini nilikutana na afisa uchaguzi mmoja ,kwenye mazungumzo naye akasema,idadi ya wapiga kura alioletewa na nec ni tofauti na aliyekuwa naye ikiwa ina maana nec wameongeza,sasa wamewaongeza toka wapi na kwa manufaa ya nani?hapa singida maafisa wote wa uchaguzi ni wagumu kukupa idadi ya wapiga kura watarajiwa,na nyepesi zilizopo ni kwamba singida ni moja ya mikoa ambayo atatumiwa na ccm kufanya uhuni,plz wazalendo tuzunguke nchi nzima kufuatilia hili,pamoja tutashinda
 
kwa kweli kama tunataka ukombozi lazima tushirikiane katika hili, maana ukombozi sio lele mama PAMOJA TUTASHINDA
 
Pamoja ya kwamba data ulizoleta ni mhimu na zinahitajika sana, nafikiri hujamtendea haki huyo afisa uchaguzi kwa kutaja jina lake na kuweka namba yake ya simu hapa. Unaweza kumsababishia matatizo. Au umesahau kwamba CCM ni chama cha visasi na mauaji? Hawataona shida kumpiga risasi hawa! Mlinde jamaa yako aliyekupa hizo data.
 
Hapo ni wizi kwa kwenda mbele, maeneo kama Simanjiro,Bumbuli,lLindi,Mtwara na kwingineko ambapo kuna wabunge waliopita bila kupingwa na ambapo CCM haina upinzani mkubwa lazima uchakachuaji mkubwa wa kura uwepo .Mimi ninaamini wapo watu wengi tu waliochoshwa na CCM na hawataki kumpa kura JK wala Mbunge japo alishapita,nimeshuhudia mwenyewe. Mimi nashauri CHADEMA wajipange na kutodharau kupeleka mawakala katika maeneo kama hayo hata kama hakuna mgombea kwani kuna kura nyingi tu zipo kwa Slaa na mimi nimeona,kwa mfano Simanjiro..wakazi wengi maeneo ya makao makuu ya wilaya na kwenye kata karibuni kumi na tatu pamoja na kuwa hamna mgombea yeyote wa upinzani lakini kuna watu wengi wanataka kumpigia kura Dr Slaa,hasa wafanyakazi serikalini,waalimu na wahamiaji (wasio masai).

Pia TABORA Mjini,pamoja na kwamba hakuna mgombea wa Chadema katika ubunge, lakini mwamko ni mkubwa mno keeping in mind ni eneo la mjini so watu wameelimika na katika pitapita zangu,wengi wanatarajia kumpa kura Dr Slaa. Hivyo kama CHADEMA haitopeleka mawakala maeneo kama hayo nchi nzima,wategemee SIFURI hata kama wamepata kura kiasi gani..KUMBUKA 50 HUANZA NA 1.
 
baada ya kusikia taarifa nyingi juu ya nec kutaka kuchakachua matokeo ya mwaka huu,kwa roho ya kizalendo na yenye kupenda mabadiliko nimeamua kuzunguka mikoa yote ya tz yenye historia ya kuipa ccm kura nyingi,nimeanzia kanda ya kati,mikoa ya dodoma na singida,jamani tuamke na tusaidiane kwenye uhuru wa kweli mwaka huu,nilipofika manyoni kabla ya kwenda singida mjini nilikutana na afisa uchaguzi mmoja ,kwenye mazungumzo naye akasema,idadi ya wapiga kura alioletewa na nec ni tofauti na aliyekuwa naye ikiwa ina maana nec wameongeza,sasa wamewaongeza toka wapi na kwa manufaa ya nani?hapa singida maafisa wote wa uchaguzi ni wagumu kukupa idadi ya wapiga kura watarajiwa,na nyepesi zilizopo ni kwamba singida ni moja ya mikoa ambayo atatumiwa na ccm kufanya uhuni,plz wazalendo tuzunguke nchi nzima kufuatilia hili,pamoja tutashinda

Na hii ndio breaking news?
 
Back
Top Bottom