NEC itoe suluhu kwa hizi chaguzi ndogo ndogo

NEC itoe suluhu kwa hizi chaguzi ndogo ndogo

Joined
Sep 4, 2012
Posts
26
Reaction score
5
Kwa hesabu za haraka haraka NEC imekua busy mwaka hadi mwaka kwa kuandaa chaguzi ndogo ndogo kila kukicha za udiwani au wabunge wanaojiuzulu nawasikilizia zao kwa sababu wajuao wao.

Ni wakati NEC kulitizama hili na kuja na jibu mbadala la kuokoa kiasi kikubwa kinachotumika kuitisha uchaguzi Mwingine either kwa kutengeneza pendekezo la kisheria litakaloipa nguvu Chama cha mbunge au diwani husika kumweka mbadala wa aliyejiuzulu kutoka Chama husika ili kuokoa kiasi cha pesa kinachopotea ili kufanya kazi nyingine za maendeleo. Ni jasho LA wananchi wanaolilia afya Bora, elimu, miundombinu ya kilimo Bora, umeme, maji , .

Mwenyekiti wa NEC litizame hili Mara mbilimbili kwa macho ya kumsaidia mtanzania anayelia maisha magumu.
 
Last edited:
Ndugu Kasambala Junken maliki kura 23 elfu, ndugu Fahim Dovutwa kura 18 elfu n.k - In Jaji Lubuva's voice
 
Mkuu mleta uzi ndio umetoka jela nini? Huyo Lubuva ameshastaafu. Wanaoweza kubadilisha hizo sheria wanafaidika na hizo chaguzi hivyo usitarajie kubadilishwa chochote.
 
Ajaelewa chombo hicho kwa sasa kinaongozwa na nani?msimlaumu,ni kumuelimisha tu.
 
Kwa hesabu za haraka haraka NEC imekua busy mwaka hadi mwaka kwa kuandaa chaguzi ndogo ndogo kila kukicha za udiwani au wabunge wanaojiuzulu nawasikilizia zao kwa sababu wajuao wao.

Ni wakati NEC kulitizama hili na kuja na jibu mbadala la kuokoa kiasi kikubwa kinachotumika kuitisha uchaguzi Mwingine either kwa kutengeneza pendekezo la kisheria litakaloipa nguvu Chama cha mbunge au diwani husika kumweka mbadala wa aliyejiuzulu kutoka Chama husika ili kuokoa kiasi cha pesa kinachopotea ili kufanya kazi nyingine za maendeleo. Ni jasho LA wananchi wanaolilia afya Bora, elimu, miundombinu ya kilimo Bora, umeme, maji , .

Mh LUBUVA litizame hili Mara mbilimbili kwa macho ya kumsaidia mtanzania anayelia maisha magumu.
Tukitaka njia za mkato tutakwama.

Wengine tunaweza kupendekeza kuwa kwa sababu mbunge/diwani yupo (hakufa) basi aruhusiwe kuhama chama na kuendelea na ubunge/udiwani wake bila ya uchaguzi.

Tumechagua kufuata hii demokrasia ya vyama vingi. Demokrasia ina gharama zake na ndio hizi tunazoziona sasa.

Lakini naona hili ni jambo la mpito tu.

Kwa sasa upinzani wamevurunda sana ndio maana tunaiona hii hama hama. Upinzani ukiimarika tutaiona stability na hakutakuwa na hama hama holela kama hizi.
 
Back
Top Bottom