Lu-ma-ga
JF-Expert Member
- Sep 21, 2010
- 4,780
- 3,227
kwanza nashukuru sana kwa kuleta suala hili. Sheria mpya ya madini inataka leseni mpya zote zitakazotoka chini ya sheria ile serikali iwe na hisa kwenye mgodi husika kwa kuanzia asilimia 15(free carried). Pia sheria mpya iliyotungwa kutokana na mapendekezo ya kamati ya bomani imeweka masharti mapya ya leseni na mfumo wa kodi.
Natumai waziri kivuli wa nishati na madini ndugu john mnyika ataweza kueleza nini hasa kimetokea kwenye mgodi wa north mara.
Sio hivyo tu, kampuni ya mantra pia imepewa leseni ya maalumu ya kuchimba urani wakati bado hawajalipa capital gains tax yetu kufuatia mgodi mradi kununuliwa na warusi.
Sijui prof muhongo ana maelezo gani kuhusu suala hili maana yeye ndie mtoa leseni kwa mujibu wa sheria
aulizwe mnyika kwani mnyika ndo serikali????? Zitto acha hizo kaka umenyea kambi tayari