ngongoti2000
JF-Expert Member
- Nov 20, 2017
- 2,235
- 2,123
Ukweli ni kwamba huyo mwanaume wala hakuhitaji
Ujue kuna tofauti ya kupenda na kuhitaji
Inawezekana anakupenda ila matendo yake yanaonyesha hakuhitaji
Kama huna kazi tafuta kazi or business taratibu ukishaweza kujitegemea ondoka tu hapo
Unavyozidi kuumia kuna siku unaweza kumuumiza huyo wifi yako alafu ndo mambo yazidi kuwa mabaya
Pole sana aisee
Habari,
Hili jambo limenitesa miaka nenda miaka rudi, natamani lifike mwisho.
Wakati naingia kwenye mahusiano na huyu ambae ni mume wangu sasa, alikuja binti mmoja ambaye alikuwa ndo kamaliza form 4 (mdogo wake) akaanza kusoma cozi kwenye chuo flani.
Nikapata ujauzito so ikabidi nilete binti wa kazi. Na mimi katika maisha yetu nimelelewa na mabinti wa kazi, sipendi wateseke kabisa maana niliona walivyomsaidia mama enzi tunakua, so shida ikaanza anamuachia yule binti kila kitu afanye, hadi ampikie amuamshe chumbani, yale mambo yalikua yananikera nikaanza kumsema kwa nguvu sana, hakubadilika. Ikabidi nimwambie kaka yake. Kaka yake akasema kama unamuona msichana wako anapata shida basi nitamuekea msichana wake yeye
Ile hali ikaendelea sana kwa muda na yule binti alikua mdogo kwa hiyo ikabidi niwe napika mwenyewe, siku zikaenda akaja tena mdogo wake wa kiume, wote kazi ikawa ile ile, huyu wa kiume hadi anamwambia dada amfulie nguo. Nilikua naongea napiga mzigo nadeki mpaka mimba ina miezi nane ndo mama angu akaja.
Kiukweli niliteseka mimba ya huyu mtoto, ugomvi ndani ya nyumba hautuliii kabisaa; wakaungana wote na mama zake kwamba niachike. Na kweli mume wangu akasema natamani kukuacha ni vile tu tumefunga ndoa.
Hapo nimeskip kipindi cha ndoa maana tulifunga ndoa tayari huyu binti tunaishi nae kuna mengi yalitokea lakini nitaeleza tu tukio moja.
Usiku wa kesho yake ndio ndoa akaniambia kwa hiyo kwenye hiyo saluni uliyofanya booking na mimi nitasuka? Nikamwambia ni maids tu wewe hautaenda pale, aliangua kilio imagne na kuna wageni, mume wangu haya maswala ya maids hajui anasema kwanini unaenda kuremba watu baki unamuacha huyu? Akaninuia tumeenda kusameshana wakati wakuvalishana pete ya ndoa.
Unaweza ukahisi movie ila sio movie ni maisha watu tunapitia.
Wakati wa sherehe huyu binti na wenzake kwenye ile meza ya wazazi wangu hawakupeleka vinywaji kabisa maana wao ndo walikua kwenye hiyo kamati ya vinywaji na mama zake wadogo.
Sasa huyu binti alikuja baadae kwenda hostel mimi mimba ikiwa kubwa kama miezi 8 ambapo na mama ndo akaja. Sasa wakati wa X-mass maana ilikuwa hata bado sijajifungua kaka yake akampigia simu aje kula sikukuu nyumbani, hakuja kabisa akaenda kwa dada mmoja ambae alikuja baadae kuwa mtu wa karibu na mimi. Huyo dada akamwambia mbona hujaenda kwa kaka kula sikukuu? Akasema, KAJAZA NDUGU ZAKE SIWEZI KWENDA PALE.
Kiukweli alikua kaja mama yangu na mjukuu wake na mdogo wangu, alikuja kusalimia, nikihesabu muda kwa ujumla waliokaa pale ni kama wiki tatu, dogo akaondoka na mimi nikawa nimejifungua nikakaa wiki2 nikaondoka na mama kurudi nyumbani.
Sasa imagne watu hawajakaa hata mwezi yeye kaona kero ila wenyewe miaka nenda rudi wapo.
Alikuja kumaliza chuo ila hakupata kazi, akaenda kwao akarudi tena akasoma tena akamaliza hakupata kazi. Na hii ya mara ya pili, wembe ukawa ule ule, hafanyi chochote analala tu dada amfanyie kila kitu.
Sasa hii mara ya tatu anasoma tena ila anawahi kuondoka asubuhi jion kuna siku anachelewa kuna siku anawahi kurudi, ila ndo hivyo hasaidii chochote, yaani dada ndo afanye kila kitu.
Namuuliza anasema naoshaga sahani yangu pekee. Namuuliza na hivyo vingine anasema nawahi kuamka kwa hiyo siwezi.
Leo mpaka naandika niko bize napika yeye amekaa anachat, nikamwambia mimi siwez kukupikia wewe unachat hapo jipe shuhuli wala hajanisikia kitu. Kaenda kununua chips.
Mbaya zaidi nyuma ya pazia kuna rafiki yake mume wangu wametafutana wanapanga yao huko (na huyo kaka alihusika sana kwa yule baby mama wa mr kumuondoa)
Na kingine kikubwa ni kwamba mama yake anaona kawaida tu hata ukimwambia.
Ashawahi iba nguo zangu akaenda kugawa, aliyempa akapiga picha akaweka Insta nikaiona ile nguo nikambana akasema alimpa, nikamwambia akaifate akampigia mama ake na mama ake akasema muulize (yaani aniulize mimi) hiyo nguo ni bei gani atume ela.
Nimeruka mambo mengi ila kuna dada wa saluni pia alishawahi kuniita akaniambia kuwa makini na huyu binti anaweza akakuua.
Sasa ndugu zangu nifanyaje hapa, wako wawili yeye na huyo shemeji wote wanataka tuwahudumie kama ambavyo namuhudumia kaka yao yaani mimi na dada ndo tuwafanyie kila kitu.
Na kingine kikubwa ana mawasiliano ya karibu mno na yule dada aliyezaa na mume wangu pamoja na yule aliyehusika kupika figisu.
Nifanyaje kuimaliza hii nightmare wandugu maana kila nikimuona anapita nakumbuka machungu hasa enzi za mimba maana ilikua niachwe kwa sababu yake.
Roho inaniuma, nina uchungu sana
=======
Michango ya wadau
Kwahiyo we unaona ni sawa akae hapo ilhali inaonekana kabisa mumewe hamuhitaji?Huu ni ushauri wa mwanamke anayeachika kila kukicha kwenye ndoa. Shameful kwa kweli. Kama ushauri ndiyo huu basi hapo hakuna ndoa tena
Sent from my iPhone using JamiiForums
Kwanza nikupe pole mdada. Mi ninachoona hapo jamaa anashindwa kubalance maamuzi kati ya ndugu na wewe mkewe. Sasa cha kufanya fanya kama upate kalikizo hivi omba ruhusa ukakae kwenu kwa muda fulani hivi hata miezi mitatu. Mara nyingi thamani ya kitu huwa inaonekana wakati hakipo utaona tuu mabadiliko then ataelewa vizuri na atakusikiliza na atasimama kama mwanamume.Habari,
Hili jambo limenitesa miaka nenda miaka rudi, natamani lifike mwisho.
Wakati naingia kwenye mahusiano na huyu ambae ni mume wangu sasa, alikuja binti mmoja ambaye alikuwa ndo kamaliza form 4 (mdogo wake) akaanza kusoma cozi kwenye chuo flani.
Nikapata ujauzito so ikabidi nilete binti wa kazi. Na mimi katika maisha yetu nimelelewa na mabinti wa kazi, sipendi wateseke kabisa maana niliona walivyomsaidia mama enzi tunakua, so shida ikaanza anamuachia yule binti kila kitu afanye, hadi ampikie amuamshe chumbani, yale mambo yalikua yananikera nikaanza kumsema kwa nguvu sana, hakubadilika. Ikabidi nimwambie kaka yake. Kaka yake akasema kama unamuona msichana wako anapata shida basi nitamuekea msichana wake yeye
Ile hali ikaendelea sana kwa muda na yule binti alikua mdogo kwa hiyo ikabidi niwe napika mwenyewe, siku zikaenda akaja tena mdogo wake wa kiume, wote kazi ikawa ile ile, huyu wa kiume hadi anamwambia dada amfulie nguo. Nilikua naongea napiga mzigo nadeki mpaka mimba ina miezi nane ndo mama angu akaja.
Kiukweli niliteseka mimba ya huyu mtoto, ugomvi ndani ya nyumba hautuliii kabisaa; wakaungana wote na mama zake kwamba niachike. Na kweli mume wangu akasema natamani kukuacha ni vile tu tumefunga ndoa.
Hapo nimeskip kipindi cha ndoa maana tulifunga ndoa tayari huyu binti tunaishi nae kuna mengi yalitokea lakini nitaeleza tu tukio moja.
Usiku wa kesho yake ndio ndoa akaniambia kwa hiyo kwenye hiyo saluni uliyofanya booking na mimi nitasuka? Nikamwambia ni maids tu wewe hautaenda pale, aliangua kilio imagne na kuna wageni, mume wangu haya maswala ya maids hajui anasema kwanini unaenda kuremba watu baki unamuacha huyu? Akaninuia tumeenda kusameshana wakati wakuvalishana pete ya ndoa.
Unaweza ukahisi movie ila sio movie ni maisha watu tunapitia.
Wakati wa sherehe huyu binti na wenzake kwenye ile meza ya wazazi wangu hawakupeleka vinywaji kabisa maana wao ndo walikua kwenye hiyo kamati ya vinywaji na mama zake wadogo.
Sasa huyu binti alikuja baadae kwenda hostel mimi mimba ikiwa kubwa kama miezi 8 ambapo na mama ndo akaja. Sasa wakati wa X-mass maana ilikuwa hata bado sijajifungua kaka yake akampigia simu aje kula sikukuu nyumbani, hakuja kabisa akaenda kwa dada mmoja ambae alikuja baadae kuwa mtu wa karibu na mimi. Huyo dada akamwambia mbona hujaenda kwa kaka kula sikukuu? Akasema, KAJAZA NDUGU ZAKE SIWEZI KWENDA PALE.
Kiukweli alikua kaja mama yangu na mjukuu wake na mdogo wangu, alikuja kusalimia, nikihesabu muda kwa ujumla waliokaa pale ni kama wiki tatu, dogo akaondoka na mimi nikawa nimejifungua nikakaa wiki2 nikaondoka na mama kurudi nyumbani.
Sasa imagne watu hawajakaa hata mwezi yeye kaona kero ila wenyewe miaka nenda rudi wapo.
Alikuja kumaliza chuo ila hakupata kazi, akaenda kwao akarudi tena akasoma tena akamaliza hakupata kazi. Na hii ya mara ya pili, wembe ukawa ule ule, hafanyi chochote analala tu dada amfanyie kila kitu.
Sasa hii mara ya tatu anasoma tena ila anawahi kuondoka asubuhi jion kuna siku anachelewa kuna siku anawahi kurudi, ila ndo hivyo hasaidii chochote, yaani dada ndo afanye kila kitu.
Namuuliza anasema naoshaga sahani yangu pekee. Namuuliza na hivyo vingine anasema nawahi kuamka kwa hiyo siwezi.
Leo mpaka naandika niko bize napika yeye amekaa anachat, nikamwambia mimi siwez kukupikia wewe unachat hapo jipe shuhuli wala hajanisikia kitu. Kaenda kununua chips.
Mbaya zaidi nyuma ya pazia kuna rafiki yake mume wangu wametafutana wanapanga yao huko (na huyo kaka alihusika sana kwa yule baby mama wa mr kumuondoa)
Na kingine kikubwa ni kwamba mama yake anaona kawaida tu hata ukimwambia.
Ashawahi iba nguo zangu akaenda kugawa, aliyempa akapiga picha akaweka Insta nikaiona ile nguo nikambana akasema alimpa, nikamwambia akaifate akampigia mama ake na mama ake akasema muulize (yaani aniulize mimi) hiyo nguo ni bei gani atume ela.
Nimeruka mambo mengi ila kuna dada wa saluni pia alishawahi kuniita akaniambia kuwa makini na huyu binti anaweza akakuua.
Sasa ndugu zangu nifanyaje hapa, wako wawili yeye na huyo shemeji wote wanataka tuwahudumie kama ambavyo namuhudumia kaka yao yaani mimi na dada ndo tuwafanyie kila kitu.
Na kingine kikubwa ana mawasiliano ya karibu mno na yule dada aliyezaa na mume wangu pamoja na yule aliyehusika kupika figisu.
Nifanyaje kuimaliza hii nightmare wandugu maana kila nikimuona anapita nakumbuka machungu hasa enzi za mimba maana ilikua niachwe kwa sababu yake.
Roho inaniuma, nina uchungu sana
=======
Michango ya wadau
Sijui bado kama una hii ndoa.mbaga jr,
Nimepata mateso sana jamani, sasa ukiongea anasema ataleta msichana mwingine wa kazi kwa ajili ya ndugu zake.
Sidhani kama bado ipo aiseeeh.Hii ndoa inaendeleaje?
Yani anahadithia kama kwamba wana pumzi yake.Mi sielewi huwa mnajing'ang'aniza Nini?
Yaani uko katika ndoa Kama slave
Huna terms zako unanyanyaaswa tu .
Hivi huwezi ondoka hapo ukaishia maisha yako .
Hiyo mume ulizaliwa nae
Ukaa na wapuuzi unavumilia tu
Raha hope mwenyewe hao huwezi wabadili
Tafuta namna ya kuishi bila msaada wa huyo mmeo .
Usiwe mzembe
Ahahaa Kuna possible ashaongeza watoto.Yani anahadithia kama kwamba wana pumzi yake.
Mi naona a very drown person kwa kweli.
Ndoa gani ina excel kwenye hii hali aiseeeh.
Sijui hata wanapeanaje utamu.
Sijui kwa kweli.
Kuna namna tu kuna vitu unafanyiwa lazima mwili akili na roho viondoke mahali hapo.
Usikute kashaongeza watoto wake watatu.
Na hapa sa hiz atakwambia hawezi ONDOKA wanae ni wadogo.
Nashindwa kuzuia hasira zangu, nishaurini nifanyeje wadau.
AhahahahahhahahaHii ndoa bado ipo???
Ndoa oliyofikia hapa.Nimepitia message yako nikaona una kitu ambacho mme wako hakijui ila ukiondoka atakijua. Mwanamke asili zake ni kuvumilia ila uvumilivu ukiisha basi ni tatizo ambalo haliwezi kuisha.
Na huyo wifi yako sijui ataolewa na mwanamme gani maana anachofanya yeye kwako ajue wazi nae atafanyiwa ila apate nafasi ya kujua kiasi gani alikuumiza uzuri Mungu huwa hakawiii wala kuchelewa kujibu kilio cha wamchao na kuomba kwa imani.
Ushauri wangu usiondoke ila muombe Mungu na kama ulifunga ndoa basi washenga jukumu lao ndo hilo la kuilea ndoa hiyo kiimani
Na ndo huwa hivyo na hakuna ANAYEJALIKwanza nimpongeze huyo mwanaume kwa kupata mke mwema. Kimsingi kwa ulimwengu wa leo kumpata mwanamke wa Kariba yako ni nadra Sana. Kiufupi Mungu atakulipa, daah pole.
Daah, kiufupi jamaa kashindwa ku_control ndg zake kwenye ndoa yake( yenu) na ninachokiona ni:
1. Ndoa inaweza haribika (ampapo yeye ndio looser zaidi),
2. Maendeleo ya familia yenu(ndoani) yatachelewa au yasiwepo kabisa. Kwa maana sasaivi sidhani Kama mnashishikishana Mambo ya maendeleo ya familia yenu.
Mwisho lakin si kwa umuhimu, hayo anayofanya mmeo asidhani anakukomoa wewe BALI wanenu(malaika wa Mungu).